Sijakuelewa. Mleta uzi anasema Arobaini ni Kesho tarehe 26/3/2023 kwa hiyo hiyo tarehe ni namba tu. nisije kuchanganya kumbe uzi umefufuliwa ni wa siku nyingi
Hii ni kudhihirisha kuwa kwenye simu ya Mwabukusi kuna mauudhui ambaye hakutuma kabla na yatumwa sasa. Unless video zinazotumwa muongeaji ni cloned Mwabukusi.
waliokuwa WANASIMAMA majukwaani na kutuhakikishia IMEUZWA, Sasa wamegeuka. Toka jana nimeanza kuwasikia wakiseme wanataka waelezwe UKWELI sababu "WANASIKIA" imeuzwa mara imebinafsishwa mara imekodishwa. Yaani sasa hanajidai hawana uhakika na walichokuwa wakiwaaminisha wananchi ktk mikutano yao.
Hoja mwanasheria wetu wa ujerumani anatuambia IGA ndio HGA na tumeingia chocho kuaminishwa hivyo. Mikataba yenye usiri ni hatua ya tatu mikataba ya TPA na Mukodishwaji ambayo wambunge wana access nayo wakiihitaji.
Hakuna huo mkataba HGA humu. Uliosainiwa/unaojadiliwa na uliopo humu ni wa IGA. HGA ni mkataba wa pili unaojadiliwa na utasainiwa baada ya kuidhinishwa kwa IGA.
Nimemsikia huyu mwanasheria wa Ujerumani. Anasema huu Mkataba tunaoujadili sasa ni wa Host Government Agreement (HGA). Wenzangu mmeuona huo mkataba nimetafuta sijauona. Umeingiwa lini halikuwa mazungumzo ya HGA yalikuwa yakisubiri kuridhiwa kwa IGA?
Swali ni gumu, tuendelee kutafiti. Kwa mahesabu ya uumbaji ktk Biblia uzao wa Adamu ni miaka 7,000 iliyopita hali kuwa leo kuna ugunduzi wa mafuvu yenye zaidi ya umri huo. Inawezekanaje haya?
Binafsi nauona usaliti, usaliti uliofanywa na waliofungua kesi na mawakili wanaojidai kuwatetea walalamikaji. Naita usaliti saba kesi hii haikutakiwa kufunguliwa, ilatakiwa nginja nginja hii waachiwe wanahatakati na wanasiasa. Naita wasaliti sababu ikitojea maamuzi ya mahakama ikawapa ushindi...
Siasa za Tanzania za sasa hicho ni kitu cha kawaida sana. Uliwahi tarajia Mkiti wa CCM wa Taifa anaweza ibukia kwenye Kingamano la Chadema na akahutubia? au Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kwenda kuhutubia mkutano wa hadhara wa ACT zanzibar? Ni miujiza ya sasa ya Tanzania mpya.
Hoja zenyewe kama ndio hizi nani ana haja ya kusikiliza
Nimemsikiliza Mwenyekiti wa Chama/Muandaaji wa Mkutano kwa ajili ya kuto elimu ya Mkataba wa Bandari toka mwanzo hadi mwisho sijasikia akisoma au kueleza kifungu kibovu cha mkataba zaidi ya salamu hii kwa watanzania,
Mpaka sasa sijaona muandishi anayechambua nini chanzo au sababu ya hii hukumu! Kesi hii imesikilizwa toka lini? Ilihusu kosa gani na aliifungua nani? Nini maana ya maamuzi ya hukumu hiyo? Madeleka alikuwa Mahakamani maana yake alienda mwenyewe akijua ni siku ya hukumu kutolewa, kama mwanasheria...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.