Pengine historia itatuhukumu. Lakini udikteta wa aina yeyote kamwe hauwezi, na wala hautakuwa, Value: Dictatorship is not a value - YouTube
Siku njema,
LSM
Kitendo cha kulifungia gazeti la MwanaHALISI ni cha kusikitisha na kinastahili kulaaniwa na wanademokrasia wote walitakiao mema taifa hili. Lakini wakati huo huo sharti pia tulaani Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976. Kwa maana, bila ya sheria hii, pengine leo hii tusingelikuwa na hali hii.
Mphw! Makala haya yanazidi kuonyesha haja ya Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kuondolewa 'Kinga ya Katiba' na Bunge, ili aweze kufunguliwa mashtaka kuhusu vitendo vya rushwa vilivyoshamiri chini ya uongozi wake. Ni muhimu hili lifanyike ili liwe kama fundisho kwa viongozi wa baadaye kutofanya...
Hivi Tanzania inapata kipato kikubwa kutoka balozi zake zilizoko nchi za nje? Je, nikutokana na kipato hicho kinachogharamia ununuzi wa majengo ya kibalozi huko nchi za nje au..? Je, baada ya ununuzi wa majengo hayo, kipato kinachobaki hutumikaje? Je, balozi zetu zina madeni ambayo bado...
Ndugu Maundumula, kuna dhana kwamba kheri kukataa neno kuliko kutaa wito. Na siyo mara nyingi watu kuwa arresting officers katika kesi inayo wahusisa wao. Katika mazingira ya namna hii, binafsi ninaridhika kwamba uwezo wa Ndugu Musendo kufungwa kwa mashtaka ya kughushi ni mkubwa mno kuliko...
Katika demokrasia ya kikatiba kuna kile kinachofahamika kama Penal Proportionality ambapo adhabu hupashwa ilingane na kosa linalodaiwa kutendeka. Kwa hiyo, inashangaza kwamba mtu anayedaiwa kupokea rushwa ya Tsh 100.000 anaweza kupata adhabu sawa na Afisa Mwandamizi wa benki (BoT), aliyehusika...
Ndugu Mukandara,
Hoja yako kuhusiana na maada hii ni ya msingi kabisa. Kama alivyoeleza Ndugu Soby, Tanganyika ilikuwa Mandated Territory. Hii inamaanisha Jamii ya Kimataifa (wakati huo League of Nations) iliipa Uingereza madaraka ya kisheria ya kuindesha Tanganyika kwa niaba yake hadi hapo...
Ta Muganyizi, waitu onganyile, okuba: tafadhali, kama unaweza, ninakuomba unipe rejea ya gazeti lililochapisha habari hizi kunako majuma matatu yaliyopita. Sikulisoma na ningelihitaji kusoma makala yote, kama yalivyochapishwa. Aidha, ningelikuomba unipe jina la gazeti hilo na/au, ukiweza...
Ndugu Bongolander,
Hata Mlowezi Ian Smith, wa Rhodesia (Zimbabwe), alipata kunena kwamba mtu mweusi kamwe asingelitawala nchi hiyo katika kipindi cha miaka 100. Of course, mwenzetu 'Uncle Bob' i.e. Robert Gabriel Mugabe, ametawala (na anaendelea kutawala) nchi hiyo hata kabla ya robo ya kipindi...
Tikerra,
Ninadhani misingi, au 'UTU', anaouzungumzia Mzee Mwanakijiji (na wengine waliochangia mada hii) ni values ambazo huwa ni msingi wa kulisimika taifa-hali. Misingi hiyo mara nyingi huwa haina uhusiano wa karibu na itikadi za vyama katika jamii ya kisiasa. Na, ingawaje, katika jamii hiyo...
Mzee Mwanakijiji,
Katika muktadha wa hoja yako, inaelekea misingi ya taifa unayoizungumzia ni ile inayofahamika kwa wengi katika lugha ya Kingereza kama values (au maadili). Mataifa ambayo yameendelea, yamefanya hivyo kwa kuwa yamejengwa kwenye misingi ya kudumu; misingi ambayo huwa ni injini...
Ndugu Taso, shukrani nyingi. Naam, mimi ndiye mtunzi wa kitabu hicho. Huo ni upande mwingine wa Awamu ya Kwanza ambao wakati huo ulikuwa hauelezwi kinagaubaga, kadamnasi. Ninamshukuru Mwenye Uweza, nilisurvive kipindi hicho cha giza jambo ambalo linanilazimu kukizungumzia kipindi hicho ili walao...
Jambo hili ni mojawapo ya matatizo ya Muungano. Lakini pia kuna jambo jingine: Wanasiasa kutoka Zanzibar wanaweza kushika madaraka ya juu nchini Tanganyika, lakini Mtanganyika hawezi kufanya hivyo huko Zanzibar. Hata Rais Mtanganyika (ambaye ndiye Rais wa Muungano) haitawali Zanzibar na wala...
Facts?! Ni serikali yenyewe iliyotoa madai hayo iliyopashwa kutoa hizo facts na wala siyo mimi au hao serikali iliodai siyo raia. Ukweli ni kwamba, wote kama raia wa Tanzania, wamelitumikia taifa hili katika nyadhifa mbalimbali na kwa moyo mkunjufu. Au na hilo unabisha? Iweje tena wasiwe raia...
Lakini Ndugu Malecela, wapo Watanzania kadhaa wanaoheshimika kutokana na mchango wao mkubwa kwa taifa hili, lakini ambao waliwahi kutangazwa kwamba wao siyo raia. Leo hii tunafahamu kwamba madai hayo (ya serikali) hayakuwa na ukweli wowote bali zilikuwa ni njama za kisiasa dhidi ya watu hao. Je...
Ndiyo, Ndugu Utingo.
Inawezekana likawa tatizo kubwa kitaifa kuliko tunavyodhani. Inawezekana wapo watu wenye shahada kutoka mikoa mbalimbali lakini msingi wa elimu yao ya mwanzo na sekondari ina mushkeli kama kesi hii inavyoonyesha.
Nadhani kijana Hamis Andrea akipata msaada wa kisheria...
Dr Kingwangalla,
Tuhuma nzito dhidi yako ni kuwa hukufaulu mtihani wa kwenda shule ya sekondari. Badala yake inadaiwa kuwa ulitumia jina la kijana aliyekuwa amefaulu, Hamis Andrea, kuendelea na masomo Shule ya Sekondari Kigoma. Yeye hakufahamu matokeo ya mtihani huo, lakini nyinyi mliofahamu...
Ndugu Nyandaigobeko,
Sababu ya wananchi kuiogopa sana serikali yao lakini bila serikali yenyewe kuwaogopa raia wake inatokana na kutokuwepo usawa wa madaraka baina ya serikali na raia wake. Ni suala la mpangilio wa Katiba yetu lililozaa utamaduni-sugu wa viongozi kutopenda kuwajibika kwa wanao...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.