Wapo mchanganyiko. Wasomi wa UD,CBE, USTAWI NA IFM wanapanua sana pale. Kuna vijumba wanaviita hostel karibu na pale. Njaa inawaua na pia wanataka kula raha zaidi ya uwezo wao.
Hao mabalozi wanasumbuliwa na njaa. Kama walidhani fedha waliyopewa itakuwa ya kudumu wamekwisha kabisa. Hawa ndio waliolia Rostam alivyotoka. Waende waendako hata SAU waende tu.
CDM hawamuwezi huyo kamanda wa Maswa. Kwanini anaongea bila wasiwasi na viongozi wanakosa majibu. Ujanja wa Mbowe na Slaa umekwama hapo. Huo ni mwiba mkali na mchungu kama mgao wa umeme Mwanza.
Msafara unakuwa mrefu kwa sababu ya idara mbalimbali zinazohusika na msafara huo. Kama atatembelea secta 10, basi tegemea wakuu wa idara hizo watakuwepo kutoa maelezo au hoja. Tusitangulize suala la mlo tu katika masuala ya kitaifa.
Igunga bila Rostam inaweza kuwa Imara zaidi. Hana mchango wowote bungeni. Siku zote yuko kimya. Aende na ashauri wenzake waharakishe kuvua magamba. Wakichelewa watatinduliwa.
Kweli sasa anataka kuvaa viatu vyake. Ubunge ndiyo saizi yake. Uraisi hata ajaribu mara mia hatapata. Itaishia kuchoka kama Mrema Lyatonga mwana wa kiraracha.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.