tafadhali nyie raia jadilini hili la kubenea/makonda mkiwa waelewa.
mawio siyo gazeti la kubenea bali mali ya victoria media servises. kumbe kwanza tafuteni wakurugenzi wa victoria media services kabla ya kukurupuka kwamba kubenea amelitumia vibaya gazeti lake. that is one.
two. gazeti lina...
:angry: mnazungumzia musoma technical high school! ndiyo ipi hiyo tena? au mna maana ya musoma alliance secondary school (mass) iliyopo nyarusuria karibu na kambi ya wakoma walikosoma akina mabere marando, mukandala wa chuo kikuu, jaji kipenka musa, nyaronyo kicheere, philip marmo, prof. katunzi...
rais kikwete alishindwa urais siku aliyowaita wezi wa epa akakutana nao (mahali sipajui) ila alitangazia umma kuwa alikutana nao na kuwaomba warudishe pesa walizokwiba! siku ile ndipo aliposhindwa urais/utawala. huwezi kuongea na mwizi ukimwomba arushe mali aliyopora huku unafunga na kunyonga...
:lol:nyaronyo hashangai kutoteuliwa mkuu wa wilaya bali ametumia makala hayo kueleza kuwa wanaoteuliwa ukuu wa wilaya ni wale wanaojikomba. pia ameeleza kuwa mbinu ya kuwahonga wandishi wa habari na vyeo hasa ukuu wa wilaya itasababisha wandishi sasa washindane kuandika habari za kuwasifia...
kumpenda magufuli ni sawa na kumpenda mzee wa nji hii kutoka kiraracha marangu kilimanjaro. kwani aliyenunua boti mbovu ya kuvutia panton za kigamboni iitwayo rescue ni nani? je boti hiyo imewahi kufanya kazi yoyote tangu inunuliwe? mbona iko juu ya mchanga pale feri na bado magufuli...
rais ateue mawaziri asiteue mawaziri hii shauri yake kwani sitegemei kupata waziri yeyote mzuri. kwa utamaduni wetu pale magogoni, rais atatakiwa na wenzake kuteua wabunge kutoka kwenye kapu lilelile la ccm ambalo ni sawa na kumtaka rais achague embe moja bivu kutoka kapu la maembe mabichi...
kwani wakenya wanalalamikia nini? si ni wao waliofungua malalamiko kuzuia barabara ya serengeti kuwa itaharibu ikolojia ya mbuga hiyo maarufu ulimwenguni eti nyumbu wakakoma kuhama tena? sasa magari mengi wanayotaka kusafirishia watalii kuja serengeti hayatazuia nyumbu kuhama? why this double...
:lol: mimi nashangaa sana kila ninapokwenda mahakamani nakuta wanasheria wamevalia mara suti nyeusi na shati jeupe, mara suti nyeusi na shati la bluu iliyokolea, mara wavae vitambaa vyeupe shingoni, mara niwakute wameniga tai nyeusi na kadhalika. hivi rasmi hasa mavazi rasmi ya wanasheria na hao...
:lol::lol:nimestushwa, nimesikitika, nimehuzunika na sasa nimeduwaa na sina la kufanya kwa chadema na tanzania kuondokewa na mwanamapinduzi huyu kijana mbichi, regia. regia mtemanenda kwa amani, lala salama, nasi tupo njiani tunakuja kwani hiyo uliyokwenda ndiyo njia yetu sote kama siyo leo basi...
hawa ni watoto wa kampuni moja ya kufanya utafiti kutoka kenya yenye ofisi yake jijini ambayo hapo nyuma ilikuwa ikitafiti mambo ya habari. mara ya mwisho ilifanya utafiti kuhusu usikivu wa redio hapa nchini na kutoa orodha ndefu kuonyesha ni chombo kipi cha habari kilikuwa kinapendwa sana...
miongoni mwa maadili ya wandishi w habari ni kutokumhusisha mtu na maovu ya ndugu zake. ukiwa fisadi wewe itakuwa makosa kumzomea mtoto wako, mke wako, hawara wako, baba yako, mama yako na rafiki yako.
hawa watu wenye uhusiano nawe watazomewa tu au kuhusishwa na nawe kama wanashirikiana nawe...
hebu tuwe wakeli katika hili. ni kazi yao takukuru kuchunguza tuhuma zozote dhidi ya mtu yeyote anayetuhumiwa kuhusika kwa njia moja au nyingine na rushwa au kwa jina la siku hizi ufisadi. kwa hiyo waacheni takukuru wachunguze.
ni makosa kama sisi raia tutawakingia kifua wabunge fulani au watu...
nakushukuru Paka Jimmy kwa hoja yako lakini ni kwa bahati mbay sana kwamba hadi leo hakuna mtaalam wa sheria hata mmoja aliyenijibu swali langu kuhusu ubaguzi kazini - nini adhabu yake na kama naweza kupata fidia au kama mbaguzi ni mgeni aweza kutimuliwa nchni.
naheshimu sana mawazo ya watu wote wanaompigia debe dk salim ahmed salim lakini ningependa mtu mwenye kujua mambo au mwenye kumbukumbu nzuri ya nini kilichojiri mwaka 1985 wakati wa mchakato wa kumtafuta mtu wa kumrithi baba wa taifa katika kiti cha urais atuambie ni kwa nini sas hakupewa nafasi...
kwani viongozi wa chama gani kingine wamewahi kuwa madarakani wakaboronga au wakafanya mema ili tuwapime? mpaka sasa nchi hii imewahi kutawaliwa na waheshimiwa wa ccm pekee na ndio tunaofahamu madudu waliyoyafanya na sina haja kuyaorodhesha hapa.
waswahili wanasema mwizi na hindi lake na hadi...
nilitarajia kukaribishwa kwa maneno ya upendo na upole. bahati mbaya hilo halikutokea bali nimekaribishwa kwa maneno ya kunituhumu na mengine ya kunibeza eti mimi na katoliki mgalatia mkubwa. hata hivyo miye nimefurahishwa sana na mawazo ya watz wenzangu. na wengine tayari wameanza kunijadili...
nimesoma sheria ya ajira na mahusiano mema kazini (employment and labour relations act) nikagundua kwamba ni kosa la jina (offence) kwa mwajiri kumbagua mfanyakazi in policy or practice. sasa je shauri la namna hiyo la kubaguliwa na mwajiri linafunguliwa katika mahakama gani na adhabu yake ni...
naitwa lovulovu, mkazi wa jijini, mpagani kwa dini au kwa lugha rahisi kafiri. nimefurahia sana mtandao huu nami naomba mnikaribishe tuungane tuweze kubadilishana mawazo hasa hili la kutaka eti kutumia kodi yangu kuwalipa mahakimu wa waungwana wasiokula visivyochinjwa waitwao makadhi na mengine...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.