Taarifa ni muhimu ifafanue wagonjwa hao wanaishi maeneo gani na majina yao, itasaidia wananchi kuchukua tahadhari lakini sio kunyanyapaa. HII ni VITA sio LELEMAMA na tuachane na hizo ethics za kuficha siri, tazama muda mfupi tu social media Inaumbua.Taarifa itolewe rasmi na kwa wakati
Kama kuna mashirika ambayo nahisi yanahitaji kupitiwa na kasi ya upepo wa JPM ni NSSF na DAWASCO - wanyonge wanadhalilika sana kutokana na utendaji mbovu
Wakati wajapani wamemaliza Ujenzi daraja la Mfugale mazingira yalikuwa mwanana majani yaliyopandwa hapo yakipendeza - pita leo UTASHANGAA jamani hata kuhudumia mandhari hatuwezi? TANROADS au City? Mpo wapi au bado mnafanya mchakato wa Tenda?
Hivi mnapopakua tozo ya kupaki magari hata kwenye mahospitali hamuoni aibu? Mfano pale kwa Kariuki, hospitali sio yenu kwa nini mgonjwa afike na kulipa tozo ya paki kwa Jiji? Matibabu huchukua muda mrefu je hamna vyanzo vingine vya mapato zaidi ya kuwatoza wagonjwa?
Habari za BOT kusimamisha TWIGABANCORP kwa nia ya kusimamia au kuifilisi ni habari zisizo njema kwa Wananchi hasa ikizingatiwa kuwa benki hiyo wateja wake wengi ni wajasiriamali wadogo. Tangazo la Governor wa BOT limechanganya watu wengi tazama wale ambao wana akaunti hapo na wanazitumia...
Hivi hawa wanaotengeneza bustani kona ya Nyerere Road na Mandela hawana habari kuwa Ujenzi wa madaraja hapo karibu unaanza? Hiyo miti na maua wanayopanda si itang'olewa tuu? Hii kweli kichekesho na ni jipu hili linafaa litumbuliwe
Ningekuwa mbunge ningetoa hoja binafsi kama ifuatavyo:
HATUA DHIDI YA MAJANGA YA BARABARANI: Kutokana na madereva wa vyombo vya moto kutobanwa na sheria kali, uzembe utaendelea nchini na tutazidi kuwapoteza ndugu zetu kutokana na ajali. Aidha ajali zinaathiri uchumi kutokana na ndugu wa...
Habari nyingi miaka na hasa siku za karibuni ni ajali na vifo vinavyotokana na ajali na sababu kubwa ni mwendo kasi. Hivi kwani waendesha magari wanakimbilia wapi? :A S 13:
Yeyote yule kwenye madaraka anayetoa idhini ya kuweka yadi za kontena ndani ya jiji la Dar Es Salaam bila kuangalia hali ya barabara kwa malori kuingia na kutoka ndani ya hizo yadi sidhani kama anajua anachokifanya, matokeo yake malori yanaziba barabara, yanageuzageuza na kupaki barabarani...
Nilipata nafasi ya kupita kuangalia chuo cha mafunzo cha Swissport pale Nyerere Road kwa ajili ya mwanangu anayemaliza chuo mwaka huu - nilishangaa kuona madarasa ya kisasa yenye viyoyozi, computer n.k. Hongera wana Swissport bila shaka mtaongeza ujuzi kwa vijana wetu ambao wanahangaika kupata kazi
Nilipatwa na dharura wakati niko tayari kwenda safari Mwanza, nikapiga call center ya precision simu inanipa matangazo ya ROYAL PAA haipokelewi hata baada ya kurudia mara tatu nikaachana nao. Kesho yake naenda airport naambiwa kalipie "No show fee Tsh 25,000" nikakumbuka siku nimekaaa Mwanza...
Men what is happenning with Precisionair flights today, most of us are stranded with only one reason "Operational reasons" what does operational stand for ?
Vituo fulani vya mafuta wame de-calibrate; ukinunua lita tano mashine yaonyesha yes 5 liters lakini ulichopata ni lita 4.5 au lita 4, unalipa bei ya lita tano. Hii nimethibitisha jana. Ukitaka kujua jaribu kununua mafuta kwa lita ulizozoea na jaribu baada ya kujaza kuangalia geji, utashangaa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.