Katiba ya Tanzania katika moja ya ibara zake inasema "Kila mtu ana haki ya kukutana na mtu yeyote... mradi havunji sheria". Sasa hicho kikao unachikikomalia kimevunja sheria ipi?
Na huko kujiamini kwako unakodai hakuhitaji mtu akushangae, bali kukupuuza!
Mkuu, tatizo kubwa la NCCR-Mageuzi ni KUKIUKWA MAKUBALIANO YA KUACHIANA MAJIMBO, zingine ni blabla. Sasa ujio wa Lowassa nd'o umefanya washindwe kuheshimu makubaluano hayo? Na je, hao viongozi WAZURI wa UKAWA si ndio walikuwepo 2010, mbona hawakushinda?
Ujio wa Lowassa ni tukio la kihistoria...
Kumbuka ahadi za JK zilitokana na ilani ya uchaguzi ya CCM, hazijatekelezwa.! Magufuli naye anayoa za kwake kwa ilani ya chama kilekile, CCM. Na wakati alipoteuliwa kuwa mgombea wa CCM, Magufuli alisema anasubiri ILANI ya chama ili kueleza ataifanyia nini Tanzania.
Ni kukosa uelewa kuzidi...
Uwaziri ni swala jingine, wagombea ubunge wanapiga kampeni kama wabunge na siyo kama mawaziri watarajiwa. Ikitokea Rais akamteua mbunge (Mnyika, Kubenea) kuwa waziri linakuwa swala jingine. Lakini "spirit" ya Mnyika itaendelezwa na wabunge wenzao ambao hawatakuwa mawaziri. Kazi ya Bunge ni...
Elba, usijifariji: Sijui ACT mara CDM Vasili... hakuna lolote. Hakuna CDM Vasili wala nini, CHADEMA na UKAWA ni wamoja. Na usishangae ACT wakapunguza kura za CCM,kwanza Zito ameshaanza kumponda mgombea wake kuwa hafai anaposema "nitagombea urais 2020".
Maistro wewe unamwandama Kubenea, mbona mwenyekiti wenu alisema kilichomkuta Lowassa ni "Ajali ya Kisiasa". Hii ni kwa sababu JK alikuwa anaujua ukweli wote, na kwa kuwa Lowassa ameuanika hadharani jamii (akiwemo Kubenea) lazima imwamini, vinginenyo JK atoke hadharani akanushe.!
Ng'wanapagi: Acha kudanganya kuhusu jimbo la Msalala kwa Maige; yupo Kamanda anapiga kazi. Kampeni alishaanzia Isaka tangu Aug.31..! Kuhusu kujulikana siyo hoja, wewe subiri Oktoba 25. Anaitwa Paul Malaika, alikuwa mfamasia wa wilaya ya Ukerewe, ame-resign baada ya kuteuliwa na CHADEMA kugombea...
Wewe endelea tu kushangaa..! Chama si mtu mmoja, ni taasisi. Kwanini yeye tu (na Lipumba) nd'o akatae kumpokea Lowasa? Huoni kwamba kuna uwezekano wa mgongano wa masirahi (kwamba kanyang'anywa tonge mdomoni?). Na kama hakubaliani na uamuzi wa chama, kwanini asiseme amestaafu tu siasa ikatosha...
Eti Ukabila na Udini..!? Nani asiyejua kwamba CCM mnasambaza sms kwa Wasukuma kuwashawishi wamuunge mkono Magufuli kwa "Usukuma wake". Hatudanganyiki, mwaka huu mtanyooka tu.
Adui #1 ni CCM na mfumo wake kandamizi, Edo alidhani angeleta mabadiliko ndani ya CCM lakini mizengwe imemkwamisha. Sasa mabadiliko anayaleta ndani ya UKAWA. CCM kwa heli ya kudumu siyo ya kuonana..! Mtabaki historia kama KANU ya Kenya.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.