Hatuna wapinzani Tanzania ila tuna magenge ya wahuni. Wapinzani wetu ni wa kwenye keyboard wanataka wachukue nchi bila kutoa Jasho kabisa. Wapinzabi wetu wanaogopa kwenda jela kwa kutetea wananchi, mwenzao wa Senegal alikuwa jela na ametoka jela amechukua nchi. Kwa sasa tunahitaji chama kipya...
Kuna biashara kubwa sana katika nishati ya umeme. JNHPP limeharibu biashara ya watu wengi sana kuanzia wana siasa na makampuni ya nje yanayomiliki vitalu vya gesi kusini mwa Tanzania ambao walitegemea kuendelea kutuuzia gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme.
Jitahidi kufikiri kabla ya kuandika. Marekani kuna bwawa la kuzalisha umeme ' Grand Coulee' lilianza uzalishaji mwaka 1942 hadi leo linafanya kazi, miaka 81 bado linazalishaji umeme.
Bila ujasiri wa JPM kujenga JNHPP nchi yote ingekuwa gizani kwa sasa. Wapingaji wa huo mradi huwezi kuwaona hapa tena walikuwa na nia mbaya sana na nchi hii.
Nafikiria tu isingekuwa ujasiri wa JPM kuanza ujenzi wa JNPP, nchi ilikuwa inaingia gizani mazima. JNPP ni 'Game Changer' linaenda ku boost uchumi wa nchi hii. Hakika JPM aliona mbali. China walipojenga bwawa la 'Thee Gorges' lenye capacity ya 22,500MW uchumi wao ulianza kukua kwa kasi maana...
Hivi vyama viwili(CCM na Chadema) ni tatizo kubwa kwa sasa katika nchi yetu. Mnaviziana hadi kwenye misiba kuona nani kasalimiwa kwa kupewa mkono au la! Nani kapewa nafasi ya kuongea kwenye msiba! Mnaenda kwenye misiba kichunguzana na si kuomboleza. Mnatuharibia nchi yetu, wote hamfai.
Bora wewe umesema kweli. Mi CCM na Mi Chadema ni tatizo kubwa sana katika nchi yetu. Hivi vyama viwili vinatuharibia nchi. Tunahitaji chama kipya kisichokuwa na unafiki, majungu na fitina.
CCM na Chadema mnaiharibu sana nchi hii, unafiki, majungu, na mambo mengi ya kuhujumiana na kusingiziana. Tanzania bila CCM na Chadema inawezekana. Tunahitaji chama kipya kitakacholeta mshikamano wa nchi bila chuki na unafiki.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.