Asanteni sana wakuu kwa taarifa mbalimbali mlizonipatia. Nilisafiri na Bus la Kilimanjaro, ni semi-luxury halina hata AC kumbe ila mwendo wao ni mzuri na uendeshaji wao ni mzuri.
Na hoteli nilipata inaitwa Briston iko karibu na mnara wa Azimio la Arusha ni mpya na bei ni 40,000. Pazuri sana.
Kwa Dar - Dodoma kuna Shabiby ni luxury kisawasawa. Nauli yao ni 40,000. Seat zake ni 1 by 2, lina choo na ni full AC. Pia lina Wifi na sehemu ya kuchajia simu na kila mtu ana TV yake kama kwenye ndege za masafa marefu.
Wakuu hasa wenyeji wa njia ya Dar - Arusha, naomba kujua Bus zuri (luxury) kuliko yote na la bei kubwa kuliko yote ni lipi na ni bei gani? Kwa wenyeji wa Arusha Hoteli gani nzuri ya kati ya Tsh. 30,000 - 50,000? Natanguliza shukrani zangu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.