Umepatia; kwa sisi tuliokuwa vijana na mashuhuda enzi hizo. Makongoro (Mako) ndiye aliyekuwa anasoma Tabora Boys wakati huo na hahusiani kabisa na tukio (la John pale Mazengo). Ingawa Makongoro naye alikuwa mtukutu fulani hivi pale Tabora Boys (ndie aliyekuwa drummer wa bendi ya muziki pale...
Inasikitisha. Huyo unayesema "hawezi" kuongea Kiingereza ni rais wa nchi na amekuwa waziri kwa takriban miongo miwili. Wewe "unayeweza" kuongea hicho Kiingereza umefanya nini cha kumshinda? Hebu tuache kuwa na akili za kitumwa kidogo. Chuki zako binafsi kwa Magufuli hazitakusaidia sana.
Tatizo hawa wapiga propaganda wa mtandaoni ndio wanaoharibu zaidi taswira ya upinzani. Sijui kwa nini wazee wao kama Baregu n.k. wanaacha hali hii ya lugha ya matusi iendelee; bila kujaribu kuingilia kati, na kuwafundisha hawa vijana namna nzuri ya kupiga propaganda enzi hizi za utandawazi.
Upinzani umerudi nyuma miongo kadhaa kwa kukumbatia siasa zisizojenga. Ni vigumu sana kutoa ushauri kwa mawazo kama haya yaliyojitokeza hapa. Ya Lowasa yangekuwa ni fundisho lakini inaonekana imekuwa ni kinyume chake. Tusubiri tuone huyo shetani anayekumbatiwa atawafikisha wapi safari hii.
Hakuna ukweli wowote. Jubril Al Sudani hajawahi kuwa Buhari. Hizo ni propaganda za waibo zikiongozwa na kupikwa na Nnamdi Kanu wa IPOB (Indigenous People of Biafra).
Tumekaririshwa kuwa hiyo ni vita vya dunia lakini kiukweli ni vita vya mataifa ya Ulaya. Sisi tuliingizwa tu kupigania ushindi wa wakoloni waliotutawala, aidha upande wa wajerumani au waingereza.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.