Niliposoma hii mada nikaingia kwa hamu kubwa nipate ushahidi wa uwepo wa Mungu, lakini mtoa mada hajaongea chochote cha ushahidi, anaishia tu kurudia maneno yale yale "... kwa IMANI yangu NAAMINI kwamba chanzo cha nguvu hizo ni MUNGU".
Hakuna ushahidi wowote, bakini na imani zenu tu, kwani...
Sijui tuwafanyeje madereva wa inji hii. Hili ni janga kubwa! Hata ukiwa Dar unaendesha gari, ukipunguza mwendo tu unapokaribia reli ili uangalie kabla ya kuvuka utasikia nyuma yako unapigiwa honi balaa, na pengine wataku-overtake kwa fujo! Nachotaka kusema hapa ni jinsi madereva wengi...
mmhh! Mie siamini kama kuna kitu ambacho UKAWA wangefanya eti kizuie Katiba kupita. Mnawonea bure UKAWA, wamejitahidi kadri ya uwezo wao. Mie nilifikiri sasa mtaelewa kwanini walitoka bungeni badala ya kubaki wakipambana humo humo!!
Mie natumia Airtel modem (HUAWEI), napiga *148*88#, najiunga vizuri kabisa. Tatizo naona hizo points, kama vile .5 kwenye 3.5GB hawatoi, wanakupa 3GB only. alafu ukiuliza salio pia naona hupati figure zaidi ya hiyo hiyo 3GB uliojiunga nayo!
Lakini hata hivyo, ukipiga hiyo *148*88# unapata machaguo mengi zaidi ya hayo waliyoweka kwenye website. mfano, ukichagua OMG wiki unapata options hizi:
1. MB 600 kwa Sh 600
2. 1.2GB kwa Sh 900
3. 3.5GB for Sh 1700
4. 6GB kwa Sh 2500
5. 11GB kwa Sh 6000
Mie nilichagua 3.5GB for sh 1700...
Kwa mujibu wa ratiba ya sasa ya BMK, Kamati ya Uandishi itawasilisha Bungeni Rasimu ya Katiba tarehe 22 Septemba 2014, Asubuhi. Sijui kama wataiweka kwenye tovuti yao au mpaka ufuatilie matangazo live. Na pia sijui wataisoma yote, mwanzo mpaka mwisho, au watatoa 'summary' tu.
Kwa wale waliopitia JKT, hasa enzi hizo, mlikuwa mnapewa magunia matatu ya mbegu za mahindi, mnaambiwa mkapande yaishe leo hii! Kinachofuata ni 'kutimiza lengo', YAISHE! Sasa wanachokifanya BMK ni kufikia lengo la kupatikana katiba. Ubora sio muhimu. Cha muhimu ifike siku, waite waandishi wa...
Lakini hizo picha haziwezi kutoa ushahidi wa kuamini kwamba hayo ndio mapokezi. Jamani kuweni wagumu kidogo kuamini mambo kirahisi rahisi hasa kunapokuwa hakuna ushahidi wa kutosha kutoka kwa mtoa habari. Huyu mtoa mada angalau angeleezea kuwa yeye alikuwepo uwanja wa ndege tokea rais anaingia...
Nafikiri watajitahidi waikabidhi hivyo hivyo tu hata kama itakuwa haijakaa vizuri. La sivyo, baada ya uchaguzi wabunge wengi hawatakuwepo na kutakuwa na wabunge wengine wengi wapya. Na tukumbuke hawa wabunge ndio wajumbe wengi katika BMK. Sijui itakuwaje tu!
Uko sahihi ESAM. Sio wana JF wote wanakaa marekani, na ni haki ya kila mwana JF kusoma na kuelewa maudhui yaliyomo humu, kulingana na taratibu. Naamini ameelewa, tunasubiri aombe msamaha, ni muungwana huyu, ana utamaduni wa majuu.
Da! Matola mbona unakuwa mbabe hivyo?! Watu wana haki ya kuuliza kujua hiyo DMV ni nini kama hawajui; waeleweshe kaka! Hata mie sikujua ni nini hicho mpaka niliposoma post nyingi.
Nafurahi sana ninapoona filamu za kitanzania zikizidi kupata umaarufu ndani na nje ya nchi. Siku hizi filamu nyingi za kibongo zinawekwa 'subtitles' za Kiingereza ili kuongeza uelewa katika lugha hiyo pia. Lakini sasa, hicho Kiingereza jamani kinachowekwa sijui ni makusudi au bahati mbaya! Ni...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.