mbona yule mjeda wa kike aliyewadhibiti majambazi kumpora silaha alipandishwa cheo kwa tukio lile bila kwenda mafunzo???
inawezekana kabisa kumpandisha askari cheo kisha baadae akaenda mafunzo. hilo linafanyika sana toka serikali awamu ya kwanza.
kauli ya rais ni amri halali. mambo ya...
huyu kwa sasa sijui aseme nini nimwamini maana ilishasema siasa ni kubadili gia angani...... "over my dead body cdm haiwezi kumpokea lowasa". sasa hata hiyo kauli yake yaweza kuwa ni yaleyale.
nasubiria dr slaa mwenyewe atoe kauli.
kwa sasa mbowe nitamwamini tu akisema mama yake mzazi ni mwanamke.
ni vema ukawamchukulia kama sahani kwa mama ntilie, huwezi kuwa na sahani yako peke yako kwa mama ntilie. kukubwa kabla hujala hakikisha imeoshwa vizuri kwa sabuni na haina shombo.
ndio inawezekana kupenda bila kutamani. fikiria mtu unawasiliana naye na hamjawahi kuonana na unajikuta unampenda kiasi ambacho hata hutamani kumaliza siku bila kuwasiliana naye tena ukizingatia hata hujui yukoje. Inawezekana kupenda bila kuona ndio maana watu wengi wanasema wanampenda Mungu...
Ikiwa ulichoandika ni sahihi, unadhani ni kwa nini ndani ya bunge la kutunga katiba limejuisha maaskofu, mashehe na wachungaji kutoka dini na madhehebu mbalimbali??? kwanini wasingeachwa ili katiba itungwe na wanasiasa pekee????
Natamani Ifike mahali kila mtanzania ajivunie kuongea lugha yake ya Taifa, yaani tuache kuzitukuza lugha za wenzetu isipokuwa kuswahili tu. si lazima mtu ajue kuongea kingereza ili awe kiongozi kwani wapo wakalimani ambao wataweza kutafsiri ilikwa wasikilizaji hawajui kiswahili, ni nafuu kuiga...
Unadhani ccm ikimnyang'anya jk uanachama wa ccm ataendelea kuwa rais wa nchi? ikiwa ndio basi fahamu kuna uhusiano wa wenye nguvu ni kati ya rais na chama chake, na njia ya kumuadhibu rais ni kukiadhibu chama chake kwani kina wajibika ktk sera na itikadi kwa rais anayeongoza.
Ikiwa ni hivyo au sio hivyo sio hoja cha kufahamu ni kwamba hata simon mchawi wa kwenye biblia aliweza kubadilishwa na Mungu, kumbuka hata Mtume Paulo alikuwa mtesaji wa wakristo kabla Mungu hajaamua kumtumia.
Mara nyingi Mungu hupenda kuwatumia watu dhaifu, Musa kutokana na udhaifu wake wa kuzungumza alihofu kutumiwa na Mungu lakini Mungu aliamua kumtumia, suala sio Kakobe kufananishwa na Moses bali ni kufahamu kuwa Mungu huamua kumtumia yeyote atamtakaye bila kujali ana nini kwani binadamu ni chombo...
Mwenyekiti wa chama ndiye aliyeteua majina, na chama husika ndicho kimempa tiketi ya kukalia ofisi inayolalamikiwa nadhani hiyo ni sehemu ya uhusiano unayoulizia.
Kwa maneno haya maana yake wewe naye uko tayari na ndivyo huwa unafanya, yaani unamchagua shetani bora badala ya kumchagua malaika au kuwa radhi kuharibu kura yako ikiwa wamesimama mashetani watupu.
ni kweli hadi kuwe na michubuko kwani una hakika gani kama hakukuwa na michubuko? eneo lenyewe linafichwa kwenye joto muda wote. ndio maana namalizia kwa kusema kupima ndio kupata uhakika.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.