Mkuu naomba nichangie kwa lugha yangu
Nachomekea kidogo,
Najua unazungumzia watu, ila kwa kuangalai sinema za wanyama, mfano nyati au nyumbu, ukizubaa peke yako peke yako unahatihati ya kuliwa na samba au fisi.
Kaa na wenzio uwe salama zaidi
Respect !!!
Ndugu yangu Deo
Nilitaka nipite tuu bila kukoment lakini uvumilivu umenishinda
Hebu achana na aina ya "maharagwe" unayokula
Badili aina ya mboga mkuu
Usisahau kunywa maji mengi kuondoa sumu mwilini na kupunguza stress
Respect !!!
Ndugu Chinchilla
Nashukuru kwa kuweka hii video ya Ndugu Rais siku ya Kismas kwa ukamilifu wake.
Kuna watu waliongea sana kuhusu Rozari nk. Wakayacha yoote mengine muhimu kwa makusudi.
Tujifunze, tutafute ukweli, tuache kuamini simulizi tuu.
Shukran Ndugu Raisi kwa hotuba safi, japo fupi...
Ndugu zangu
wakati mwingine nashindwa kuwaelewa watanzania wenzangu
Hivi vita dhidi ya ufisadi nk ni vyetu sote kwa faida yetu wote.
Sasa tunaposema Ndugu Rais kapigwa nk sii ni ujuha uliopitiliza ? Hasara ni ya nani ? Mtu kajitolea watu wanaleta ujuha. Inakera sana hii
Ndugu zangu...
Shukran sana ndugu Pondamali kwa kuleta taarifa hii.
Nimepitia mwanzo mwisho angalau nipate namba ya simu au njia yeyote ya kuwasiliana na familia ya ndugu George.
Tafadhali kama kuna ndugu yeyote humu atakayeweza kusaidia hili nitashukuru sana.
Ahsante
Respect !!!
Salaam bro Andrew
Kwa hiyo mantiki ya maelezo yako hapo juu ni kwamba
Tufumbie macho uvunjifu wa sheria ?
Pia na ni sawa "two wrongs = right ?"
Au nimelewa ugali wa hamira niliokula mchana huu ?
Tafadhali tusaidie ufafanuzi mkuu wangu, ni hayo tuu
Reaspect !!!
Ndugu zangu
Na mimi nianze kwa kumshukuru sana mwenyezi Mungu kwa mengi sana na yote. Mojawapo ni kwa kunipa pumzi ya kushuudia haya. Utendaji wa raisi wetu Ngugu John Magufuli na timu yake unaleta matumaini makubwa sana ambayo nikiri bila hiyana yalikuwa yamefifia sana kama sio karibu...
Shukran sana Rev.
Maswali ya msingi sana haya, na mengine meengi tu kuhusiana na ufisadi, uadilifu, uzembe, uonevu, uporaji, uuwaji nk nk.
Wahusika wajulikane, waadhibiwe kwa mujibu wa sheria na kilicho chetu kirudishwe na fidia juu.
Vinginevyo ni "Usanii" tu. Haki lazima itamalaki...
Mzee MM Asalaam Alheikum
Tukiwa wawazi na wakweli kwa nafsi zetu binafsi sijashawishika na hawa woote wanaojipitisha pitisha, kujifaragua na kupiga makelele kila kona.
Na hata hawa wanaopigiwa chepuo mhhhh, sidhani, ila huyu labda, pengine anazo silaha za maangamizi ambazo amezificha mpaka...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.