Sio maarufu TU, kikawaida msiba ni WA watu wa karibu sana na aliyefariki. Sio kama KiTanzania, msiba mtu yeyote TU anakuja kadiri anavyojisikia na haulizwi kitu na mtu. Hapo usiwasahau wale wanaokuja ili kugonga chai, chakula cha mchana mpaka cha usiku kwenye misiba ambayo hata haiwahusu.
Kwa hiyo ukipiga haswaaa, siku ukifa ndio hakutawekwa mbadala wako!? Hiyo ni falsafa ya maisha "kufa kufaana". Hata Katiba ina provision kabisa ikitokea Rais kafariki arithiwe vipi, ndio wewe mshika mic studio usirithiwe!
Mnafiki haachi unafiki! Nakumbuka alipowaharibia tamasha lao la Fiesta ule mwaka na kuwasababishia hasara kubwa waliochukua tenda za kuuza vyakula na vinywaji. Hapo Bado suala la kuvamia studio.
Ni kweli.. Baadhi ya watu wanaamini huo ni utajiri wa fedha zilizoko benki kumbe ni thamani ya uwekezaji wake inavyopokewa na soko .
Leo hii Kanye West aliyekuwa anathaminishwa kuwa bilionea Leo anathamani ya Dola milioni 400 TU, baada ya mgogoro wake na Wayahudi.
Mimi natetea Haki yake ya kuishi maisha yake bila ya kubugudhiwa na mtu. Nashangaa Wabongo kushupalia ishu yake ya Uchoko wakati hao waliomfunga hawajamfunga kwa kosa Hilo. Wanamuhukimu vipi mtu ambaye mamlaka za kwao hazijamuhukumu kwa kosa Hilo!? Ina maana anaathiri Tz kuliko Naija!?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.