Kumtoa huyo Mkurugenzi kunanishangaza kwani alitamka mwenyewe kuwa amefanya kazi ya kina kuwateua hao wakurugenzi. Alisema hata wengine anawafahamu kwa majina. Je huyu alipitia chekeche lipi?
Nimeibuka tena wana Jamii. Kuhusu hao vijana ni bahati wametambuliwa lakini wengine wanaofanya vitendo wanapoteza ushahidi kwa kumpoteza muathirika. Ni vyema adhabu iwe nzito kama fundisho. hivi miaka 30 ndio maximum?
Naungana nanyi kwamba mbali na TV Clouds hata FM88.5 kuna vipindi watangazaji wanakuwa kama watoto wanaongea pumba...huwa nashindwa kuwasikiliza kwani haina mantiki kabsa. Hata kama ni vipindi vya vijana view angalau vya kuelimisha kwa kiduchu. JIREKEBISHENI TV CLOUDS NA FM 88.5
Vodacom kwanini mmeshindwa kuboresha mtandao wenu hususan mteja akitaka kununua Luku? Hakika mmenichosha mno. Kwanza hamjibu haraka kuna wakati nilihitaji umeme jioni nyie mnatuma asubuhi. Leo tar 2.6.2015 naagiza umeme mnarudisha ujumbe eti nimekosea namba ya mita wakati sio kweli. Isitoshe...
Ninalazimika kutoa dukuduku langu kuhusu kauli za "kiongozi" kama Mulongo ambazo zinaonyesha jinsi anavyohatarisha amani ya nchi. Anajiandaa kwa pesa kupata Uongozi? Hapo amepotoka labda aseme ameteleza lakini si kauli njema kwa mambo yalio mbele yetu hususan uchaguzi unaokuja. Wananchi sasa ni...
Kwa ujumla hoja iliotolewa ni ya kitoto kabisa. Ningependa kujua alieanzisha mada hii ana watoto wangapi? Hata hivyo kumwona motto wangu haendi au hafuati maadili hainifanyi maamuzi unayojaribu kuyapenyeza hapa. You are simply using the wrong analytical tools to arrive at decision. Pole sana.
assadsyria3 - Unakosa maana, hekima na utu wa kumstahi mwenzio. Lugha uliotumia haikubaliki kamwe. Imetokea wapi. Sielewi ufahamu wako uko kwa kiwango gani hata 'reasoning capacity" yako, hivyo punguza jazba zisizo na msingi.
Binafsi nimependa hatua iliyochukuliwa na Rais Kenyatta katika kusafisha safu yake ya Mawaziri ambao wametajwa na Tume ya Rushwa ili kuruhusu uchunguzi wa kina. Amewaagiza kupisha uchunguzi huo. Je Tanzania tunajifunza nini kutokana na hatua hizo au maamuzi magumu? Lazima nchi yetu ichukue hatua...
Naafiki wizi wala sio wa kujificha wa salio ambapo Voda wanaiba. Nazima data package kwenye simu baaa ya muda hamna salio. Huwa nashangaa sana. Ina maana TCRA hawalijui hili au nao wanashiriki? Mchezo huu ufe.
Jiulize Kwanza, hata kama umeandika la maana ama la, tafadhali badilisha rangi ya hoja yako. Inaumiza macho labda ingekuwa kichwa cha habari peke yake sio neon ila ukitaka upate input kwa hoja yako fuata hilo.
Nilishuhudia vitambulisho vya zamani kupewa watu ambao si Watanzania. Tulipofikia ni njia panda na inabidi maamuzi magumu yafikiwe vinginevyo itakuwa hapakaliki.
Ukweli ni kuwa hukumu ya mwisho ya kila mmoja wetu ni Mwenyezi Mungu aliye na mamlaka nayo. Kifo cha Kepteni Komba kinatukumbusha kuishi maisha mema hapa duniani. Kitu ninachokiona ni kuwa baadhi ya waombolezaji walikuwa wanalia wakiona kuwa "Chama Chao" kinakosa mhamasishaji. Yote kwa yote...
Mtandao wa Vodacom mara kadhaa umeniadhiri hususan wakati wa kununua Luku kupitia mtandao wao. Sijawahi kupata charge mapema kama mitandao mingine. Ni kero kutumia Vodacom kwani unaweza kukaa hata masaa 6 hujapata majibu na umeme umeshakata. Hii sio sawa marekebisho makubwa yanahitajika ili...
:A S embarassed:Nimekuwa mdau wa Vodacom kwa muda mrefu lakini la kushangaza ni huduma yao ya kununua Luku kupitia mtandaoni inavyosuasua. Hakika ni tofauti na wengine kwani Vodacom inaweza kukaa hata masaa zaidi ya sita hujapata huduma. Naomba waliangalie suala hili kama wanao vijana wa IT...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.