Mimi niliona kwenye tv. mheshimiwa alimpelekea mkewe alipolishika tu huyo mzungu hapo kulia akamfuata akamwambia no no kwa ishara ya mkono mama wa kwanza akaliachia
Kumpa mtu jina la mzazi ndio ni heshima ila mara nyingi tabia huambatana na jina kama mtu amepewa sababu ya fulani. Na hilo la tamthilia pia siliafiki, wakae chini watafute jina watakalokubaliana pamoja bila kupendelea upande mmoja..wanaweza hata kutunga la kwao ila majina ya kurithi siyafagilii...
Jamani sio kupangiana zamu bali ni kufanya kwa upendo. Hebu fikiri mtu anasafiri akirudi anakuta chumba hakijulikani mlango upo wapi na kabati lipo wapi. Ch*#i zimetapakaa kila mahali, kitanda shaghalabaghala na viatu ndo usiseme..hivi hata hamu ya majamboz itakuwepo kweli
Tuwe na utu jamani, wote mnaamka saa 11 na kwenda kazini na kurudi saa 12 jioni, hamna house girl wala mtoto kweli utashindwa kumsaidia mkeo kazi za nyumbani wakati naye pia anachoka na kuleta fungu nyumbani?
Tiba, mapenzi ni sehemu ya maisha ambayo nayo inahitaji tiba ili maisha yaweze kuwa sawa, kama wewe haupendezwi na jukwaa hilo hakuna tabu waache wanaohitaji kufahamishwa na kufahamisha waendelee sio kutoa hypothesis zisizo na reseach
Kuna kipindi kilikuwa kinaanza na wimbo wa ..tujengeee tujengeee tujenge na mwananchi engneering contractor..watu shule wakawa wanaimba tujenge na mwananchi chini ya likomtata
Pamoja na mambo ya uzalendo, ushirikiano na kufanya kazi kwa bidii, Jumong pia inafundisha imani thabiti kwa Mungu unayemwamini. Kila mara wanaomba ushauri toka kwa miungu yao katika mambo yote wanayotaka kuyafanya..inafurahisha sana
Mbona hata mimi nilipojifungua ilibidi mume wangu na mdogo wake wafanye usafi nyumba nzima kila mahali ilikuondoa vumbi? Mtoto wa kwanza ana mambo mengi wandugu. Mwambie huyo jamaa yako kama kweli anampenda mkewe wakae chini waongee bila kushutumiana wamlee mtoto wao waache malumbano na mtoto...
Mimi nadhani tangu mwanzo hawana mawasiliano mazuri. Sio jambo la ajabu mama akaomba kukaa na mwanae wiki zaidi tena ambapo amejifungua kwa operation. Ila huyo mke alitakiwa amueleze mumewe mapema na wakubaliane.
Swala la kwenda sokoni mi naona huyo mume ame-react sana, simu yaweza kuzima kwa...
Nasukuru kwa ushahuri huo, dada dina tulikalishana mara ya mwanzo na mume wangu alikuwa haamini kama hisia zinaweza kufa kutokana na matendo yake na akasisitiza kuwa simpendi na simuheshimu, mara ya mwisho tumekalishana na akakubali nusu nusu kuwa amesababisha mimi kuwa 'cold' ila haonyeshi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.