Serikali ipo na haingozwi na Slaa wala CDM ila imeparaganyika ile mbaya. Walau Rostam mwenyewe aliyesababisha JK kukosa nguvu ya kutawala angeamua kuionea huruma serikali na kuwaacha wajiendeshe kwa kutumia busara pasipo kuogopa yeye (RA) ataonaje.
Mungu isaidie serikali yetu. Japokuwa ni...
Ala kumbe wewe umejihisi kwamba u-mamluki!!
Kwa taarifa yako mimi ni mmoja wa wale wanaoweka TAIFA KWANZA kuliko vyama vya siasa. Sijui wewe mwenzangu uko upande gani? Yaelekea hata hujali taifa likitumbukia shimoni na wewe ukiwemo kwa kudhani kwamba wote wanaochangia humu ni wafuasi wa...
Bila shaka hukunielewa ama umekurupuka tu kwa ushabiki usio na tija. Nimeuliza gazeti la MAJIRA la leo. Mitandao ya CHADEMA ama CCM hainihusu sana nilichokuwa nataka kujua ni kitu gani kiko kwenya MAJIRA kiasi cha gazeti hilo kukosekana sehemu nyingi.
Once upon a time Jamiiforums was a...
Alikuwa sahihi kwa yote mawili. Hilo la kwanza alilisema akijua wakati huo kwamba CCM kilikuwa kimejaa wanachama na viongozi wazoefu ambao wangeliweza kuwania uongozi na kuliongoza taifa bila matatizo.
Halikadhalika, alikuwa sahihi kwa sababu hata Dk. Slaa anayesifika hivi sasa ametoka ndani...
Sidhani kwamba Mwalimu angelikubali chama alichokiasisi kiendelee kufanya madudu hata kufikia kukataliwa na wananchi waziwazi kama tunavyoona sasa. Alternatively, angelinawa mikono na kujitoa CCM. Tukumbuke alishatamka kwamba CCM si baba wala mama yake.
Naunga mkono maneno yako kwa asili mia. Hatupendi kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa letu kujenga misingi ya amani na utulivu ije ibomolewe kwa sababu ya watu kutaka uongozi kwa lazima. CCM chama changu, kama wana mipango hiyo basi watakuwa wamepotoka kupita kiasi. Mungu alinusuru taifa...
Asante Malunde-Malundi,
At least wewe umenipa jibu zuri kuliko mgonwa wa Malaria Sugu! Sasa najua kwa nini limeshabikiwa! Naendelea kulitafuta nisome nijue nini kimesemwa humo.
Ubarikiwe.
Asubuhi nilipigiwa simu na jamaa yangu akaniambia nitafute gazeti la MAJIRA la leo Jumapili. Nimelitafuta gazeti hilo kwenye stalls za jirani na zile za mbali zaidi lakini sikuweza kupata gazeti hilo. Je kuna anayeweza kunnijuvya gazeti hilo lina habari gani kiasi cha kununuliwa na kwisha kwa...
Na mie Bibi Ntilie nimekuja mjini toka kijijini (ambako hakuna umeme kwa hiyo hakuna TV) na nimeweza kuuona mdahalo wa vijana wanaowania kuchaguliwa kuwa Wabunge kutoka vyama vya CUF na CHADEMA. Naweza kudiriki kusema kwamba vijana wote (pamoja na wale walioonekana kama wazee!) wamejieleza...
Kama kuna wezi wengine wa EPA ambao hawajafikishwa mahakamani, je Mzee Kinana anatuambia wasiguswe hao kwa sababu wenzi wao tayari wana kesi mahakamani?
Inavyoelekea CHADEMA hawakujiandaa ipasavyo kwa upande wa utumiaji wa vyombo vya habari kwa kuanzisha vyombo vyao binafsi vya TV, Radio na magazeti ili visaidie katika kusaidia shughuli za kampeni zao. Halikadhalika, hawakujishushughulisha vya kutosha kuwahamasisha wana CHADEMA katika mitaa...
Chuki binafsi nazo huwa na matatizo yake! It seems Dr. Salim stepped on your toe at one point or another. Lakini tukichukulia historia yake kama kiongozi wa kitaifa na kimataifa aliyoianza tangu ana umri wa miaka 22, nani anayeweza kumshinda Salim kwa uwezo na uzoefu wa kuongoza?
Mkuu, unaposema tuna matatizo makubwa sana ya EXPOSURE, ina maana bila ya Watanzania kuwa na EXPOSURE basi hawawezi kuelewa tofauti ya uongozi mbovu na uongozi mzuri? Ina maana katika yale majimbo ambayo yameweza kuchagua viongozi kutoka vyama vya upinzani basi wapigakura wa majimbo hayo...
Ukitaka kujua kama kuwa na magari mengi Dar ni dalili ya watu kuendelea waulize makondakta wa daladala. Hawaishi kuwatukana madreva wenye magari madogo barabarani kwa kuwaambia kwamba wanaringia magari ya mikopo tu! Ni wazi, magari mengi Dar hayatokani na maendeleo ya watu bali mikopo toka...
Wakuu,
Naona wengi wamekazana sana kumjibu Mzee Mwanakijiji kwa madhumuni ya kutaka kumshinda kwa hoja kiasi cha ku-miss points muhimu zinazoletwa na wachangiaji wengine.
Nampongeza Mwanakijiji, aelewe kwamba kichwa chake kimejaa ubongo na anayoyatoa humo kichwani na moyoni mwake...
Diplomatic immunity? Hivi mawaziri wana diplomatic immunity inayowaruhusu kuvunja sheria za uliipaji wa ushuru wa forodha? Tatizo ninaloliona ni kwamba watu tumekuwa tukihalalisha mambo katika akili na vichwa vyetu kwa kudhani kwamba ndivyo yanavyotakiwa yawe. Sidhani kwamba kuna diplomatic...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.