Hata nyinyi: Nkya na Kimwaga hamna haki ya kuitisha mikutano ya waandhishi wa habari kuliongelea hili jambo. Mlichofanya ni kile alichofanya Makonda, hili linatakiwa liongelewe na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Taifa, hata hayo mliyotoa si ya Umoja wa Vijana Taifa wala Umoja wa Vijana Morogoro...
Mkuu Makonda tafakari hizo sentesi niilizoziwekea rangi. Kwa kifupi CCM haijasema kama imepoteza imani kwa wananchi hata siku moja, mie ndiyo kwanza nasikia toka kwako. Pili, kubeza ziara ya viongozi hao ni pamoja na kutokutekeleza yale ambayo wameibua na kuyapendekeza , kumbe tuangalie ni nani...
Pamoja na mchango wako mkubwa wa kutaka kukinusuru chama, bado thamani yako haionekani, hili ni anguko la pili, kujivua magamba sasa mawaziri mizigo, pole sana kiongozi, tunajua una nia nzuri lakini chama kinakuangusha, tangu ulipokuwa umoja wa vijana ulisimamia haki, ukachukiwa, na sasa kile...
Kwa shida, matatizo, na mzigo wa maisha unawakabili walimu katika Tanzani, wewe nadhani una agenda moja na serikali ya kuwakandamiza walimu. Alichosema Mnyika ndiyo hali halisi ya maisha ya watu hawa muhimu sana kwa taifa na serikali inayojali, sioni udhalilishaji hapo bali ni ukweli kabisa na...
Naungana nawe katika hili, maana naona ushabiki wa vyama ndio umemkolea badala ya kuangalia taifa, hapa watu hawajadili vyama bali weledi wa hao waheshimiwa, kwa watu walio serious nadhani wangeangalia hilo badala ya kushabikia vyama. Taifa litaangamia kutokana na ushabiki tuuuuuuu usio na tija...
Mkuu mbona unanitisha maana kama hakuna kitu hicho sasa unafikiri tuko salama kama taifa? Hao viongozi wabadhilifu wanaponaje kama taifa likiwa si salama? ama kupitia usalama wao na yaifa linakuwa salama? Ninavyojua katika idara zote na hata majeshi, bila idara hii nyeti basi taifa liko...
Asante Mkuu, kumbe ndivyo ilivyo, basi kumbe hatuna sababu ya kushangaa teuzi mbalimbali maana kumbe mfumo wa vyama vingi Usalama wa Taifa hawahusiki kabisa. Looh, inasikitisha saana, sitoshangaa siku moja tukaona watu tusiowafahamu wakashika nyadhifa muhimu katika nchi. Kutohusisha Usalama wa...
Zamani baba yangu alipokuwa katika "System" alinisimulia kuwa teuzi zote za viongozi Mwalimu alikuwa anazifanya kupitia ushauri wa Usalama wa Taifa na alihakikisha kuwa anapata mtu anayeaminika walau mbele ya jamii, sasa sijui siku hizi kama bado hilo lipo ama ni teuzi zinafanywa na team...
Wizara ya Elimu tangu enzi za marehemu Kabeho mpaka sasa inayumba sana, nadhani wataalamu wa maswala ya Elimu pale UDSM inafaa wasaidie katika kushauri teuzi za wizara hii, hakika inayumba sana.
Mkuu ni kweli lakini mbaya zaidi ni kwa hao wanaodai wanamuenzi Mwalimu kama muasisi wa chama chao lakini hata haya ambayo kayasema huyo wanaodai wanamuenzi hawayafuati. Ni propaganda tuu, na hata wanapoyatumia ni katika propaganda utafikiri bado tuko katika mfumo wa chama kimoja, hakuna cha...
Mwenye sifa za aina hiyo HAFAI HATA KUWA KIRANJA WA CHEKECHEA, HAFAI HATA KATIKA MFUMO WA VYAMA VINGI, KIFUPI HAFAI KUWA NA CHAMA CHOCHOTE AMA MWANACHAMA WA CHAMA CHOCHOTE!
Mkuu Dr. Kitila, achana na mabishano hasa baada ya kumalizana na cdm, unajua sisi tuliokuwa naawe Southampton tunakushangaa sana jinsi unavyojiingiza katika mambo ambayo yanakushusha hadhi yako kama mwana taaluma, jamaa huku St. MARY'S wanakusikitikia sana kufikia hapo, achana na mambo haya ...
Unaweza fanya mambo mawili: 1. Nenda TAKUKURU watakupa mbinu za kumuwekea mtego wa rushwa ya ngono na atashikwa bila mashaka yoyote 2. Omba usahauri kwa Lecturers wengine chuoni kwake ama hata chuo kingine juu ya kulifikisha jambo hilo kwa uongozi. Hii inategemea lakini kama kweli unaona mkeo...
Afadhali kesho mahakama iamue maana tumechoka kusoma habari za Zito na CDM hapa, tuanataka kujipanga sasa kufanya mambo ya maana zaidi kuliko haya. Yanachosha
Mkuu Slaa na Mbowe siyo Kamati kuu wao ni sehemu tu ya wajumbe. Sidhani kama wameharibu, najua watu wengi wanapenda kuona CDM yenye utulivu na umoja kama Chama tegemeo cha kuikomboa Tanzania lakini lazima tukumbuke nidhamu na ukweli usio na hila na unafiki ni muhimu kwa wanachama na viongozi ili...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.