wewe kama nani ufichue madudu ya mbowe, kama siyo uchochezi huo nini? wanaopaswa kulalamika au kufuatilia mambo ya kodi ni TRA siyo wewe unayedandia gari ambalo hata hulijui, wahindi ni wakwepaji wakubwa sana wa kodi kwa kubadilisha nyaraka za mapato, mbona hamuwafatilii, unayemwona ni mbowe tu...
very sory, habari ni nyeupe hakuna mfano, mwandishi anatakiwa aende intensive trainning coures ya kuandika report, hii ni aibu kubwa, afisa mawasiliano msaidizi. shame!!!!!! upon you
wasukuma na waaramo ni watani wa jadi, kwa hiyo usishangae sana hiyo kauli ya mh rais ilikuja tu automatically kuwapiga dongo watani, ni mambo ya kawaida sana kwenye misiba, labda kama kabila lako halina watani.
jamani mimi naomba kujua professional ya huyu jamaa plus cv yake, nilimheshimu sana kipindi cha bunge la katiba mpya alivyokuwa anatoa madongo kutetea maoni ya wananchi yaliyoachwa, kumbe ni mganga njaa, hana lolote, kaja kuharibu sana mwishoni wakati wa uchaguzi, nahisi sasa anajaribu...
mtoa mada naona hakumwelewa vizuri rais JPM, ni kwamba yeye anataka kubalance mtu anayepata mshahara mkubwa sana na yule anayepata mshahara kiduchu, atashusha kiwango cha mshahara kwa watu wanaolipwa mfano milioni 40, na atawaongeza wanaopata mfano laki tatu kwa mwezi ili kuwe na uwiano...
hivi vitu vinanikumbusha mbali sana huko kijijini kwetu, enzi hizo maisha yalikuwa rahisi sana, vyakula vingi, nyumbani siku wakipika wali watoto hamlali mapema, hadithi nyingi mpaka mnapiga hizo punje
huyu mwandishi aliyepost hii habari ina mapungufu kidogo, kwanza yule mgonjwa alivunjika taya na wala siyo mguu kama alivyoandikwa, pili tusiangalie upande mmoja tu wa daktari kupigwa, lazima tujaribu kuhoji kwa nini alipigwa, inawezekana matatizo yapo pande zote mbili, na kitu kinachoponza ni...
hii ni kama desturi tu, kumbuka hata kwenye kusanyiko kama vile kwenye mkutano wanawake hukaa kushoto wanaume kulia, kanisani wanawake kushoto wanaume kulia, pia hata kitandani mwanamke hulaa kushoto mwanaume kulia
ongw'ise umenikumbusha mbali mambo ya ubeshi, marehemu kaka yangu aliacha shule ya sekondari shinyanga akaanza biashara ya ubeshi mwadui, niliposoma story hii, nimefurahi sana maana hii siyo copy and paste, ni vitu real ambavyo vipo kwenye mgodi wa almasi mwadui, vijana wengi ndiyo shughuli yao...
safi sana hii mkuu, inanikumbusha sehemu za dodoma, bahi huko. hizi nyumba kama umemwaga zege juu, ukimkuta mgogo mdani na chungu cha ugali wa mtama mwekundu na mlenda, maisha safi kabisa yanakwenda, anashangilia tu, ccm nambari one eheee!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.