Ni lipi serikali haijui kuhusu maisha na uwezo wa wananchi wake? Serikali inafanya tu makusudi na imewadharau mno wananchi wake na haina huruma japo serikali ni watu.
Hivi kazi ni za ofisini tu?
Mbona vijijini sehemu kubwa wanawake hawafanyi kazi za ajira (kama hizo ndio mbaya) na bado malezi ni duni? Nadhani ni mfumo wote umeenda kombo na sio tu wanawake eti wanataka kujilinganisha na wanaume. Na kama wapo si wote. Wako wanawake wanaofanya kazi na bado...
Ongea na mkeo. Muulize ni nini kinaendelea. Muonye kuwa hupendi jambo hilo.
Na endeleeni na ndoa yenu. Enaendelea kusisitiza usilolipenda mpaka nyumba inakaa sawa na ndoa inaendelea vizuri. Na wewe jiweke vizuri, sio unamlaumu mwenzio kumbe wewe hizo ndio zako.
Sioni kwanini iwe taabu kwenda kufanya DNA test, ni sehemu tu ya kuhakikisha na ikibidi kuwekana sawa. Mbona wanaume wanahisiwa au kushukiwa vibaya na wanaulizwa? Si ili kuwe na uhakikisho kwamba lisemwalo halipo na kama lipo ieleweke kuwa halipendezi na liachwe. Ni kwa mtaji huo huo na DNA test...
Siku huyo shemeji yako akikuletea tena lalamiko kuhusu mumewe, chukua nafasi hiyo kumuonya yeye kwa mifano mingi tu. Kama anajidai haelewi basi mpe la wazi kuhusu hiyo tabia yake ambayo unahisi anafanya. Rafiki yako akielezwa basi utachukua jukumu la kumueleza lililokuwa linaendelea na hatua...
Unaweza pia kujaribu kupitia kwenye baadhi ya orphanage ukapata idea ya umri wa mtoto, jinsia, n.k unayekusudia kuadopt na huenda watakufahamisha utaratibu stahili. Vilevile utapata nafasi ya kujifunza mengi ikiwa na pamoja wengine walioadopt na ushauri mwingine mwingi. Ni mawazo yangu tu.
Faida na hasara za family friends zinategemeana na mambo mengi sana,mfano:nini misingi ya Ndoa yenu au mahusiano yenu. Misingi hiyo iko imara kiasi gani. Nini mtazamo wenu kuhusu hao family friends. Nini mipaka yenu,i.e.wapi family friends wanahusishwa na wapi hawahusishwi. Kuna wengine...
Haya ni yale mambo ya msingi mliyopaswa kujadili miaka saba au zaidi nyuma. Lakini kama halikufanyika basi linapaswa kujadiliwa na kusimamishwa/kuzuiwa mara moja. Fedha ni mojawapo ya yale mambo yaletayo vurugu katika ndoa hivyo ni budi swala hilo liangaliwe kwa undani na umakini.
Kwa wazazi...
Ndoa ni zaidi ya maudhi ya mume, hivyo huyo dada hatumii busara kutokuwajali na wanae. Kwa mzazi wa kike aliyeimara na instincts za kike kweli lazima aone vibaya kurudi saa 5 usiku hata kama si kila siku lakini mara nyingi.
Wakinamama mara nyingi sana wanajitahidi kila nafasi waipatayo kuwa...
Kama ni wa kwako atakuja tu siku moja, ila kwa sasa sio vyema kuwaharibia huyo mama na mtoto hayo maisha wanayoisha. Muache mtoto awe in a stable home, as far as hali halisi ndio kama ulivyoielezea.
Kuna zaidi ya hayo maendeleo ya mwanamke yanayozungumziwa. Endapo mliooana mnapendana na mna mipango ya pamoja, hilo huwa si rahisi kutokea. Ila kama mmekuwa na mahusiano yanayosuasua japo mpo ndani ya ndoa, then tegemea lo lote iwepo shule au isiwepo. Kiwepo kipato au kisiwepo.
Ni kweli...
Kwa kweli nakubaliana kabisa na De Novo, hali ya nchi yetu inakatisha tamaa. Kila nikifikiri sipati jibu na sijui vizazi vijavyo itakuwaje. Elimu mbovu, biashara ni lazima uwe na mtaji mkubwa au utoe kitu kidogo ili usogee, hospitali ndio basi tena, polisi ukiwa na kesi ni lazima uwe na gari au...
Si vizuri kuadvocate wanandoa kuachana, lakini si vibaya kuelewa kuwa hiyo nafasi ipo. Saa zingine watu tunafanya vitu kwa kufikiria matokeo fulani hayawezekani kutokea.
Kwa muda huo, huyo binti kwanza afocus kwenye afya yake. Hayo mengine yatachukua mkondo wake.
Siamini kuwa mkosaji hawezi...
Pole zake huyo dada kwa yaliyomkuta. Huyo jamaa hana ujasiri hata kidogo. Alitakiwa tu kuondoka, kwani mkewe angefanya nini? Siku inayofuata angejua arudije nyumbani, na sio kumpiga mtu na kusababisha uharibifu wa kiasi hicho.
Mbona Wanaume wana uwezo wa kuondoka nyumbani na hawaulizwi au...
Kama huyo dada hakuwa na huo ujasiri wa kusema huko nyuma, ni vyema akaendelea na ujasiri huo huo. Leo akitaka kusema atakuwa anataka kuumiza watu wawili. Mumewe na MMJ. Kwa maoni yangu hilo si jingine bali ubinafsi na kupenda kuona watu wanasonononeka juu yake.
Ingekuwa vyote tuvitakavyo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.