Kama alikuwa sio polisi kwanini asikamatwe pale alipofanya hivyo, kama atakua ni raia tujiulize alijiamini vipi mpaka kuweza kumtolea bastola waziri mstaafu mbele ya halaiki ya watu bila woga wowote.
Kama itakua imekutwa passport ya nchi nyengine nyumbani kwake kuna kipi kinangojewa asipelekwe mahakamani, ukitizamama tuhuma ambazo ametuhumiwa kwa kuanzia madawa ya kulevya, kuajiri wafanyakazi sio halali na sasa uraia wake na hatujui kitachofuata, ukiutazama musalsala unapata jibu.
Kinachoshangaza vipi mfanyabiashara au kampuni inawezaje miliki mpaka eka 3500, kwa kununua maeneo kidogo kidogo kwa wanavijiji bila kulipima, kuwa na hati au kuliendeleza, na huku hakuna hatua yeyote kuchukuliwa na serikali. Huyu inaonyesha hakutoa bure hizo eka 1500 ila aliona mbali, kwa...
Kitu ambacho nashindwa kufahamu ikiwa kitengo kinachoshughulika na madawa ya kulevya kimeanza kazi rasmi na tumeambiwa wamekabidhiwa majina kwo ili washughulikiwe, kwanini majina mengine yabaki mikononi mwa polisi, nadhani umefikia wakati kila kitengo kiachiwe kifanye kazi zake.
Serikali ni Serikali lakini inaongozwa kwa katiba na Sheria nchi yetu siyo Somalia, na haya mambo kama yatakuwa kweli tunaona madogo lakini yatatuulia uchumi wetu, wawekezaji na wafanyabiashara wanaona kinachendelea ulimwenguni kote kwa sasa.
Wewe unazungumza utumbo sasa, iachie serikali ifanye kazi yake imeanza kuwasiliana au kutuma maafisa wake kwenda huko. kwanini tuwe kama wao wakati Tanzania ni nchi salama na inaendeshwa kisheria.
kwani nini kinatisha kama ukitaka kufanyiwa uchunguzi au ukitakiwa kujieleza ukijifahamu wewe msafi. Kuna mbunge Uingereza alijipeleka mwenyewe Umarekani kuhojiwa mbele ya ma senator, baada ya kutuhumiwa na Umarekani alipokea Rushwa kutoka kwa Sadam Hussein, kwa hiyo mtu ukiwa msafi huna sababu...
Usitake kumpakazia kwasababu haziingii akilini, wananchi waliomchagua wanamfahamu vizuri, wakati wote ulikuwa wapi hukuupinga uraia wake, huwezi kujua uraia wa mtu kwa jina lake na unaweza kuwa raia kama mmoja wa wazazi wako ni Mtanzania.
Yusuf Manji amefikishwa mahakamani Kisutu katika kesi inayomkabili ya matumizi ya dawa za kulevya. Amepata dhamana ya shilingi mil. 10. iliyowekwa na CHARLES BONIFACE.
Kwa kweli nimeshangaa hili suala limechukuliwa kama kosa la kuhifadhi magaidi katika kampuni, suala la wafanyakazi kufanya kazi au kuajiriwa bila kibali lipo kawaida karibu ulimwenguni kote, wamejaa ukitizama katika nchi za kiarabu, Uingereza, Umarekani na hata nchi za kiafrika mfano South...
Hii ni hulka ya wenzetu wahindi huwa wana wafundisha na kuwakabidhi biashara watoto au ndugu zao ili hata bahati mbaya limekutokea jambo au hata umefariki biashara inaendelea, kinyume na sisi mpaka unakufa hata watoto zako hawajui shughuli zako matekeo yake unarithi mali zote zinapotea. Sidhani...
Mtumiaji dawa ya kulevya hawezi kuacha kwa kushitakiwa ama kuwekwa chini ya uangalizi, anatakiwa apelekwe hospitali na sio kwa kulazimishwa, mtumia madawa ya kulevya hawezi kuacha addiction kwa vitisho ila ni mpaka mwenyewe akubali kwanza ana tatizo, na kwa dhati mwenyewe ana nia ya kuchana na...
Kwa kweli sijawahi kuona kokote au kusikia, hata huko Ulaya au Marekani mtu anapelekwa mahakamani kwasababu anatumia madawa ya kulevya bila kukutwa nayo akitumia, hata hiyo rehab hupelekwi mpaka ukubali mwenyewe kwenda lakini huwezi kulazimishwa.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.