Naomba Mwongozo wa maswali au ushauri kuhusu interview aptitude test ya tarehe 24 mwezi
huu pale Udms Yombo No5 na 6!!!?
Naomba Mwongozo wa maswali au ushauri kuhusu interview aptitude test ya tarehe 24 mwezi
huu pale Udms Yombo No5 na 6!!!?
Mimi nimeitwa na hawa jamaa lakini sikuweza kuwajua vizuri ni watu gani maana nilikuwa bega kwa bega na bosi wangu kwa hiyo hata sikuweza kumuulizia alienipigia simu, tafadhari nijulishe muda ni saa ngapi na inatakiwa twende na viambatanisho gani, pia sikuipata fresh kampuni / taasisi hiyo maana si unajua katika kuhangaika tunatuma CV sehemu nyingi, please naomba ufafanuzi ndugu yangu
There is a saying in aviation "You haven't crashed until you've crashed. Until then, keep flying the plane".
mi pia nimeitwa, duh kumbe tupo wengi,ni GEPF, nimeitwa kwa nafas ya acountant, nimeambiwa niende na pen pensel na lula,
Ukisha ambiwa uje na peni na karatasi bila kusahau lula unataka nini tena? chukua vitini vyako vyote vya chuo vya professional yako kisha meza kimoja baada ya kingine. Ukimaliza jikumbushie vihesabu vidogovidogo vya ufahamu kama Variation, simple algebra. baada ya hapo usikae mbali na englishi hasa structure. Kiufupi maticulation paper ndo mfano wa unachokwenda kukutana nacho. Kama vipi na Mofimu za ngeli
Jamani naombeni kujuzwa muda wa kufika maana sikuwa makini maana nilikuwa na bosi wangu, please msaada wenu tafadhari
There is a saying in aviation "You haven't crashed until you've crashed. Until then, keep flying the plane".
Me pia nimepigiwa muda si mrefu,halafu wanasema yombo 6 wakati pale ud haipo,mwisho yombo 5
mtiani wa kwanza ni kusoma ratiba
we utakuwa wa 2010 kurudi nyuma mjomba...hata yombo cafeteria hujaiona acha niku-update, cafeteria ya hall 6 ilifutwa mjomba...ofisi za daruso ndo zilihamia hapo ilipokuwa cafe ya hall 6...kale kapori kalikokuwa mbele ya yombo three kalifyekwa, sasa hivi wameongezea yombo 4 na yombo 5...majengo ambayo yanafanana kabisa na theatre one&two sema haya yana ghorofa kama nkurumah....mjomba ile packing iliyokuwa pale katikati ya nyumba ya Mkandala na NBC bank imeanza kusongwa, kuna tuvibanda wanajenga pale nyuma sijui twa kazi gani...pale UDBS yanashushwa majengo ya hatari mjomba sijui yote ya kusomea yale au niaje (nisamehe kama uliondoka enzi udbs haijazaliwa)...mjomba unakumbuka lile eneo la wazi lililokuwa pale COET opposite na NMB bank...nimepita juzi nimekuta limezungushiwa mabati yani kuna ujenzi unaendelea sikufanikiwa kujua ni ujenzi wa nini unaendelea. Mjomba unakumbuka enzi zile za FASS, FIVE, FoS,IJMS, Bcom etc...hatuna tena enzi hizo, siku hizi wanaitwa CASS, COICT, School of law,SJMS, UDBS respectively....mambo yamebadilika sana mjomba, ukipata muda tembelea chuo chako cha zamani upate kujionea mwenyewe, ila pamoja na mabadiliko hayo yote kuna mambo bado hayajabadilika mpaka leo....tangu ile 1st class ya yule rafiki yako aliyemaliza miaka kadhaa mbele yako kitengo cha sheria, haijapata kutokea first class nyingne mpaka leo kwenye tasnia ya sheria, si unakumbuka ma-TO wa chuo walikuwa wanatokea sana science na mara chache economics, hiyo hali bado haijabadilika mpaka leo mjomba....nina mengi sana ya kukuandikia mjomba ila kwa leo naomba niishie hapa, panapo majaliwa nitakuandikia barua nyingine....Ubarikiwe sana Mjomba
IF U LIVE EACH DAY AS IF IT WAS YOUR LAST, SOMEDAYS U WILL MOST CERTAINLY BE RIGHT-stEvE jObS
Hii ni kazi ya kwanza kabisa kuomba kwa kutuma barua posta na kuitwa,
Peni ,Penseli na Rula saa 2 nipo yomboni---bahati iliyoje
"Be not afraid!" Giovanni Paolo Segundo
Follow Us Here