Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ssra na mafao ya wafu

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      shabibu's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Posts : 2
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Ssra na mafao ya wafu

      Salaam,
      Nikiamini kuwa Mola ni mkarimu na mwema kwetu kwa kutujaalia afya, uzima na uhai hata muda huu. Ni mapenzi yake ya dhati ambayo kamwe binadamu hata wawe wema kiasi gani hawawezi kuyadiriki. Ni maajabu twashangaa vitengenezwa badala ya kushangaa mtengenezaji wake. Sitaki kuamini kuwa watanzania wote tuna akili kama za baadhi ya watawala wetu ambao hawaamini kuwa watawaliwa wao wana akili na shuleni au chuoni wanaenda kutafuta maarifa tu.

      Ni ukweli dhahiri usiohitaji, lenzi mbinuko wala mbonyeo kuukuza wala kuudogosha ili watu wauone. Ukweli kuhusu ukakasi wa sheria mpya ya Mifuko ya Jamii kama ilivyopitishwa bungeni na kushadidiwa ni Mamlaka ya mifuko ya Hifadhi (SSRA). Ni ukweli ambao takriban kila alochangia mafao yake kule ameshtushwa na kushtuka pale aliposikia kuwa michango yake itakuwa salama ikitumika kuendeshea shughuli mbalimbali za kiuchumi kwa 'maslahi ya wenye nchi'.

      Nimejaribu kupitia taarifa mbalimbali kupitia mitandao kutaka kujua na kubaini ni kwa kiasi gani mafao ya wafanyakazi hawa yatawasaidia kujikwamua baada ya kufikisha miaka 55 ya kustaafu kwa mujibu wa sheria.

      Hii ni kwa sababu wastani wa umri wa kuishi kwa Tanzania ni kati ya miaka 51 na Kwa kifupi nilichogundua ni kuwa kama wapo watakaofanikiwa kupata mafao hayo basi watayatumia au yatatumika kununulia jeneza, sanda na kusakafia makaburi yao badaya ya kuyatumia kuendeshea maisha yao ya hapa duniani.

      Miongozi mwa vyanzo mtandao hivyo ni: Index Mundo Tanzania Life expectancy at birth, UNDP Human Development Report 2011, etc. kama zilivyoorodhesha chini.

      Tanzania Life expectancy at birth - Demographics
      http://hdrstats.undp.org/images/explanations/TZA.pdf
      Average Life Span Expectancy Chart - How Long Will I Live

      Yawezekana nimekuwa na mawazo ya kishabiki zaidi wakati napitia vyanzo hivyo, ila naamini takwimu zilizowekwa ni sahihi au zinakaribia kwenye ukweli. Kwa mantiki hii wangapi wataishi kuchukua na kutumia mafao yao zaidi ya kutumika kununulia sanda na majeneza na kujengea makaburi yao au kufanyia arobaini na kusomea khitma!

      Tumewasikia Mh. Job Ngugai, Nicholaus Mgaya na wanaharakati wakionesha msimamo unaokaribiana au kushabihiana na ule wa wafanyakazi hasa wa hali ya chini wa kutoridhika na Marekebisho ya Sheria ya mifuko ya jamii.

      Naombeni wataalamu na wataaluma wa fani husika watusaidie kuelewa manufaa ya sheria hii badala ya kulalamika kwani kwangu na kwa ufahamu wangu finyu haya ni MAFAO YA WAFU.

      Nakutakieni kila la kheri na nakuombeni tusimtangulie Mungu katika uumbaji wake na makadirio yake kwa viumbe wake bali tumtegemee yeye kwa dhati kwani wanasiasa na watawala wanataka tuwaabudu na kuwanyenyekea ili watende yenye manufaa kwetu. Nani anajua, yawezekana tukaishi miaka au umri wa ahadi yaani 70+ na mafao haya yakatusaidia kweli!


    2. #2
      Cul Naf's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th February 2012
      Posts : 22
      Rep Power : 375
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Ssra na mafao ya wafu

      Umeongea kitu cha maana sana ndugu...

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...