heshima nyingi kwa wakuu wote mliopo humu jamvini, na poleni na majukumu ya kitaifa na kifamilia. Mimi ni kijana wa kitanzania ninayetarajia kuhitimu masomo yangu agosti mwaka huu kutoka taasisi ya usimamizi wa kodi "institute of tax administration" ngazi ya stashahada "diploma in customs and tax administration". Katika kozi yangu nimepata utaalam kuhusu maswala ya kodi za ndani na usimamizi wa forodha, na kutokana na ujuzi huo nilioupata naweza kufanya kazi katika nafasi kama vile,:
ushauri wa kodi
kwenye kampuni za "clearing"
mhasibu msaidizi.
kutokana na maelezo hayo wakuu naomba mtu anayehitaji au anayefahamu sehemu wanahitaji mtu mwenye sifa zangu asisite kuwasiliana nami kupitia [email protected]
nawasilisha ombi langu

Reply With Quote
Follow Us Here