Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

    Report Post
    Results 1 to 10 of 10
    1. #1
      itagata's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th September 2011
      Posts : 68
      Rep Power : 404
      Likes Received
      8
      Likes Given
      1

      Default Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      SEKRETARIATI ya ajira ilipoanzishwa moja ya lengo lake ilikuwa ni kuajiri watu wenye sifa ikiwa ni pamoja na kupunguza urasmu uliokuwa ukitokea wakati taasisi zinazojitegemea na mamlaka za serikali za mitaa zilipokuwa na jukumu la kuajiri watumishi wake.
      Pamoja na malengo hayo mazuri, hali imekuwa tofauti sana na ni afadhar mamlaka za serikali za mitaa pamoja na taasisi zinazojitegemea zilipokuwa na mamlaka ya kuajiri wafanyakazi wake, hali ilivyo sasa katika sekretariati ya ajira ni mbaya, bila kujuana au kutoa kitu kidogo usitegemee kupata kazi, imekuwa ni dili kubwa kwa ma-HR waliopo hapo na wenye jukumu la kuajiri.
      Ninachojiuliza jamani wana JF kweli hadi Afisa Mtendaji wa Kijiji anasafiri kutoka Kigoma kuja Dar kwa ajili ya kufanya interview? Mi napingana sana na utaratibu huu kwani tunaoumia wengi ni watoto wa masikini tunaoka mikoa ya mbali na Dar.
      Kwanini serikali isizipe na kuimarisha mikoa ili iweze kuajiri wafanyakazi wake badala ya kutegemea makao makuu ya secretariat pekee? Kama ni lazima utumishi waendelee kuajiri basi wachague baadhi ya kada angalau zenye vyeo vya juu ili wafanyakazi wenye vyeo vidogo waajiriwe na mamlaka za mikoa badala ya wote kutegemea kufanyiwa usaili na makao makuu ya utumishi.
      Nina amini kuwa sisi watoto wa masikini tuliomaliza vyuo vikuu ambao hatuna uwezo wa “kuhonga” milioni moja ili tupewe kazi na tunaochangiwa na kijiji ili tupate nauli ya kuja Dar kufanya usaili ndio tunaoumia.
      Nawaomba wapiganaji wetu, Zitto, Mbowe, Tundu, Mnyika na wapiganaji wengine wenye mapenzi mema na maisha ya vijana walipigie kelele hili ili angalau interview ziwe zinafanyika kwa ngazi ya kanda au mikoa ili kuwapa fursa watoto wa masikini kupata ajira.
      Nimeamua kuandika mawazo yangu haya kwenu wana JF kwani nimefanya interview 3 ambazo nina uhakika nilifanya vizur lakini mpaka leo sijapata hiyo ajira, na ninatoka mikoa ya mbali nalazimika kusafiri siku mbili ili kufika Dar.

    2. Miaka 50

    3. #2
      panadol's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 11th February 2012
      Posts : 352
      Rep Power : 0
      Likes Received
      42
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Mleta hoja acha uzushi kuzushia watu kama wanakula rushwa inamaana wote waliopata ajira kupitia utumishi wamehonga?huo ni uzushi sana ukweli ni kwamba pale watu wanapata ajira kwa uwezo wao mimi nina jamaa zangu wameajiriwa serikalini kupitia utumishi bila hongo yoyote ukikosa ujue umekosa hukufanya vizuri aliyekwambia wewe lifanya vizuri kwa interview zako zote tatu ni nani,wewe umejuaje? Wangapi wanamaliza shule wakijiamini watafaulu na matokeo yakitoka huwa wanakuwa wamefeli,mbona hawalaumu iweje wewe ulaumu au unapewa maswali na mitihani ya interview? Acha uongo na unafiki jijue unakosa hujakidhi viwango,kama uko vizuri kwa nini private sekta zisikuajili unakomalia serikalini tu?acha uzushi jipange vizuri siku moja utafanikiwa lakini si kulalama na kusingizia watu wanaingia kwa rushwa na kubebwa kumbe wewe mwenyewe unafeli interview kwa kutokujiandaa vizuri,suala la interview ziwe zinafanyikia kwa kanda hilo naliafiki ili kuokoa gharama za watu wote kuja dar,mengine ya rushwa na undugu siyaafiki ni uzushi mtupu na kuchafua watu!

    4. #3
      salosalo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2012
      Location : Arusha
      Posts : 528
      Rep Power : 538
      Likes Received
      133
      Likes Given
      36

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Quote By itagata
      SEKRETARIATI ya ajira ilipoanzishwa moja ya lengo lake ilikuwa ni kuajiri watu wenye sifa ikiwa ni pamoja na kupunguza urasmu uliokuwa ukitokea wakati taasisi zinazojitegemea na mamlaka za serikali za mitaa zilipokuwa na jukumu la kuajiri watumishi wake.
      Pamoja na malengo hayo mazuri, hali imekuwa tofauti sana na ni afadhar mamlaka za serikali za mitaa pamoja na taasisi zinazojitegemea zilipokuwa na mamlaka ya kuajiri wafanyakazi wake, hali ilivyo sasa katika sekretariati ya ajira ni mbaya, bila kujuana au kutoa kitu kidogo usitegemee kupata kazi, imekuwa ni dili kubwa kwa ma-HR waliopo hapo na wenye jukumu la kuajiri.
      Ninachojiuliza jamani wana JF kweli hadi Afisa Mtendaji wa Kijiji anasafiri kutoka Kigoma kuja Dar kwa ajili ya kufanya interview?Mi napingana sana na utaratibu huu kwani tunaoumia wengi ni watoto wa masikini tunaoka mikoa ya mbali na Dar.
      Kwanini serikali isizipe na kuimarisha mikoa ili iweze kuajiri wafanyakazi wake badala ya kutegemea makao makuu ya secretariat pekee? Kama ni lazima utumishi waendelee kuajiri basi wachague baadhi ya kada angalau zenye vyeo vya juu ili wafanyakazi wenye vyeo vidogo waajiriwe na mamlaka za mikoa badala ya wote kutegemea kufanyiwa usaili na makao makuu ya utumishi.
      Nina amini kuwa sisi watoto wa masikini tuliomaliza vyuo vikuu ambao hatuna uwezo wa “kuhonga” milioni moja ili tupewe kazi na tunaochangiwa na kijiji ili tupate nauli ya kuja Dar kufanya usaili ndio tunaoumia.
      Nawaomba wapiganaji wetu, Zitto, Mbowe, Tundu, Mnyika na wapiganaji wengine wenye mapenzi mema na maisha ya vijana walipigie kelele hili ili angalau interview ziwe zinafanyika kwa ngazi ya kanda au mikoa ili kuwapa fursa watoto wa masikini kupata ajira.
      Nimeamua kuandika mawazo yangu haya kwenu wana JF kwani nimefanya interview 3 ambazo nina uhakika nilifanya vizur lakini mpaka leo sijapata hiyo ajira, na ninatoka mikoa ya mbali nalazimika kusafiri siku mbili ili kufika Dar.
      Je unaconclude kuwa kuna rushwa 7bu umefanya interview 3 bila mafanikio au 7bu kuna mtu alikuambia ametoa rushwa na kufanikiwa?
      Angalia vizuri hizo red hapo juu kwani zina mambo sana
      Kama wakiruhusu kanda kuajiri haina maana kuwa gharama zitapungua bali zitaongezeka zaidi, mfano Mtwara wakitangaza nafasi yoyote na mtu wa Bukoba akaomba na kuitwa kwenye interview unadhani itakuwaje? ukisema kila watu waajiriwe kwenye Mkoa wao utapalilia Ukabila na kuvunja umoja wetu watanzania. Ajira za serikalini ni haki ya kila raia bila kujali mkoa au ukanda atokako mwombaji.

      Majina ya Wabunge uliyoyataja hujayatendea haki, ilikuwa vizuri uombe wabunge kwa ujumla wao waliisemee hii unayodhani ni kero kwako.Yeyote mbunge atakayeliona ombi lako na kuliafiki atalisemea.

      Kumbuka kuwa nafasi za ajira ni chache kuliko Wahitaji,hivyo unapokosa usichukulie umeonewa wakati wote maana hata wenzako huwa wanajibu vizuri interview kama au zaidi ya wewe.

      Kama ni issue ya rushwa basi hiyo inabidi ichunguzwe au wewe mwenyewe wakikuomba hao ma HR nenda kawachukulie pesa TAKUKURU wapelekee wakamatwe ili kukomesha tabia na kuondoa mbegu hii mbovu.

      Au tuwaombe tume ya ajira wajaribu kuweka uwazi katika interview process, au wachunguzwe kwa tuhuma wanazotuhumiwa nazo

    5. #4
      Nicholas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Posts : 5,253
      Rep Power : 3668
      Likes Received
      1325
      Likes Given
      2214

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Pengine kazi yako uliyopata haikuwa chagua la wenye network.Shukuru kwa hilo?
      SIMPLY THE RADICAL: I can`t wait to see the criminalization of CCM,UWT,Bunch of Policemen/women,and all wanafiki na wachumia tumbo.

    6. #5
      obama wa bongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2012
      Location : WHITE HOUSE
      Posts : 1,031
      Rep Power : 621
      Likes Received
      274
      Likes Given
      229

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      huyu bwana itagata ,anonesha anatabia za kulalamika sana na unafiki ndani yake .anataka psrs waonekana wa image mbaya kwa wata nzania kwa sabaubu hajapata ajira ,yeye kama ameona kuna dalili za rushwa kwa nini asipeleke taarifa takukuru
      alafu ana usiasa ndani yake kwanini ?zitto,mbowe,mnyika kwani hao ndo wawakilishi pekee? alafu si kila interview lazima utakayo fanya upate!
      but usikate tamaa ipo siku tutapata kijana mwenzangu


    7. #6
      Kilahunja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2011
      Posts : 935
      Rep Power : 562
      Likes Received
      161
      Likes Given
      3

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Mbowe, zito, mnyika, tundulisu..HAO NDO WABUNGE PEKEE UNAOTAKA WAKUSAIDIE? KWANINI USISEME WABUNGE WOTE KWA UJUMLA..

      Pia kazi zinazotangazwa ni chache na watu ni weng ukikosa haimanish umeonewa bali kuna wakali zaid yako kumbuka ukizidiwa hata point moja anachukuliwa aliekuzid,na ikitokea mko draw, anangaliwa mwenye extra atributes hata moja 2..so jipange zaid

    8. #7
      uwiii's Avatar
      Member Array
      Join Date : 25th June 2012
      Posts : 14
      Rep Power : 350
      Likes Received
      4
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Mimi sitaki kuamini hilo kabisaaaa!Kuna watu wanapata kazi bila kufahamiana na mtu wala kuwa na cha njano kupitia taasisi hiyo.Nafikiri mimi(Bado ni nasaka job) na wewe tujipange tu upya,tutapata tu siku moja hizo nafasi na sisi.

    9. #8
      itagata's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th September 2011
      Posts : 68
      Rep Power : 404
      Likes Received
      8
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Quote By panadol
      Mleta hoja acha uzushi kuzushia watu kama wanakula rushwa inamaana wote waliopata ajira kupitia utumishi wamehonga?huo ni uzushi sana ukweli ni kwamba pale watu wanapata ajira kwa uwezo wao mimi nina jamaa zangu wameajiriwa serikalini kupitia utumishi bila hongo yoyote ukikosa ujue umekosa hukufanya vizuri aliyekwambia wewe lifanya vizuri kwa interview zako zote tatu ni nani,wewe umejuaje? Wangapi wanamaliza shule wakijiamini watafaulu na matokeo yakitoka huwa wanakuwa wamefeli,mbona hawalaumu iweje wewe ulaumu au unapewa maswali na mitihani ya interview? Acha uongo na unafiki jijue unakosa hujakidhi viwango,kama uko vizuri kwa nini private sekta zisikuajili unakomalia serikalini tu?acha uzushi jipange vizuri siku moja utafanikiwa lakini si kulalama na kusingizia watu wanaingia kwa rushwa na kubebwa kumbe wewe mwenyewe unafeli interview kwa kutokujiandaa vizuri,suala la interview ziwe zinafanyikia kwa kanda hilo naliafiki ili kuokoa gharama za watu wote kuja dar,mengine ya rushwa na undugu siyaafiki ni uzushi mtupu na kuchafua watu!
      nashukuru kwa maoni yako kwa mtizamo wako, ni kweli sio wote wanaopata kazi kupitia utumishi wanahonga, lakini si jambo la kupinga kuwa hakuna rushwa katika mchakato wa kupata ajira kupitia utumishi. najua umetumia maneno makali katika kuchangia uzi huu kwani yawezekana wewe mwenyewe ni sehemu ya hao wa utumishi, ila kwa taarifa yako kama hujui, nina rafiki yangu ambae alifanya usaili mara mbili akakosa, mara ya tatu akatafuta mtu akamuunganisha na wahusika akatoa "mpunga" huyo mhusika akalisimamia jina lake kuanzia kwenye '' k-ushort list'' mpaka interview zote na sasa yupo kazini. una haki yako kupinga lakini ukweli ndo ulivyo.

    10. #9
      itagata's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th September 2011
      Posts : 68
      Rep Power : 404
      Likes Received
      8
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Quote By Kilahunja
      Mbowe, zito, mnyika, tundulisu..HAO NDO WABUNGE PEKEE UNAOTAKA WAKUSAIDIE? KWANINI USISEME WABUNGE WOTE KWA UJUMLA..

      Pia kazi zinazotangazwa ni chache na watu ni weng ukikosa haimanish umeonewa bali kuna wakali zaid yako kumbuka ukizidiwa hata point moja anachukuliwa aliekuzid,na ikitokea mko draw, anangaliwa mwenye extra atributes hata moja 2..so jipange zaid
      Samahani kama ntakuwa nimeeleweka tofauti kwa kuwataja hao Majemedali wetu wachache, lakini katika kazi yoyote ili ifanyike lazime kuwe na viongozi, hawa nimewataja kama makamanda wa mstari wa mbele katika mapambano ya kuleta haki! kama uliusoma vizuri uzi wangu, nilimalizia na kusema ''na wapiganaji wengine'' hii inaamanisha sio wao peke yao.

    11. #10
      josam's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd November 2011
      Posts : 203
      Rep Power : 419
      Likes Received
      32
      Likes Given
      530

      Default Re: Mbowe, Zitto, Mnyika, Tundu tusaidieni vijana kulizungumzia hili

      Tanzania hii, organisation zote za serikali BILA RUSHWA HAKUNA HUDUMA!!!

      Bodi husika inatakiwa kulipa gharama zote za usafiri, malazi na chakula kwa muda wote wa interview.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...