Habari wakuu.
Sikujua hii post niweke wapi. Kama mtaona humu nimekosea...mezea!
Nina swali la muhimu sana kwangu litakalo nisaidia kufanya maamuzi magumu.
Ni vipi upatikanaji wa part time jobs hapo London? Na je ni rahisi mtu kuweza kujilipia accomodation na food kwa kupitia part time jobs hizi. Naskia accomodation iko juu. Vipi kuhusu shared apartments indian style?
Nataka nipige ka Masters ila mfukuoni na hela hio hio ya ada tu!
Aksante!
You only live once, but if you do it right, once is enough.- Mae West
Re: KWA MLIOKO LONDON au mliokuwepo mkarudi. Ushauri.
Unaweza kusoma na kumaliza. Gharama ya London ipo juu na pia upatikanaji wa kazi siyo rahisi sana. Cha kukushauri tafuta network ya watu waliopo London wakupatie michongo kwanza then ujue utafanyeje. Mi sipo huko naishi Mlandizi mitaa ya kwa mama peuke, ningekusaidia.
Re: KWA MLIOKO LONDON au mliokuwepo mkarudi. Ushauri.
Siko London niko USA....
Kama jamaa livyokwambia hapo Tafuta network ya watu hapo London angalau wakusaidie accomodation unaweza kuchemsha kazi unawezausipate mapema ingawa uzuri wa miji mikubwa kazi zisizo rasmi hazikosekani ni wwkuchangamuka na kutokuwa na noma ....anyway wasiliana na wabeba box wa London
Re: KWA MLIOKO LONDON au mliokuwepo mkarudi. Ushauri.
tatizo ni fees,kama hiyo ni sorted just drop in.Kazi ni ngumu kupata sababu ya dip in the economy,but all in all huwezi lala njaa na accomodation zipo-with time probably 3 months you will be up and running
Re: KWA MLIOKO LONDON au mliokuwepo mkarudi. Ushauri.
Nyamgluu tafuta hela ya kupanga kama miezi 3 na chakula.
ukifika jichanange na wa bongo utafanikiwa kupata kazi siyo shida ukiwa na karatasi za kufanyia kazi.
Vijiwe vikubwa vya wa bongo london ni canning town (club afrique) na barking club ambassador.
Ukienda maeneo ya eastham high street au green street haitakuchukua dakika kumi na tano barabarani kukutana na mtu anaongea kiswahili.Kila lan heri na nyumba za kushea zipo kibao.
-
Re: KWA MLIOKO LONDON au mliokuwepo mkarudi. Ushauri.
mkuu london ni mji mkubwa,kwa tanzania unaweza linganisha na dar.gharama za maisha zipo juu kiukweli hususana kodi ya kupanga nyumba.na pia kazi hizi za kawaida uwa inategemea na unavyojituma kutafuta na pia hali ya uchumi kwa kipindi hicho.kuna wakati unaweza ukapata kazi hata ndani ya wiki tu lakini kuna kipindi unaweza sota hata miezi 3 hujapata kazi.na kiukweli maisha ya ulaya ni kama kwenye bible vile asiyefanya kazi na asili,vinginevyo uwa na pesa ya kutosha.kila la kheri mkuu
Follow Us Here