wanaJF nisaidie sheria za kazi zinasemaje kuhusu mtumishi wa umma anayeenda kusomea kada tofauti na ile aliyoajiriwa nayo? mf.niliajiliwa kama mwalimu nina miaka 8 kazini na nimejiendeleza kwenye evening class nikafikia vigezo vya kusomea Udaktari MD,mwajiri yaani serikari atanilipia masomo?mshahara wangu wa ualimu nitaendelea kupata wakati ninasoma?nikimaliza masomo nitaomba kuajiliwa upya au nitaamishwa tu kwenda department nyingine? Naomba msaada japo kidogo tu,nawasilishaj.
Hongera sana,hapo unaomba kupangiwa kazi ya fani yako baada ya kuhitimu,me ofcn kwetu kuna mtu alikua mlinzi akasoma acc kwa ngazi ya adv dip saiv ni auditor
Kweli jf tunatisha kwa knowledge anuwai. kaka gerrad kwanini waajili wengine hawabadili increment za mshahara kwa wakati?
yaani ni vigezo gani vinatumika kupandisha madaraja ya mshahara?? Are they open ???
Increment na madaraja ni vitu viwili tofauti. Increment ni nyongeza ya kila mwaka yaani kila tarehe 1 Julai unatoka ngazi kidato kimoja kwenda kingine mfano TGTS C1 kwenda TGTS C 2. Hii hufanyika kama hakuna nyongeza ya mshahara. Kupandfisa daraja (Promotion) ni kutoka level/ ngazi moja ya mshahara kwenda nyingine mfano kutoka Afisa Elimu Msaidizi III (AEMIII) TGTS C kwenda AEMII TGTS D. Hii ni kati ya miaka mitatu hadi mitano tangu uanze kazi au last promotion.
Sababu zinazochelewesha kuanda daraja zipo nyingi mfano kutokuwa na TSD Na, kuchelewesha vyeti/ kujaza mikataba ya ajira, kuhama toka wilaya moja kwenda nyingine hivyo kupoteza taarifa, kutokuwepo kwenye mapendekezo ya mwajiri, matatizo ya kinidhamu kama utoro n.k, poor performance, uzembe wa ofisi kutotunza kumbukumbu, uhaba wa bajeti (kasungura kadogo) na nyingine zinazofanana na hizo. Lakini unatakiwa kupewa promotion si zaidi ya miaka mitano
"Tumefika hapa kutokana na udhaifu wa Rais Kikwete,Uzembe wa Bunge na Upuuzi wa CCM"
Hapo hapo mkuu Gerrad inabidi uendelee kutupatia somo zaidi,mfano mimi nimeajiriwa mwl wa cheti mwaka 2006 na juzi tu nimemaliza BA ed na juzi mwezi wa 7 ndio nmepata first appointment na zaidi nmeomba ajira mpya,je unanishauri nn kwamba nienda ajira mpya au niandike barua kwa mwajiri wangu? Na zaidi nahofu je kweli watanihamisha pale nlipokuwepo awali na kwenda sehem nyingine? Nishauri mkuu maana naambiwa wakuu wapo Moro wanapangia watu Mikoa,natanguliza shukrani
Wewe kama una transcript kimbia haraka sana kakabidhi kwa Mwajir wako kwani nina uhakika hujafikia TGTS D so ukipeleka mara moja unabadilishwa kuwa Afisa Elimu II. Pia utapelekwa sekondari kwani kwa sasa hairuhusiwi Mwalimu mwenye shahada kufundisha huko msingi. Ukiomba Mkoa mwingine utapoteza haki zako zote PSPF na kila kitu kwani utaanza upya na by the way jina lako lazima litaonekana kwenye database ya wizara kwamba wewe ni mwajiriwa tayari
"Tumefika hapa kutokana na udhaifu wa Rais Kikwete,Uzembe wa Bunge na Upuuzi wa CCM"
GERRAD mimi nimemaliza MASTERS YA MANAGEMENT NINA BACHELOR PIA YA MANAGEMENT NIMESPECIALIZE KWENYE ORGANIZATIONAL MANAGEMENT NA HUKO NYUMA NILIKUA MWALIMU NA SASA NILIFANYIWA RECATEGOLIZATION NA KUA AFISA UTUMISHI NINA MWAKA TOKA NIPATE CHEO HIKI SASA NINACHOOMBA KUJUA ILI NIWE MKUU WA IDARA NATAKIWA NIWE NA UZOEFU WA MIAKA MINGAPI INGAWA HIYO AJIRA YA UALIMU NILIITUMIKIA KWA MIAKA 12
God doesn't require us to succeed; he only requires that you try
Follow Us Here