Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Nafasi za Kazi na Tenda (Job Vacancies + Tenders)


Nafasi za Kazi na Tenda (Job Vacancies + Tenders) Fuatilia nafasi mbalimbali za kazi zilizotumwa na wanachama wetu. Kama unahitaji mfanyakazi/kufanya kazi basi tufahamishe kwa kuwasiliana nasi.


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 4th February 2010, 07:59 AM   #1
Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia
Ogah Ogah is offline 4th February 2010, 07:59 AM

Fuata hii link

http://www.tanzaniaembassy.or.jp/english/e_index.html

gonga hapo kwenye "What's New"

All the Best

Ogah
JF Premium Member
Points: 5,280,770, Level: 100 Points: 5,280,770, Level: 100 Points: 5,280,770, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
Join Date: Fri Mar 2006
Posts: 3,412
Thanks: 1,392
Thanked 383 Times in 211 Posts
Views: 1452
Reply With Quote
  #2  
Old 9th February 2010, 08:10 AM
Kabengwe Kabengwe is offline
Kabengwe never trust appearances
Senior Member
Points: 67,331, Level: 100 Points: 67,331, Level: 100 Points: 67,331, Level: 100
Activity: 9% Activity: 9% Activity: 9%
 
Join Date: Tue Oct 2009
Location: Kusadikika
Posts: 64
Thanks: 72
Thanked 29 Times in 20 Posts
Rep Power: 21
Kabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enoughKabengwe will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

03 / Feb / 2010
AJIRA MPYA 2009 - 2010


WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa anapenda kuwatangazia Watanzania wenye sifa kutoka Bara na Visiwani, kuomba kazi zilizotangazwa hapa chini. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inazingatia usawa wa kijinsia katika kutoa ajira. Hivyo Wanawake wenye sifa wanahimizwa kuomba.
Nafasi zinazotangazwa ni kama ifuatavyo:-

1. AFISA MAMBO YA NJE DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS D, TSH. 322,460.00) - NAFASI 33 (KITUO : DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR)
SIFA ZA MWOMBAJI
i. Awe mwenye Shahada ya Sanaa (B.A.) ambaye amejiimarisha (major) katika fani ya Uhusiano wa Kimaataifa (International Relaions), Sheria au Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
SIFA ZA ZIADA
i. Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani, Kihispania na Kiarabu.
ii. Mwenye Shahada/Stashahada ya Uzamili (Masters/Postgraduate Diploma) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapo ya fani zifuatazo:-
a. Uhusiano wa Kimataifa;
b. Public Policy;
c. Uchumi;
d. Biashara ya Kimataifa; na
e. Sheria ya Kimataifa.

KAZI ZA KUFANYA
i. Kuandaa Muhtasari, nakala na taarifa zinazohusu masuala ya mahusiano ya Kimataifa;
ii. Kuhudhuria mikutano mbalimbali;
iii. Kuandaa mahojiano;
iv. Kufuatilia masuala mbalimbali ya kimataifa;
v. Kufanya utafiti juu ya masuala mbalimbali yanayohusu uchumi, siasa na jamii; na
vi. Kutunza kumbukumbu za matukio mbalimbali.

2. AFISA UTUMISHI DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS D, TSH. 322,460.00) – NAFASI 1 (KITUO : ZANZIBAR)
SIFA ZA MWOMBAJI:
i. Awe mwenye Shahada ya kwanza ya Sayansi ya Jamii au Sanaa kutoka katika Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali ambao wamejiimarisha (major) katika mojawapo ya fani zifuatazo:
a. Menejimenti ya Raslimali Watu (Human Resources Management) ;
b. Elimu ya Jamii (Sociology) ;
c. Utawala na Uongozi (Public Administration) ;
d. Mipango ya watumishi (Manpower Planning).

ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
SIFA ZA ZIADA
Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani, Kihispania na Kiarabu.
KAZI ZA KUFANYA:
i. Kutunza Kumbukumbu sahihi za watumishi wote katika Wizara ;
ii. Kutafsiri na kushughulikia utekelezaji wa Miundo ya Utumishi ;
iii. Kutafiti, kuchanganua na kukadiria idadi ya watumishi wanaohitaji mafunzo ;
iv. Kuandaa na kupanga mipango ya mafunzo ya muda mfupi na mrefu ;
v. Kukadiria na kupanga mahitaji ya vifaa vya mafunzo kwa kushirikiana na vyuo vilivyopo chini ya sekta zinazohusika;
vi. Kukusanya, kuchambua na kupanga takwimu na kumbukumbu zote zinazohusu mipango ya watumishi.

3. AFISA TAWALA DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS D, TSH. 322,460.00) – NAFASI 2 (KITUO : DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR)
SIFA ZA MWOMBAJI:
i. Awe mwenye Shahada ya kwanza kutoka katika Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapo ya fani zifuatazo:
a) Utawala
b) Elimu ya jamii
c) Sheria (baada ya intenship)
d) Menejimenti Umma
e) Uchumi.

ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
SIFA ZA ZIADA
Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani Kihispania na Kiarabu.

KAZI ZA KUFANYA
i. Kuweka kumbukumbu za matukio muhimu ya Serikali
ii. Kuainisha, kuchambua na kushauri kuhusu matatizo ya watumishi
iii. Kusimamia nidhamu ya watumishi
iv. Kusimamia utekelezaji wa sheria, sera, kanuni na Taratibu mbalimbali serikalini kutegemea mahali alipo.
v. Kusimamia kazi za utawala na uendeshaji katika ofisi za Serikali.

4. MCHUMI DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS D, TSH. 322,460.00) – NAFASI 9 (KITUO : DAR ES SALAAM)
SIFA ZA MWOMBAJI:
i. Awe wenye shahada ya kwanza kutoka vyuo vinavyotambulika na serikali ambao wamejiimarisha (major) katika mojawapo ya fani zifuatazo:
a) Uchumi (Economist)
b) Takwimu (statistics)

ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.
SIFA ZA ZIADA
i. Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani Kihispania na Kiarabu.
KAZI ZA KUFANYA
i. Kuhudumia kamati mbalimbali za Bunge (kamati za mahesabu ya serikali, kamati za Uchumi na Fedha, kamati ya mahesabu ya Mashirika ya Umma)
ii. Kukusanya takwimu na taarifa mbalimbali za kiuchumi kwa ajili ya uchambuzi na uandaaji wa sera na mipango ya kiuchumi na kijamii.
iii. Kufanya utafiti juu ya masuala mbalimbali yatokanayo na utekelezaji wa sera za uchumi jumla
iv. Kufanya utafiti na kubaini fursa zilizopo katika sekta husika.
v. Kuchambua na kutafsiri takwimu na taarifa mbalimbali.

5. MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS B, TSH. 151,240.00) – NAFASI 7 (KITUO : DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR).
SIFA ZA MWOMBAJI:
i. Awe mhitimu wa Kidato cha sita;
ii. Awe na cheti cha utunzaji wa kumbukumbu katika fani ya Masjala kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali.
KAZI ZA KUFANYA:

i. Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji;
ii. Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka;
iii. Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi;
iv. Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka n.k.) katika mafaili; na
v. Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali.

6. KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III, (NGAZI YA MSHAHARA TGS B, TSH. 151,240.00) - NAFASI 3 (KITUO: DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR)
SIFA ZA MWOMBAJI
i. Awe amehitimu kidato cha nne (IV) na kuhudhuria Mafunzo ya Uhazili na kufaulu mtihani wa Hatua ya Tatu.
ii. Awe amefaulu somo la Hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika moja na awe amepata mafunzo ya Kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na kupata cheti katika programu za Windows, Microsoft Office, Internet, E-mail na Publisher.
SIFA ZA ZIADA
Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani, Kihispania na Kiarabu.
KAZI ZA KUFANYA
i. Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida ;
ii. Kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa ;
iii. Kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadi, wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi, na kumuarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitajika ;
iv. Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi Wizarani ;
v. Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao ;
vi. Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa Maofisa walio katika sehemu alipo, na kukusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika.

MASHARTI KWA WAOMBAJI WOTE :-
1) Maombi yaandikwe kwa mkono na kuambatanishwa nakala zilizohakikiwa za vyeti vya Shule, Vyuo, Vyuo Vikuu (Certificate and transcript) na kozi ulizohudhuria .
2) Wasifu binafsi wa mwombaji (CV) pamoja na picha moja ya pasipoti ya siku za karibuni.
3) Waombaji wote walioajiriwa katika Wizara na Taasisi za Umma maombi yao ya kazi ni lazima yapitie kwa waajiri wao.
4) Waombaji wawe na umri kati ya miaka 18 na 45.
5) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi yote ni Februari 8, 2010.

Maombi yote yatumwe kwa anuani ifuatayo:- Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
S. L. P. 9000
DAR ES SALAAM.
Reply With Quote
  #3  
Old 9th February 2010, 08:51 AM
Mponjoli's Avatar
Mponjoli Mponjoli is offline
Mponjoli Adui wa Maadui wa Taifa
JF Senior Expert Member
Points: 164,050, Level: 100 Points: 164,050, Level: 100 Points: 164,050, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Fri Feb 2008
Posts: 335
Thanks: 57
Thanked 135 Times in 65 Posts
Rep Power: 23
Mponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enoughMponjoli will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

Safi kazi nzuri
__________________
"The important thing is not to stop questioning" - Albert Einstein
Reply With Quote
  #4  
Old 9th February 2010, 09:04 AM
JS's Avatar
JS JS is offline
JS is tired
JF Senior Expert Member
Points: 107,719, Level: 100 Points: 107,719, Level: 100 Points: 107,719, Level: 100
Activity: 20% Activity: 20% Activity: 20%
 
Join Date: Tue Sep 2009
Location: Home/Office/Bar/Saloon!!
Posts: 516
Thanks: 193
Thanked 266 Times in 156 Posts
Rep Power: 22
JS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enoughJS will become famous soon enough
Send a message via Yahoo to JS
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

deadline ilikuwa jana lakini.
Reply With Quote
  #5  
Old 9th February 2010, 09:13 AM
Pape's Avatar
Pape Pape is offline
Pape has no status.
JF Premium Member
Points: 986,888, Level: 100 Points: 986,888, Level: 100 Points: 986,888, Level: 100
Activity: 100% Activity: 100% Activity: 100%
 
Join Date: Thu Dec 2008
Posts: 3,644
Thanks: 253
Thanked 591 Times in 412 Posts
Rep Power: 29
Pape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enoughPape will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

ouch, too late for me! its now 9th feb! so sad!
__________________
A true soldier would rather die than surrender!
Email: pape@jamiiforums.com
Reply With Quote
  #6  
Old 9th February 2010, 01:24 PM
pee-pee pee-pee is offline
pee-pee has no status.
Junior Member
Points: 50,900, Level: 100 Points: 50,900, Level: 100 Points: 50,900, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Thu Jan 2010
Posts: 5
Thanks: 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power: 0
pee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enoughpee-pee will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

thanx mkuu hizi kazi ndo mpaka ujue kihispania, kiarabu kwa kweli wanahitaji ma proffessional
Reply With Quote
  #7  
Old 9th February 2010, 01:37 PM
Maarifa Maarifa is offline
Maarifa senior member
JF Senior Expert Member
Points: 128,903, Level: 100 Points: 128,903, Level: 100 Points: 128,903, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Nov 2006
Location: ULIMWENGU WA MAFISADI
Posts: 272
Thanks: 4
Thanked 6 Times in 3 Posts
Rep Power: 24
Maarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enoughMaarifa will become famous soon enough
Send a message via MSN to Maarifa Send a message via Yahoo to Maarifa
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

Halafu malipo kiduchu au ndo wanakulengesha kwenye manunuzi ya mabilion?? Je kweli are they serious sio kwamba wanataka watu watumbukie kula rushwa? Yaani Master degree ni sifa ya ziada ya kupata sh. Laki TATU kweli kwa mwezi? Oanisha na kazi anazozifanya. Jamani mjionee wasomi wanavyobezwa Tanzania na hata hawana hiana wameoredhesha malugha kibao!!! Kwa laki tatu! Duh Membe upo hapo?
1. AFISA MAMBO YA NJE DARAJA LA II, (NGAZI YA MSHAHARA TGS D, TSH. 322,460.00) - NAFASI 33 (KITUO : DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR)

SIFA ZA MWOMBAJI
i. Awe mwenye Shahada ya Sanaa (B.A.) ambaye amejiimarisha (major) katika fani ya Uhusiano wa Kimaataifa (International Relaions), Sheria au Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

ii. Awe na ujuzi wa kutumia kompyuta.

SIFA ZA ZIADA

i. Awe mwenye uwezo wa kuzungumza lugha za kigeni kama vile Kifaransa, Kireno, Kirusi, Kichina, Kijerumani, Kihispania na Kiarabu.

ii. Mwenye Shahada/Stashahada ya Uzamili (Masters/Postgraduate Diploma) kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapo ya fani zifuatazo:-

a. Uhusiano wa Kimataifa;
b. Public Policy;
c. Uchumi;
d. Biashara ya Kimataifa; na
e. Sheria ya Kimataifa.

KAZI ZA KUFANYA

i. Kuandaa Muhtasari, nakala na taarifa zinazohusu masuala ya mahusiano ya Kimataifa;
ii. Kuhudhuria mikutano mbalimbali;
iii. Kuandaa mahojiano;
iv. Kufuatilia masuala mbalimbali ya kimataifa;
v. Kufanya utafiti juu ya masuala mbalimbali yanayohusu uchumi, siasa na jamii; na
vi. Kutunza kumbukumbu za matukio mbalimbali.
Reply With Quote
  #8  
Old 11th February 2010, 12:58 PM
Ben Ben is offline
Ben The Little Boy among Men
JF Senior Expert Member
Points: 648,728, Level: 100 Points: 648,728, Level: 100 Points: 648,728, Level: 100
Activity: 56% Activity: 56% Activity: 56%
 
Join Date: Thu Jan 2007
Posts: 2,201
Thanks: 254
Thanked 272 Times in 174 Posts
Rep Power: 68
Ben is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the roughBen is a jewel in the rough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

no wonder hatuna policy nzuri foreign affairs
__________________
In Order to conquer them,Let us dare,and keep on daring and dare forever-Che Guevara
Reply With Quote
  #9  
Old 11th February 2010, 01:02 PM
Bwana Mdogo Bwana Mdogo is offline
Bwana Mdogo has no status.
Senior Member
Points: 85,817, Level: 100 Points: 85,817, Level: 100 Points: 85,817, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Wed Jul 2007
Posts: 96
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 23
Bwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enoughBwana Mdogo will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

Walisahau sifa moja muhimu. HAWA NI MTOTO AU NA UHUSIANO WA KARIBU NA KIGOGO SERIKALINI
__________________
Globalization of the local depends on the localization of the global
Reply With Quote
  #10  
Old 11th February 2010, 01:16 PM
Kinyambiss Kinyambiss is online now
Kinyambiss Res Firma Miscetere Nescit
JF Senior Expert Member
Points: 126,915, Level: 100 Points: 126,915, Level: 100 Points: 126,915, Level: 100
Activity: 10% Activity: 10% Activity: 10%
 
Join Date: Sun Dec 2007
Posts: 902
Thanks: 85
Thanked 93 Times in 51 Posts
Rep Power: 27
Kinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enoughKinyambiss will become famous soon enough
Default Re: Kazi Wizara ya Foreign Affairs- Changamkia

Hii mishahara inachekesha kidogo..lol
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
affairs, changamkia, foreign, kazi, wizara


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Baraza Dogo la Mawaziri na Muundo wa Wizara John Mnyika Jukwaa la Siasa 79 19th December 2009 03:47 PM
Serikali ilivyotekeleza Maazimio ya Bunge Richmond-Pinda. Mpaka Kieleweke Jukwaa la Siasa 178 29th August 2008 02:48 PM
Miaka miwili ya JK Ikulu Utendaji wa mawaziri waanikwa Keil Jukwaa la Siasa 3 17th December 2007 10:11 AM
Kikwete afanya mabadiliko baraza la mawaziri The Invincible Jukwaa la Siasa 70 30th August 2007 12:25 AM
Badiliko la baraza la mawaziri Sam Jukwaa la Siasa 2 16th October 2006 01:47 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 04:48 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com