Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Michezo (Sports & Games)


Michezo (Sports & Games) Tujadiliane juu ya yote yanayohusiana na Michezo, Burudani, sanaa n.k


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 20th November 2008, 09:23 AM   #1 (permalink)
Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji
JuaKali JuaKali is online now 20th November 2008, 09:23 AM

Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jana ililipa kisasi baada ya kuifunga Msumbiji `The Mambas` kwa bao 1-0 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja mkuu wa taifa jijini Dar es Salaam.

Stars ilipokea kipigo kama hicho kutoka kwa Msumbiji wakati timu hizo zilipokutana Septemba 8 mwaka jana kwenye uwanja huohuo mkuu wa taifa.

Baada ya kukukuruka kwa dakika 78 ikitafuta bao katika mchezo huo wa jana, Stars hatimaye ilifanikiwa kuona mwezi katika dakika ya 79 baada ya Kigi Makassi kufunga akipokea pasi kutoka kwa Mrisho Ngasa aliyeuwahi mpira uliopigwa na Abdi Kassim.

Dakika 22 Msumbiji ilikosa bao kupitia kwa Alimiro Lobo baada ya krosi safi iliyopigwa na mchezaji mmoja wa timu hiyo na kuokolewa na Godfrey Bonny wa Stars na kumkuta Lobo aliyeshindwa kufunga licha ya kuwa katika nafasi nzuri.

Jerry Tegete dakika sita baadae naye alishindwa kufunga akiwa ndani ya mita 18 baada ya beki wa Msumbiji Antonio Gravata kuuwahi mpira na kuokoa hatari katika lango la Msumbiji.

Idd Moshi Boban nusura aipatie Stars bao katika dakika ya 35 lakini alishindwa kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na Juma Jabu baada ya kupiga shuti dhaifu na kuokolewa na beki wa Msumbiji Guilherme Manhique.

Msumbiji ilifanya shambulio jingine la nguvu katika dakika ya 44 lakini Antonio Gravata alishindwa kuifungia bao baada ya kupaisha mpira juu ya goli akiunganisha vibaya krosi ya Ticotico.

Stars kupitia kwa beki wake Shadrack Nsajigwa nusura ifunge baada ya mchezaji huyo kupanda na kupiga shuti kali lakini kipa wa Msumbuji Marcelino Cumbane alifanya kazi nzuri kuokoa mpira huo kabla haujatinga wavuni.

Kocha wa Stars, Marcio Maximo alisema baada ya mchezo huo, kuwa mchezo ulikuwa mgumu kama alivyotarajia na Msumbiji walicheza vizuri licha ya kufungwa kwani walipata nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia.

Alisema kuwa ushndi huo utawaongezea ari wachezaji wake kwa ajili ya pambano lijalo dhidi ya Sudan litakalofanyika Novemba 29 jijini Dar es Salaam kusaka kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka katika ligi za nyumbani tu.

Naye kocha wa Msumbiji, Mooij Martinus alisema kuwa ushindi huo ni zawadi tosha ya Krismas kwa Stars pia aliweapongeza wapinzani wao kwa ushindi huo, ambapo alisisitiza kuwa kwa sasa timu yake inajifua kwa ajili ya hatua ya pili ya kufuzu kwa mashindano ya Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia.

Timu zilikuwa; Taifa Stars: Shabaan Dihile, Shadrack Nsajigwa, Juma Jabu, Nadir Haroub `Cannavaro`, Salum Sued, Godfrey Bonny, Mrisho Ngassa/Mussa Hassan Mgosi (dk.89), Henry Joseph/Nurdin Bakari (dk.74), Jerry Tegete/Nizar Khalfan (dk. 59), Haruna Moshi `Boban`/Abdi Kassim (dk.71) na Athumani Iddi `Chuji\'/Kigi Makassi (dk.63).

Msumbiji: Marcelino Cumbane, Antonio Gravata, Gonclaves Fumo/Momed Hagi (dk. 59), Elias Pelembe, Manuel Bucuane, Dario Monteiro/Lus Muchue (dk.55), Guilherme Manhique/Nasser Carimo (dk.77), Carlos Parruque/Carlos Chimomole (dk.89), Francisco Massinga, Alimiro Lobo na Fanuel Massingue

 
JuaKali's Avatar
JuaKali
Senior Member
Join Date: Wed Nov 2007
Location: USA
Posts: 141
Thanks: 38
Thanked 41 Times in 30 Posts
Views: 249
Reply With Quote
  #2 (permalink)  
Old 20th November 2008, 11:30 AM
Roya Roy's Avatar
Roya Roy always on the feet
JF Premium Member
 
Join Date: Sat Mar 2007
Location: On Earth
Posts: 667
Thanks: 287
Thanked 299 Times in 193 Posts
Rep Power: 24
Roya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud ofRoya Roy has much to be proud of
Credits: 1,381,601
Default Re: Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji

Kwa sababu hawa Nyoka weusi walitukandamiza kwenye mechi ya kimashindano na kutuharibia safari (kama ilikuwepo) yetu ya kwenda Bondeni 2010 (na Angola), basi hatuwezi kusema tumelipiza kwa kuwafunga kwenye mechi ya kirafiki.
Tusubiri tukutane nao kwenye mechi ya kimashindano.
BTW: Viva Stars kwa ushindi, yaweza kutusaidia kupanda kidogo (labda hadi kwenye top 100) kwenye chati ya FIFA.
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Roya Roy For This Useful Post:
Next Level (20th November 2008)
  #3 (permalink)  
Old 20th November 2008, 12:55 PM
Next Level's Avatar
Next Level is optimistic one day yes
JF Premium Member
 
Join Date: Mon Nov 2008
Location: Pwani
Posts: 1,139
Thanks: 465
Thanked 576 Times in 341 Posts
Rep Power: 23
Next Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud of
Credits: 2,691,903
Default Re: Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji

Quote:
View Post
Kwa sababu hawa Nyoka weusi walitukandamiza kwenye mechi ya kimashindano na kutuharibia safari (kama ilikuwepo) yetu ya kwenda Bondeni 2010 (na Angola), basi hatuwezi kusema tumelipiza kwa kuwafunga kwenye mechi ya kirafiki.
Tusubiri tukutane nao kwenye mechi ya kimashindano.
BTW: Viva Stars kwa ushindi, yaweza kutusaidia kupanda kidogo (labda hadi kwenye top 100) kwenye chati ya FIFA.
Bora umeliona hilo......jana hatatungeshida bao kumi na moja, ilikuwa si venue ya kulipiza kisasi, ilikuwa ni mechi ya kirafiki kwaajili ya kujipima nguvu tu!

Stars wakitaka kulipiza kisasi wasubiri mashindano ya kufuzu tena world cup...hope itakuwa Brazil 2014, ndipo tulipize kisasi au hata mshindano ya kufuzu Kombe la Africa ...sio mchezo wa kirafiki!

Tufungue macho na ubongo jamani ...eeeh!
__________________
CHANGIA JF: MKONO MTUPU HAULAMBWI- SIKONGE
Reply With Quote
  #4 (permalink)  
Old 20th November 2008, 03:52 PM
africa6666 always cool
Senior Member
 
Join Date: Mon Aug 2008
Location: dar es salaam
Posts: 56
Thanks: 20
Thanked 21 Times in 13 Posts
Rep Power: 21
africa6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud ofafrica6666 has much to be proud of
Credits: 71,635
Send a message via Yahoo to africa6666
Default Re: Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji

Kwa records za FIFA, wanahesabu mchezo wowote wa kimataifa kuwa ni sawa friend match or otherwise, ndio maana ktk mechi kama za jana ambazo zimechezwa kote barani africa, FIFA wanazitumia kutathmini ubora wa timu husika.
Please don't comment some thing you are not sure of.
Ile ni mechi muhimu sana mbali na kulipiza kisasi pia inatusaidia fifa kwa records
__________________
Hata Mbuyu ulianza kama Mchicha
Reply With Quote
  #5 (permalink)  
Old 20th November 2008, 04:19 PM
Next Level's Avatar
Next Level is optimistic one day yes
JF Premium Member
 
Join Date: Mon Nov 2008
Location: Pwani
Posts: 1,139
Thanks: 465
Thanked 576 Times in 341 Posts
Rep Power: 23
Next Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud ofNext Level has much to be proud of
Credits: 2,691,903
Default Re: Stars yalipa kisasi kwa Msumbiji

Quote:
View Post
Kwa records za FIFA, wanahesabu mchezo wowote wa kimataifa kuwa ni sawa friend match or otherwise, ndio maana ktk mechi kama za jana ambazo zimechezwa kote barani africa, FIFA wanazitumia kutathmini ubora wa timu husika.
Please don't comment some thing you are not sure of.
Ile ni mechi muhimu sana mbali na kulipiza kisasi pia inatusaidia fifa kwa records
Mkuu sijakuelewa vyema hapa, ubora gani unaosema hapa kwa stars ambayo perfomance yake iko very inconsistence hivyo? jana mko nafasi ya 90, leo 102 keshokutwa 104 for what? Tunacho comment hapa, ni kusherekea kuifunga Black Mambas kwenye friendly mechi halafu unasema umelipiza kisasi! Kwanza kikosi kilicho ifunga stars last year sidhani ndo hicho kilicheza jana, pili sidhani split ya timu yao ya jana sidhani inafanana na ile ilioyotufunga kwenye qualifying match!

Therefore unavyozungumzia kulipiza kisasi mimi sikubali ukiwa unazungumzia mchezo wa jana, cause malengo ya michezo hiyo miwili ilikuwa tofauti kabisa!
__________________
CHANGIA JF: MKONO MTUPU HAULAMBWI- SIKONGE
Reply With Quote
Reply

Bookmarks


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Bado tunamkumbuka carlos cardoso Mtambuzi Habari/Hoja mchanganyiko 0 30th October 2008 07:37 AM
Dhana ya kulipa kisasi Shy Mahusiano, mapenzi, urafiki 0 24th October 2008 04:18 PM
Kashfa ya Richmond: The FACTS FairPlayer Celebrities Forum 1352 16th August 2008 12:06 PM
Taifa Stars, Msumbiji waingiza Sh605milioni Bubu Ataka Kusema Michezo (Sports & Games) 1 12th September 2007 09:05 PM
Baada ya kipigo Taifa Stars, mashabiki wamgeukia Maximo Bubu Ataka Kusema Michezo (Sports & Games) 2 9th September 2007 10:44 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 02:04 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com

no new posts