Showing Visitor Messages 1 to 2 of 2
-
20th August 2009 11:21 AM
IBRA
inakuaj mtu mzima
-
11th October 2008 04:22 PM
Mkora
bandari salama hatarini kukosa tenda
Na Irene Bwire, Nambia
BANDARI ya Dar es Salaam iko hatarini kupoteza wateja wa nchi zisizo na bandari kama haitamaliza tatizo la msongamano wa mizigo bandarini.
Hayo yamebainika jana wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipotembelea Mamlaka ya Bandari Namibia (NAMPORT) katika bandari ya Walvis Bay iliyopo Namibia na kuelezwa mpango wa bandari hiyo kuhudumia nchi zote za SADC ifikapo mwaka 2015.
Meneja Mauzo wa bandari hiyo, Bw. Elias Mwenyo alimweleza Waziri Mkuu kwamba mamlaka hiyo ya bandari iliyoanzishwa mwaka 1994 imepata hadhi ya kimataifa na kuweza kutoa huduma kwa nchi za Amerika Kusini, Amerika Kaskazini, Afrika Magharibi, Ulaya na Asia.
Alisema mwanzoni bandari hiyo ilikuwa ni uchochoro tu wa kuupitisha bidhaa lakini sasa inahudumia nchi za Zambia, Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Botswana, na Zimbabwe ambazo hazina bandari.
“Urahisi wa mawasiliano ya barabara, reli na ndege kwenda nchi za SADC umetuwezesha kuhudumia nchi hizo tunakatisha jangwa la Kalahari badala ya kwenda Durban au Capetown, Afrika Kusini na hivyo kuokoa siku saba hadi 11 za mizigo kukaa njiani,” alisema.
Alipoulizwa na Waziri Mkuu Pinda ni muda gani meli zinatumia kukaa majini tangu zinapofika hadi kutia nanga bandarini hapo, Bw. Mwenyo alisema hakuna meli zinazokawizwa kwa sababu wanapopewa notisi ya saa 72 kabla meli haijafika maeneo ya kwao wanaanza maandalizi ya kuipokea na hivyo kuwa tayari kuzihudumia pindi tu zinapofika.
Alisema bandari hiyo ambayo haijawahi kupoteza mzigo hata mmoja ina uwezo wa kuhudumia tani milioni nne za mizigo kwa mwaka na uwezo wa kupokea meli za mizigo 350 kwa mwezi. Pia ina vitengo vya kukarabati meli zinapoharibika tofauti na zamani zilipokuwa zikilazimika kupelekwa Cape Town, Afrika Kusini.
Taarifa hizi zimekuja wakati Rais Jakaya Kikwete amemwagiza Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa ampe jibu la siku kamili za mtu kusubiri mzigo bandarini na kumtaka apunguze siku hizo kutoka siku 23 za sasa hadi 10.
Taarifa ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ambayo alisomewa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga Septemba 24, mwaka huu, inasema bandari za mwambao ambazo ni Dar es Salaam, Tanga na Mtwara zina uwezo wa kuhudumia tani milioni 11 kwa mwaka lakini katika mwaka 2007/8 ziliweza kuhudumia tani milioni 6.2 ambayo ni sawa na asilimia 58 ya uwezo wa bandari.
“Shehena ya kontena katika kipindi hiki ilikuwa makontena 325,000 ambayo ni asilimia 30 juu ya uwezo wa kitengo [WINDOWS-1252?]hicho,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Waziri Mkuu kesho (Ijumaa) atakutana na Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia na baadaye kutembelea mradi wa maji wa Goreangab ulioko eneo la Katutura na mchana anatajiwa kuondoka Namibia kurejea nchini.