Nimemuona Mpoto nae kama kawaida yake akitoa salamu,akadai pamoja na kuwa yeye huwa anakuwa kwenye shughuli za watu mashuhuri sana leo yupo hapo kusherehekea, nimemuona kanyoa nyusi, sijui imekuwaje mwanaume kunyoa nyusi!
Huyu aliwahi kumwambia rafiki yangu mlokole mjanja ambaye ana nyumba za kupangisha 15 maeneo mbalimbali ya jiji ya Dar Es Salaam, kuwa ha yaani nyumba 15 nawe unasema una nyumba hapa jijini, yaani unatakiwa angalau una nyumba kuanzia 30 na kuendelea bwashee, maneno hayo anamwambia hapo kanisani...
Kweli kabisa siku hizi hela ipo Instagram, ndio maana tunawaona machawa kama akina Mwijaku,Doto Magari ,Haji Domo, Konde na wajinga wajinga wengi wakiwa mamilionea kwa kuwa wajinga na wengine kwa kuonyesha misambwanda huko Instagram.
Huyu mleta uzi kashindwa tu kueleza kule Kenya mkuu wa majeshi huwa anateuliwa kwa kuzunguka kutoka kwenye majeshi makuu matatu lakini yote ya ulinzi ,kuna jeshi la wanamaji, kuna jeshi la nchi kavu na kuna jeshi la anga,sasa kwa utaratibu wao kila jeshi hupewa zamu ya kutoa kamanda mkuu wa...
Ndio maana niliondoka jiji la Chalamila hapo wote ni wahuni si hao wazee wala vijana wanaoshangilia upumbavu, mtu ukifika kuitwa mzee inabidi urudi kwenu kijijini kusikia matusi ukiwa na wajukuu ni laana, wazee wa jiji wengi wanakosa staha, ndio hao utawasikia wazuri hawafi,tunalamba asali.
Badala tu ya kukanusha na kusema mtalii ni mjinga nadhani ingekuwa jambo zuri ungetupatia majibu ya yale aliyoyasema, kwa mfano ungetuambia si kweli kwamba intaneti TZ ni sawa na mwendo wa konokono na huku vifurushi vikiwa bei juu,je si kweli kwamba lugha ya mawasiliano na wenzetu wa nje sisi ni...
Mawakala wa utalii kule Zanzibar wanatuhujumu Watanganyika, ratiba ya watalii wakifika Zanzibar huwaweka na kutembelea mbuga za bara, lakini hufanya watalii wasilale bara kwani ndege ambazo huleta watalii huku bara huwa zinaleta watalii asubuhi na kurudi nao jioni, huu upuzi unakosesha mapato...
Sijawahi kusikia bunge la Kenya lilisema tunamshukuru Mheshimiwa Ruto kwa kutupa pesa ya kujenga shule, au Ruto akitajwa kwa jina lake pale mambo ya maendeleo yanapozungumzwa kwenye vikao na halaiki mbalimbali za maendeleo kutoka kwa wabunge au maseneta au wakuu wa majimbo na hata madiwani, huu...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.