Recent content by Kubota

  1. Kubota

    Kwanini wengi huishia kupata hasara kwenye kilimo?

    Mleta mada asante sana kwa kuwekea msisitizo vipengele hivyo vinavyoangusha wengi. Kilimo ni shughuri ya kiuchumi kama biashara nyingine. Kwa anaetaka kufanya kwa tija lazima kujifunza mbinu za ujasilia mali nyingi iwezekanavyo. Mbinu hizo zitamsaidia kujua nini cha kulima, wapi soko, iwapo...
  2. Kubota

    Msaada: Naitaji kulima mpunga (saro), naitaji mawazo yenu

    Laki saba inatosha kwa eka moja tu. Usiwaze eka mbili hasa kama watarajia kupanda kitaalamu labda kama ni wa kurusharusha mbegu unaishia kuvuna gunia saba kwa eka
  3. Kubota

    Kubota yupo wapi??

    Wakuu majira kama haya mwaka jana nilinyanyasika kuuza nyanya debe kwa buku....mwaka huu majira haya mm roho ya ppaka niliyestahimili kurudia kulima nyanya majira haya haya hatarishi nakamua bei ya 15,000 debe!! Wadau hivi kumetokea nn!! nchini? Hali hii itafuatwa na mafuriko ya nyanya Sept -...
  4. Kubota

    Natafuta Pampu ya umwagiliaji

    Kuna mambo mengine mengi ya kuzingatia unaponunua pump. Aina ya umwagiaji Wamwagiliaji mjini Morogoro humwagia kwa kuifuata mimea na kutembea na mpira shamba zima kila mmea ukimwagiwa maji peke yake. Kwa umwagiaji wa aina hii wakulima hutumia pump ndogo za inchi 2. Saizi ya pump hizi ni nzuri...
  5. Kubota

    NATAFUTA SOKO LA VITUNGUU

    Kwa mwezi wa saba naamini utapata bei nzuri hata Hapo MBUYUNI. Kwani umeona dalili ya kuwepo mafuriko ya vitunguu utakapokuwa unavuna ww?
  6. Kubota

    Picha nne ambazo ningependa Mh. Rais azione!

    Kuhusu hizo picha za Google earth, si sahihi kutumia picha hizo kama uthibitisho wa hali ya uoto uliopo muda huu. Google earth huwa updated baada ya muda mrefu kupita kwaio yawezekana zikawa picha za zamani na zisiwasilishe hali ilivyo leo.
  7. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Ekari moja kama ni ufugaji huria unapaswa kuweka kuku wa kubwa 400 unahitaji ekari mbili na nusu kama lengo lako ni kufuga kuku 1000
  8. Kubota

    Kubota yupo wapi??

    Asante wakuu kwa juhudi za kunitafuta. Nashukuru na nafarijika sana ninapodhihirishiwa kuwa michango yangu JF inasaidia jamii. Mimi nipo sana jukwaani, nimekuwa mzito kuchangia jukwaani kutokana na kujichimbia sana kwenye dili langu la huko maporini kuchoma mkaa maana maeneo yetu hayo ya...
  9. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Mkuu Soya beans sio maharage ni zao tofauti kabisa ingawa liko jamii moja sawa na maharage, mbaazi na kunde. Soya beans ni maarufu kwa kusheheni protein kuliko mazao mengine jamii ya mikunde. Kwenye kutengeneza vyakula vya kuku source rahisi ya protein huwa ni dagaa. Wataalamu siku hizi badala...
  10. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Sijawahi kufanya huo utafiti maana huwa nanunua starter mash mfuko mmoja tu kuwalisha kuku mia moja kwa mwezi wa kwanza na kisha hununua growers mash mifuko miwili na huwalisha hao kuku mia kwa mwezi mwingine, baada ya hapo kuku huwa wakubwa huwaachia wakapekue na pia huwatengenezea cha ziada...
  11. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Asante sana kwa maneno yako yanayotia moyo. Kuna wachangiaji walinilalamikia niachane na kuchoma mkaa kutokana na athari zake kwenye mazingira. Kwakuwa nilishajua utamu wa biashara ya mkaa niliamua kutengeneza mkaa kwa kutumia mabua ya mpunga na mabua ya mahindi, kama hujui ingia You Tube Kuna...
  12. Kubota

    Magufuli, watanzania wana shida zaidi ya hapo!

    Unachonga sifa za madikteta kufit agenda yako ya kumchafua mkombozi wa wanyonge, mtatoka mapovu sana mimi ninachojua unawakilisha majizi, mafisadi na wanufaikaji wa mfumo unaoenda kufumuliwa. Na mtatumbuliwa tu hata mseme vipi! Maandishi yako yanaonesha unafanya hapa mahali pa kujifunzia kujenga...
  13. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Mlioko mashambani limeni sana zao la mikunde aina ya soya (soya beans) haya yanaondoa kabisa haja ya kutumia dagaa kwenye utengenezaji wa chakula cha kuku, kinachotakiwa ni kununua amino acid aina mbili ambazo zinakosekana kwenye soya bean lakini zinapatikana kwenye maduka ya kilimo. Ukilima...
  14. Kubota

    Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Masoko yake

    Asante sana Mkuu kwa mrejesho wako ! Ukweli asilimia 95 kufikia mafanikio ni juhudi na maarifa, asilimia 5 tu ndiyo bahati ! Tuko pamoja sana.
Back
Top Bottom