Go Back   JamiiForums.com > Public Forums > Matangazo madogomadogo

Reply
 
LinkBack Thread Tools Display Modes
  #1 (permalink)  
Old 19th November 2008, 09:23 PM
JF Senior Expert Member
 
Join Date: Thu Nov 2006
Location: Tulsa, Oklahoma/MFA-TZ
Posts: 757
Rep Power: 24
Mwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud of
Thanks: 582
Thanked 673 Times in 267 Posts
Credits: 31,545
Default Mike sikawa afariki dunia

Mwandishi wa Habari wa siku nyingi Mike Sikawa (55) amefariki Dunia,Nyumbani kwake Njiro - Arusha siku ya Jumatatu (17.11.2008).Marehemu Sikawa amefarikiki baada ya kusumbuliwa na Ugonjwa wa Kisukari kwa muda mrefu.

Katika uhai wake amewahi kufanya kazi Katika kampuni ya magazeti ya serikali (TSN),Pia amewahi kuwa Mtangazaji wa BBC Idhaa ya Kiswahili huko Johannesburg - Afrika kusini.Marehemu ameacha mke na watoto wawili.(wanaishi South Afrika).Mazishi ya marehemu yatakuwa kwao Arumeru Arusha...Mwenyezi Mungu amlaze mahali Pema Peponi!!
__________________
Its not enough to do good if you can do better.
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Mwawado For This Useful Post:
SteveD (20th November 2008)


  #2 (permalink)  
Old 19th November 2008, 09:26 PM
Shy's Avatar
Shy Shy is offline
JF Senior Expert Member
 
Join Date: Thu Nov 2006
Posts: 2,664
Rep Power: 28
Shy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud ofShy has much to be proud of
Thanks: 3
Thanked 771 Times in 496 Posts
Credits: 75,983
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

hata katika magazeti sijaona watu hawatilii mkazo lakini poleni wahusika wa msiba huu , sijui jk akitoka huko alipo ataenda katika msiba ngoja tuone
__________________
Don't assume anything. Take the time to brush up your knowledge because the computer world is always changing , The problem isn't your problems, it's your ridiculous solutions.
Reply With Quote
  #3 (permalink)  
Old 19th November 2008, 09:31 PM
JF Senior Expert Member
 
Join Date: Thu Nov 2006
Location: Tulsa, Oklahoma/MFA-TZ
Posts: 757
Rep Power: 24
Mwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud ofMwawado has much to be proud of
Thanks: 582
Thanked 673 Times in 267 Posts
Credits: 31,545
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Shy !,Tumeipeleka habari hii kwenye magazeti...itaonekana kama ilivyo chini
Mike Sikawa wa BBC afariki dunia

MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari.

Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha.

Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni.
Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote.

Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia.
Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti.

Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro.

Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini.

Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi.

Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo.

Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.
__________________
Its not enough to do good if you can do better.
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Mwawado For This Useful Post:
Mzee Mwanakijiji (19th November 2008)
  #4 (permalink)  
Old 19th November 2008, 10:07 PM
Mzee Mwanakijiji's Avatar
JF Senior & Premium Member
 
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 12,987
Rep Power: 51
Mzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud ofMzee Mwanakijiji has much to be proud of
Thanks: 7,173
Thanked 9,916 Times in 3,688 Posts
Credits: 746,363
Send a message via MSN to Mzee Mwanakijiji Send a message via Skype™ to Mzee Mwanakijiji
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Poleni na msiba wafiwa wote, Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi. Amina.
__________________
Ukipewa uchaguzi na adui yako, chagua kile wanachohofia! - M.M. Original
Kijarida cha "Cheche za Fikra" kimetoka!
Jipatie nakala yako hapa
Reply With Quote
  #5 (permalink)  
Old 19th November 2008, 10:07 PM
Mama's Avatar
Senior Member
 
Join Date: Mon Mar 2008
Location: on planet earth
Posts: 2,535
Rep Power: 4026
Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!
Thanks: 1,409
Thanked 1,572 Times in 946 Posts
Credits: 317,585
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Rest in peace Mike.
Reply With Quote
  #6 (permalink)  
Old 19th November 2008, 10:11 PM
Ushirombo's Avatar
JF Senior & Premium Member
 
Join Date: Tue Oct 2007
Location: Lahore
Posts: 869
Rep Power: 63
Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!Ushirombo is one of most respected JF members!
Thanks: 203
Thanked 517 Times in 285 Posts
Credits: 55,590
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mungu amrehemu Mike Sikawa na pole wafiwa wote
__________________
""Without knowledge, there is no freedom." — Anon."
Reply With Quote
  #7 (permalink)  
Old 19th November 2008, 10:17 PM
Ladslaus Modest's Avatar
JF Senior Expert Member
 
Join Date: Fri Jun 2008
Location: Arusha Tanzania
Posts: 417
Rep Power: 21
Ladslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud ofLadslaus Modest has much to be proud of
Thanks: 552
Thanked 177 Times in 124 Posts
Credits: 16,567
Send a message via Yahoo to Ladslaus Modest Send a message via Skype™ to Ladslaus Modest
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi aliyemuumba Mike Sikawa, hatimaye amemrudisha kwake.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana libarikiwe. Amen.

Poleni wafiwa wote, Mwenyezi Mungu awape nguvu na uvumilivu wakati huu mgumu wa majonzi.
__________________
Wa-Tanzania tupendane, tushirikiane, tuijenge nchi yetu.
Reply With Quote
  #8 (permalink)  
Old 19th November 2008, 10:47 PM
JF Senior & Premium Member
 
Join Date: Fri May 2006
Posts: 2,472
Rep Power: 27
Jasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud ofJasusi has much to be proud of
Thanks: 3,051
Thanked 1,478 Times in 703 Posts
Credits: 136,422
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mwawado,
Nimeipokea habari hii kwa masikitiko makubwa. Nilimfahamu Mike Sikawa kwa muda mrefu. Katika ziara yake hapa Marekani alinipigia simu akiwa ubalozini na nikamchukua nyumbani kwangu. KInachonisikitisha ni kwamba he died too young. 55 is a very young age, lakini mapenzi ya mwenyezi Mungu hayana makosa. I will miss him and may his family find refuge in the fact that he was loved by many.
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Jasusi For This Useful Post:
Mwawado (19th November 2008)
  #9 (permalink)  
Old 19th November 2008, 11:26 PM
JF Senior Expert Member
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 2,482
Rep Power: 4027
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Thanks: 541
Thanked 799 Times in 544 Posts
Credits: 82,858
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

RIP Mike Sikawa
__________________
Save Water Drink Beer "Beer helping ugly people to have sex..."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
  #10 (permalink)  
Old 20th November 2008, 12:33 AM
Mwazange's Avatar
JF Senior & Premium Member
 
Join Date: Fri Nov 2007
Location: Nyanda za Juu Kusini
Posts: 353
Rep Power: 22
Mwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud ofMwazange has much to be proud of
Thanks: 56
Thanked 138 Times in 96 Posts
Credits: 61,537
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Ilikuwa inatia raha sana kusikiliza BBC. RIP brother.....
__________________
Wise men talk because they have something to say; fools talk because they have to say something.....
Reply With Quote
The Following User Says Thank You to Mwazange For This Useful Post:
Jasusi (20th November 2008)
Reply

Bookmarks


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are On
Pingbacks are On
Refbacks are On

Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Ngozoma Matunda afariki dunia Bubu Ataka Kusema Michezo (Sports & Games) 9 20th November 2008 03:58 PM
Hadithi - shujaa wa mashariki Shy Jukwaa la Lugha 2 3rd October 2008 01:04 PM
Ofisa ubalozini Nigeria afariki dunia Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 2 3rd July 2008 07:47 AM
Dunia Adonis afariki dunia Bubu Ataka Kusema Michezo (Sports & Games) 2 13th November 2007 01:55 AM
Sheikh NURDIN HUSSEIN AL-SHADILY afariki dunia samvulachole Jukwaa la Siasa 25 27th August 2007 11:46 AM


All times are GMT +3. The time now is 12:26 PM.



Copyright JamiiForums.com