Mike sikawa afariki dunia - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Matangazo madogomadogo


Matangazo madogomadogo Matangazo ya misiba, mikutano n.k yawekwe hapa. ONYO: Usiweke links za aina yoyote! Uongozi wa JF hautahusika kwa namna yoyote kwa mawasiliano ya mauzo yaliyowekwa na wanachama bila kutushirikisha.


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 19th November 2008, 08:23 PM   #1
Mike sikawa afariki dunia
Mwawado Mwawado is offline 19th November 2008, 08:23 PM

Mwandishi wa Habari wa siku nyingi Mike Sikawa (55) amefariki Dunia,Nyumbani kwake Njiro - Arusha siku ya Jumatatu (17.11.2008).Marehemu Sikawa amefarikiki baada ya kusumbuliwa na Ugonjwa wa Kisukari kwa muda mrefu.

Katika uhai wake amewahi kufanya kazi Katika kampuni ya magazeti ya serikali (TSN),Pia amewahi kuwa Mtangazaji wa BBC Idhaa ya Kiswahili huko Johannesburg - Afrika kusini.Marehemu ameacha mke na watoto wawili.(wanaishi South Afrika).Mazishi ya marehemu yatakuwa kwao Arumeru Arusha...Mwenyezi Mungu amlaze mahali Pema Peponi!!
__________________
Its not enough to do good if you can do better.

 
Mwawado's Avatar
Mwawado
JF Senior Expert Member
Points: 219,786, Level: 100 Points: 219,786, Level: 100 Points: 219,786, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Thu Nov 2006
Location: Tulsa, Oklahoma/MFA-TZ
Posts: 1,075
Thanks: 51
Thanked 73 Times in 33 Posts
Views: 1276
Reply With Quote
  #2  
Old 19th November 2008, 08:26 PM
Shy's Avatar
Shy Shy is offline
Shy is yours
JF Senior Expert Member
Points: 2,372,423, Level: 100 Points: 2,372,423, Level: 100 Points: 2,372,423, Level: 100
Activity: 12% Activity: 12% Activity: 12%
 
Join Date: Thu Nov 2006
Posts: 4,256
Thanks: 0
Thanked 165 Times in 110 Posts
Rep Power: 32
Shy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enoughShy will become famous soon enough
Send a message via Yahoo to Shy
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

hata katika magazeti sijaona watu hawatilii mkazo lakini poleni wahusika wa msiba huu , sijui jk akitoka huko alipo ataenda katika msiba ngoja tuone
__________________
I.T. Specialist and Digital Security Consultant
Reply With Quote
  #3  
Old 19th November 2008, 08:31 PM
Mwawado's Avatar
Mwawado Mwawado is offline
Mwawado Mossad Sensei
JF Senior Expert Member
Points: 219,786, Level: 100 Points: 219,786, Level: 100 Points: 219,786, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Nov 2006
Location: Tulsa, Oklahoma/MFA-TZ
Posts: 1,075
Thanks: 51
Thanked 73 Times in 33 Posts
Rep Power: 26
Mwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enoughMwawado will become famous soon enough
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Shy !,Tumeipeleka habari hii kwenye magazeti...itaonekana kama ilivyo chini
Mike Sikawa wa BBC afariki dunia

MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari.

Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha.

Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni.
Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote.

Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia.
Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti.

Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro.

Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini.

Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi.

Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo.

Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.
__________________
Its not enough to do good if you can do better.
Reply With Quote
  #4  
Old 19th November 2008, 09:07 PM
Mzee Mwanakijiji's Avatar
Mzee Mwanakijiji Mzee Mwanakijiji is online now
Mzee Mwanakijiji anawashangaa wanaoitetea sheria mbovu
JF Premium Member
Points: 12,846,095, Level: 100 Points: 12,846,095, Level: 100 Points: 12,846,095, Level: 100
Activity: 97% Activity: 97% Activity: 97%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Location: Kijijini
Posts: 18,323
Thanks: 8,086
Thanked 4,377 Times in 1,226 Posts
Rep Power: 44
Mzee Mwanakijiji is on a distinguished roadMzee Mwanakijiji is on a distinguished road
Send a message via MSN to Mzee Mwanakijiji Send a message via Skype™ to Mzee Mwanakijiji
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Poleni na msiba wafiwa wote, Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi. Amina.
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Reply With Quote
  #5  
Old 19th November 2008, 09:07 PM
Mama Mama is offline
Mama has no status.
JF Premium Member
Points: 10,194,467, Level: 100 Points: 10,194,467, Level: 100 Points: 10,194,467, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Mar 2008
Posts: 2,897
Thanks: 0
Thanked 7 Times in 7 Posts
Rep Power: 4027
Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!Mama is one of most respected JF members!
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Rest in peace Mike.
__________________

Reply With Quote
  #6  
Old 19th November 2008, 09:11 PM
Masanilo's Avatar
Masanilo Masanilo is offline
Masanilo is back the to alcohol Rehab centre
JF Premium Member
Points: 822,641, Level: 100 Points: 822,641, Level: 100 Points: 822,641, Level: 100
Activity: 70% Activity: 70% Activity: 70%
 
Join Date: Tue Oct 2007
Location: Swat valley
Posts: 7,006
Thanks: 1,020
Thanked 1,083 Times in 704 Posts
Rep Power: 77
Masanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the roughMasanilo is a jewel in the rough
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mungu amrehemu Mike Sikawa na pole wafiwa wote
__________________
To be able to do everything by knowing nothing is dangerous

E-mail:
masanilo@jamiiforums.com
Reply With Quote
  #7  
Old 19th November 2008, 09:17 PM
Ladslaus Modest's Avatar
Ladslaus Modest Ladslaus Modest is offline
Ladslaus Modest is a Mchungaji (Shepherd)
JF Premium Member
Points: 136,737, Level: 100 Points: 136,737, Level: 100 Points: 136,737, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Jun 2008
Location: Nachunga Kondoo
Posts: 574
Thanks: 20
Thanked 43 Times in 24 Posts
Rep Power: 23
Ladslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enoughLadslaus Modest will become famous soon enough
Send a message via Yahoo to Ladslaus Modest Send a message via Skype™ to Ladslaus Modest
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi aliyemuumba Mike Sikawa, hatimaye amemrudisha kwake.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana libarikiwe. Amen.

Poleni wafiwa wote, Mwenyezi Mungu awape nguvu na uvumilivu wakati huu mgumu wa majonzi.
__________________
Wa-Tanzania tupendane, tushirikiane, tuijenge nchi yetu.
Reply With Quote
  #8  
Old 19th November 2008, 09:47 PM
Jasusi Jasusi is offline
Jasusi is a truth seeker
JF Premium Member
Points: 277,411, Level: 100 Points: 277,411, Level: 100 Points: 277,411, Level: 100
Activity: 23% Activity: 23% Activity: 23%
 
Join Date: Fri May 2006
Posts: 4,143
Thanks: 1,081
Thanked 559 Times in 289 Posts
Rep Power: 32
Jasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enough
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Mwawado,
Nimeipokea habari hii kwa masikitiko makubwa. Nilimfahamu Mike Sikawa kwa muda mrefu. Katika ziara yake hapa Marekani alinipigia simu akiwa ubalozini na nikamchukua nyumbani kwangu. KInachonisikitisha ni kwamba he died too young. 55 is a very young age, lakini mapenzi ya mwenyezi Mungu hayana makosa. I will miss him and may his family find refuge in the fact that he was loved by many.
Reply With Quote
  #9  
Old 19th November 2008, 10:26 PM
Kibunango's Avatar
Kibunango Kibunango is offline
Kibunango Mapinduzi Daima...! CCM Damu.
JF Senior Expert Member
Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100 Points: 10,820,469, Level: 100
Activity: 39% Activity: 39% Activity: 39%
 
Join Date: Tue Aug 2006
Location: Tampere
Posts: 4,870
Thanks: 351
Thanked 207 Times in 169 Posts
Rep Power: 4033
Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!Kibunango is one of most respected JF members!
Send a message via MSN to Kibunango Send a message via Yahoo to Kibunango
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

RIP Mike Sikawa
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk."
Vituko Vya Zenj
Reply With Quote
  #10  
Old 19th November 2008, 11:33 PM
Mwazange's Avatar
Mwazange Mwazange is offline
Mwazange Mtu Poa
JF Premium Member
Points: 133,366, Level: 100 Points: 133,366, Level: 100 Points: 133,366, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Nov 2007
Location: Nyanda za Juu Kusini
Posts: 805
Thanks: 0
Thanked 31 Times in 23 Posts
Rep Power: 24
Mwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enoughMwazange will become famous soon enough
Default Re: Mike sikawa afariki dunia

Ilikuwa inatia raha sana kusikiliza BBC. RIP brother.....
__________________
A positive attitude may not solve all your problems,but it will annoy enough people to make it worthwhile......
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
afariki, dunia, mike, sikawa


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Felix Makene Afariki Dunia! Morani75 Habari na Hoja mchanganyiko 69 29th January 2008 12:50 PM
Dunia Adonis afariki dunia Bubu Ataka Kusema Sports & Entertainment Forum 2 13th November 2007 12:55 AM
Sheikh NURDIN HUSSEIN AL-SHADILY afariki dunia Samvulachole Jukwaa la Siasa 25 27th August 2007 11:46 AM
Chifu Fundikira Afariki Dunia Saidi Yakubu Celebrities Forum 45 14th August 2007 08:23 AM
Dunia Salama shy Habari na Hoja mchanganyiko 1 12th October 2006 06:46 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 06:35 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com