| Find/Invite Friends | Register | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| FAQ | Members List | Bongo Flava | Zilipendwa | Taarab | Injili |
|
|
#1 | |||||||||||
|
||||||||||||
|
Views: 1276
|
||||||||||||
|
#2
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
hata katika magazeti sijaona watu hawatilii mkazo lakini poleni wahusika wa msiba huu , sijui jk akitoka huko alipo ataenda katika msiba ngoja tuone
__________________
I.T. Specialist and Digital Security Consultant |
|
#3
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Shy !,Tumeipeleka habari hii kwenye magazeti...itaonekana kama ilivyo chini
Mike Sikawa wa BBC afariki dunia MTANGAZAJI wa idhaa ya Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Mike Sikawa (55) ,amefariki dunia jana mchana baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kisukari. Sikawa, ambaye pia aliwahi kufanya kazi katika Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN) inayomiliki magazeti ya Daily News na HabariLeo, alifariki dunia juzi majira ya saa 8.47 mchana nyumbani kwake Njiro, nje kidogo ya mji wa Arusha. Kwa mujibu wa mdogo wake marehemu, Mchungaji Charles Sikawa, ndugu yake alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu na kutokewa na kidonda mguuni. Mchungaji huyo alisema ndugu yake alipata matibabu katika hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwamo AICC, KCMC, St. Thomas na Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili iliyoko Dar es Salaam lakini hakupata nafuu yoyote. Alisema ilifika wakati nusura akatwe mguu uliokuwa na kidonda lakini madaktari walifanikiwa kukwangua nyama ya mguu wa kidonda lakini haikuweza kusaidia. Mchungaji huyo aliendelea kusema kuwa baada ya kuhangaika kwa muda mrefu katika hospitali mbalimbali hapa nchini na kushindwa kupata nafuu, Sikawa alikuwa akipata matibabu akiwa nyumbani kwake hadi alipofikwa na mauti. Alizaliwa King’ori wilayani Arumeru mkoani Arusha na kusoma elimu ya msingi katika eneo hilo kabla ya kufaulu na kuendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Ilboru na Mzumbe ya mkoani Morogoro. Katika miaka ya 1970, aliajiriwa katika kampuni ya TSN kama mwandishi wa kawaida na baadaye kujiunga na idhaa ya Kiswahili ya BBC kama mtangazaji. Ameacha mjane na watoto wawili ambao wako Amerika ya Kusini. Mipango ya maziko inasubiri ndugu, jamaa na marafiki walioko nje ya mkoa wa Arusha na sehemu zote alizofanyia kazi. Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha-Rose Migiro ametuma salamu za rambimbi kutokana na kifo cha mwandishi huyo na kuelezea jinsi alivyoguswa na msiba huo. Dk. Migiro alisema alipoteuliwa kushika wadhifa huo katika UN, Sikawa alikuwa mwandishi wa kwanza kumtafuta kwa ajili ya kumhoji juu ya uteuzi huo.
__________________
Its not enough to do good if you can do better. |
|
#4
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Poleni na msiba wafiwa wote, Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi. Amina.
__________________
Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" |
|
#5
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Rest in peace Mike.
__________________
|
|
#6
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Mungu amrehemu Mike Sikawa na pole wafiwa wote
__________________
To be able to do everything by knowing nothing is dangerous
E-mail: masanilo@jamiiforums.com |
|
#7
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi aliyemuumba Mike Sikawa, hatimaye amemrudisha kwake.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana libarikiwe. Amen. Poleni wafiwa wote, Mwenyezi Mungu awape nguvu na uvumilivu wakati huu mgumu wa majonzi.
__________________
Wa-Tanzania tupendane, tushirikiane, tuijenge nchi yetu. |
|
#8
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Mwawado,
Nimeipokea habari hii kwa masikitiko makubwa. Nilimfahamu Mike Sikawa kwa muda mrefu. Katika ziara yake hapa Marekani alinipigia simu akiwa ubalozini na nikamchukua nyumbani kwangu. KInachonisikitisha ni kwamba he died too young. 55 is a very young age, lakini mapenzi ya mwenyezi Mungu hayana makosa. I will miss him and may his family find refuge in the fact that he was loved by many. |
|
#9
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
RIP Mike Sikawa
__________________
Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problems,
But, if you think again, neither does milk." Vituko Vya Zenj |
|
#10
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Ilikuwa inatia raha sana kusikiliza BBC. RIP brother.....
__________________
A positive attitude may not solve all your problems,but it will annoy enough people to make it worthwhile......
«
Previous Thread
|
Next Thread
»
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako! All times are GMT +3. The time now is 06:35 PM.
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com | ||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||