Mkuu Tanzania Bado sana, Na Tatizo kubwa linalo kabiri wafanya biashara wa Tanzania ni kupenda kufanya Biashara kiujanjaujanja sana, sasa sehemu ambazo hazina njia za mikato wanapata shida sana, that is wahy
MFANO:
1. Chukulia Ujenzi holela wa magorofa yasiyo fuata utaratibu kule kariakoo- Nchi nyingine hawana njia za mikato ni lazima sheria zifuatwe,
2. Cheki sheri za mafuta zinavyo jengwa bila kufuata sheria
KWA NCHI AMBAZO ZINAFUTA SHERIA ZOTE NA HAKUNA RUSHWA HATA KIDOGO WABONGO TUNAPATA SHIDA SANA
Swala Jingine ni Watanzania kuto penda kabisa kufanya Network, tunasubiri serikali ndo ituambie twende SUDANI, wakati wakenya wao wameenda wenyewe na wala hawajasubiri kuambiwa, kwenye bara la africa kuna Maonyesho kibao ya biashara lakini sijui kama Watanzania huwa wanahudhuria,
Angalia hata Maonyesho ya Sabasaba, Wakati Wafanya biashara wa Nchi zingine wamekuja kutafuta masoko na kutafuta watu wa kufanya nao BIASHARA Watanzania tuko bise kuuza, na ukipita Banda la wabongo usipo nunua wananuna, Wakati wachina wako bise kuchukua contact na kuuliza kama mnaweza fanya biashara,
Nakumbuka kuna kipindi fulani kule Arusha wakati Jumuia ya Africa mashariki ndo inaanza, Kulifanyika MAONYESHO YA WAFANYA BIASHARA WA NCHI TATU KWENYE UWANJA WA MPIRA WA ARUSHA, na yalikuwa maalunu kwa ajiri ya wafanyabaisha wa Tanzania , kenya na Uganda kufahamiana, Cha kushangaza WAFANYA BIASHARA WA TANZANIA WAKATI WANAITWA KUJITAMBULISHA WAO WALIENDA NA BENDI YA TOT kipindi hicho ikipiga Bilingo, na hawakuwa na cha kuonyesha, Wakati wenzao wa Kenya na Uganda walikuja full na Business card na kazalika, Wabongo hata Business card waliona haina haja, KWA KIFUPI NDO HIVYO,
Maonyesho ya SABASABA ni PICHA tosha kwamba hatuwezi hata kwenda Burundi Achilia mbali huko SUDANI KUSINI, maonyesho yametawaliwa na Promosheni za pombe, full miziki, na full kuchuuza bidhaa za kichina, NA KINACHO UMA ZAIDI NI KWAMBA UCHUUZI UNAOFANYWA NA WATANZANIA PALE NI WA KUCHUUZA BIDHAA ZA CHINA BORA HATA ZINGEKUWA ZA TANZANIA, hivi kwa stail hii tunaweza enda SUDANI?
Mkuu kwa kifupi ni vigumu sana na Mifano ni mingi sana hata humu JANVINI KUNA MIFANO TOSHA,
Follow Us Here