Hapa kuna takwimu za uzalishaji wa dhahabu Tanzania kwa miaka 11 iliyopita.
Mwaka
Kilo
Ounce
Average price
$/ounce
2001
30,090
962,880
271.04
2002
43,320
1,386,240
309.73
2003
48,018
1,536,576
363.38
2004
48,178
1,541,696
409.72
2005
52,276
1,672,832
444.74
2006
47,000
1,504,000
603.46
2007
40,193
1,286,176
696.39
2008
36,434
1,165,888
871.96
2009
40,000
1,280,000
972.35
2010
35,600
1,139,200
1224.54
2011
40,400
1,292,800
1571.52
Bei ya dhahabu inazidi kupanda. Ilifikia kiwango cha juu $1781 tarehe 28 Februari, na hivi sasa ni around $1600.
laiti Taifa lingefaidika kikamilifu na dhahabu hii!
Iwapo wakati wanafanya appraisal ya kuanzisha miradi bei ya dhahabu ilikuwa chini hivyo, na bado wakafanya projection ya faida wakaona inalipa, kisha bei inapanda kiasi kikubwa hivi Makampuni hayo yanafaidi kweli.
Kwa kiasi kilichozalishwa mwaka jana, hata ukisema kuwa gharama ya uzalishaji kwa ounce ni $500, bado mapato ya madini ni zaidi ya $1.2 billion!
Kama makampuni hayo yangekuwa yanalipa kodi 30% pato la TRA kutokana na hayo madini lingekuwa $360 millioni, sawa ma Shilingi billioni 576!
Lakini katika walipa kodi wakubwa makampuni ya madini hayamo (isipokuwa Resolute tu)!!!!
1. Tanzania Breweries Ltd. (Shilingi Bilioni 165.4); 2. National Microfinance Bank (ShilingiBilioni 108.6); 3. Tanzania Cigarette Company (ShilingiBilioni 92.1); 4. National Bank of Commerce (Shilingi Bilioni 89.9); 5. CRDB Bank Ltd. (ShilingiBilioni 79.2); 6. Tanzania Ports Authority (Shilingi Bilioni 76.8); 7. Tanzania Portland Cement (ShilingiBilioni 73.4); 8. Airtel (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 63.6); 9. Tanga Cement Company Ltd. (Shilingi Bilioni 43.6); 10. Standard Chartered Bank Ltd. (Shilingi Bilioni 40.0); 11. Citibank (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 35.7); 12. Resolute (T) Ltd. (Shilingi Bilioni 32.1); 13. Tanzania International Container Terminal Services (Shilingi Bilioni 25.9); 14. Tanzania Distillers Ltd. (Shilingi Bilioni 13.4); na 15. Group Five International (PTY) Ltd. (Shilingi Bilioni 9.5).
Source: Hotuba ya Waziri Mkuu Bungeni
hapo nimeona tu Resolute ule mgodi wa nzega ambao ndo wanataka kuufunga (wengine wanasema wanawauzia barrick sijui), ila pale yamebaki mashimo tu gold imeisha....sijasikia barrick wanatoa kiasi gani,...kuna ndege kila wiki inatoa gold toka barrick kule kahama bunzwagi, bulyanhulu na Tulawaka...lakini kwa migodi yao yote hii ukiongeza na nyamongo, ndo kusema hawatoi kodi? sasa hawa watu wa nini?>si bora wasingekuwepo?
Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!
Follow Us Here