Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 51
    1. #1
      tanga kwetu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Posts : 936
      Rep Power : 650
      Likes Received
      116
      Likes Given
      30

      Default Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Nina umri wa miaka 37 na nimeoana na mke wangu huyu miaka mitani iliyopita na tumejaaliwa mtoto mmoja wa miaka mimme na nusu sasa.

      Maisha yetu kiuchumi na kimahusiano ni mazuri...kama kuna mikwaruzana ni ile 'ya kawaida' ndani ya ndoa.


      Sie wote ni asili yetu ya bara na tumekulia katika maadili mazuri ya Kikristo. Wazazi wetu wote hawakuwavalisha watoto wao yale 'makolokolo' ambayo watoto wengi huwa wanavaa na hadi sasa kati yetu wawili hakuna aliye na 'chale' mwilini kumaanisha kwamba hatukuwa waumini wa mambo ya kienyeji!


      Last week nilikuwa safarini kikazi lakini nikarudi nyumbani siku 1 kabla ya siku iliyokuwa ikijulikana pale nyumbani. Nyumbani hakukuwa na mtu maana wote huwa tunaenda makazini na shuleni except housemaid aliyekuwa amesafiri wakati huo. Kwa kuhitaji Pasi (Iron) iliyokuwepo chumba cha wasichana kinachotumiwa na housemaid na mdogo wake wife, niliifuata. Next to ilipokuwepo Pasi, kulikuwa na mfuko mdogo wa plastic (Rambo) ambao nilivutiwa kuuangalia.


      Nilipoufungua-nilikaribia ku-faint kwa niliyoyaona!!!!! Kulikuwa na karatasi kama 3 zenye maandishi ya kiarabu na in between some lines kulikuwa na ama jina la mke wangu au langu. Pia kulikuwa na karatasi kadhaa zilizoandikwa kiarabu na maelezo kama 'CHOMA OGA 1 X 2 SIKU 3, CHOMA MWINAMO' pia kulikuwa na vitu kama unga unga kwenye makaratasi yenye maelekezo 'CHAKULA LIMBWATA' na 'KUNYWA 1 X 3 SIKU 6 na KUNYWA USIKU TU SIKU 2'.

      Kiufupi ni tunguri za limbwata. Nikaenda mjini kuwatafuta wanaojua maandishi haya na kuongeza uhakika niliwaulizia watu wawili tofauti sehemu tofauti na wote walinitafsiria kitu kimoja kwamba ni dawa toka kwa mganga za mtu anaeitwa (jina la mke wangu ndani ya baadhi ya karatasi zile) akitaka kumtia kwenye chupa mtu anaeitwa (jina langu) yaani nisisikie wa kuona wala kupinga chochote!
      Nilipowauliza, eti shemeji yangu anasema mzigo ni wa kwake ambapo kwa mimi naamini kaamua kuji-sacrifice. Wife yeye ameendelea kuukana katkata ule mzigo.

      My take:
      Kama ameshaanza biashara ya waganga wa kienyeji, leo kwa hilo, next time ataniendea kwa lipi? Mke wangu hakuwa mshabiki kabisa wa mambo kama hayo, sasa hofu yangu ni kwamba ameshaanza mambo ya mjini likely kudanganywa na wanawake wa mjini (Tanga) maana ni mambo common.
      What should I do?


    2. #2
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 15,052
      Rep Power : 3723
      Likes Received
      3621
      Likes Given
      5885

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Duuuh pole sana labda wife anakupenda sana anaona aendee kukandamizia malav dav.
      Kuna jamaa mmoja nafanya nae kazi huwa anasema akimuona wife anamfanyia Limbwata atamwambia ongeza tu mama eti kwa vile anamfanyia yeye ampende kwa hivo sio mbaya:A S 8:
      Mkalishe na umuulize kwa nini ana hayo matunguli ndani
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..
      Hadi tufike 2015 tutakuwa tumekoma

    3. #3
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,328
      Rep Power : 3455
      Likes Received
      1339
      Likes Given
      864

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Mkuuu huku utapata wezi wa ndoa yako tuuuuu basii we kaa na mkeo tafuta sababu za yeye kufanya hivyo na mwambie anataka uweje mkae msuluhishe hata familia awatakusaidia nasema hivi kama mwanandoa nikiwa nimesimama na ndoa iliopita kwenye mabonde na milima wewe na mkeo ndio suluhisho la hili na kama uamini mpigie hata wazazi wako hii issue uone kama mtakaa kwa amani la maana simama na mungu kama aujaokoka anza sasa bado ujachelewa karibu sana pale biafra kwenye nyumba ya ibada kwa mwakasege upate neema ya bwana mungu asimame na ndoa yako tunaitaji kumwachia mungu asimame na ndoa zetu watu wengi wanahisi ukiwa na pesa nyumba nzuri shule nzuri na mengineyo ndoa imetulia kwa info wenye haya yote waulize usiku wanalalaje wacha ukiwaona mjini wanacheka kama si mngo wa 4 basi gorofa ya chini na ya juu isiwe kwako in jesus name

    4. #4
      Kigogo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,484
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1302
      Likes Given
      318

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      piga chini huna mke hapo mjukuu wangu

    5. #5
      Lukolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Location : Iringa
      Posts : 4,104
      Rep Power : 7086
      Likes Received
      2267
      Likes Given
      1706

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Kwa vyovyote vile shemeji yako ameamua kujilipua ili kulinda ndoa ya dadake. Pole sana mkuu. Biblia inasema enyi wanaume ishini kwa akili na wake zenu, na inasema wanawake ni viumbe wadhaifu. Usimuache, bali chukua tahadhari kwa kila jambo mnalofanya naye. Maji ya kuoga, chakula na vitu kama hivyo. Jitahidi kuhakikisha kwamba akikuandalia maji basi mnaoga wote, akiandaa chakula, mnakula wote pia.
      Mtaji mkubwa kabisa wa CCM katika chaguzi zake ni umaskini na ujinga wa watanzania. CCM haitafanya kosa la kuyamaliza matatizo hayo kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wamehatarisha nafasi yao ya kuendelea kutawala


    6. #6
      Ramthods's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd June 2009
      Posts : 443
      Rep Power : 600
      Likes Received
      54
      Likes Given
      49

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Pole mkuu kwa yaliyokufika.

      Tatizo kubwa ambalo mi naliona hapo si kumshika mkeo na hayo 'makorokoro', bali ni huko kuukana huo mzigo.

      Kukosea kwa binadamu ni jambo la kawaida. Mkeo kama mtu mwingine anaweza teleza kwa kushawishiwa na rafiki/mashoga n.k na kujikuta katika matatizo asiyoyatarajia. Hili ni jambo la kawaida, hata sisi wanaume tunakosea mara kwa mara tu.

      Cha msingi sio kukosea, bali ni KUKUBALI KOSA na kuahidi kujirekebisha. Kama mtu hakubali kosa alilofanya, kuna uwezekano mkubwa kuwa hataliacha, pengine kwa sababu anaona ni sawa yeye kufanya hivyo, na uwezekano mkubwa ni kwamba atalirudia hilo kosa siku za mbeleni.

      Mkeo kutakaa kuwa hayo madubwana ni yake, inawezekana kuwa ana hofu na kile kitakachofuata pindi atakapokiri kuwa ni yake.

      Mimi ningekushauri utafute nafasi wewe na mkeo mkiwa mmetulia (pengine muende outing n.k), ongea nae kwa upole (usiwe mkali), mweleze ni nini madhara ya limbwata, na cha msingi mwonyeshe ni jinsi gani unamjali na kumpenda hivyo hakukuwa na haja ya yeye kufuata limbwata.

      Mwambie kwamba tayari umeshamsemehe, ila akuahidi kuwa hato rudia tena.

      Pia, nisingependa kuelemea upande mmoja. Hata wewe pia inabidi ujichunguze mwenendo wako. Inawezekana umebadilika na mkeo anahisi una hawara nje. Hakuna mwanamke aliye tayari kupoteza ndoa yake, tena ukizingatia mna mtoto na bado anakupenda. Atafanya juu chini kuhakikisha anaendelea kukumiliki. Kama mwenendo wako umebadilika kwa kiasi fulani (mfano kama kupungua kwa mapenzi), hata wewe utakuwa umehusika kiasi fulani kumshinikiza mkeo kutafuta njia za kukuweka karibu nae, ingawa alitumia njia isiyo sahihi.

      Natumaini hamta achana wewe na mkeo umpendaye. Lakini lazima uelewe kuwa kuna umuhimu wa wewe na mkeo kuwa karibu sana na Mungu kiroho na sio kimwili kawa walivyo wengi. Wekeni ratiba za kusali na kufanya ibada nyumbani, wewe mkeo na wote wanaoishi chini la paa la nyumba yako. Hayo yanayotokea kwenye nyumba yako sasa ni madhara ya kufanya ibada kwa mazoea - unaenda kanisani lakini hubadiliki kiroho.

      Pia, angalia sana mwenendo wa mkeo na marafiki zake, na ndugu zake pia. Pengine mdogo wa mkeo ndio mshauri wa hayo mambo? sisi sote hatujui. Ila usimwache mkeo mbali kiasi cha kuwa na tabia kama hiyo ambayo hukuitarajia (maana umesemea karibu uzimie ulipokutana na huo mfuko).

      Nakutakia kila laheri.
      .... ukiniazima tochi mchana haitanisaidia ....

    7. #7
      22nd's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st August 2010
      Posts : 488
      Rep Power : 548
      Likes Received
      105
      Likes Given
      151

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      mi hata sioni tatizo kama hiyo story hapo ya first lady, kama hilo limbwata ni kwa ajili ya wewe kumpenda mkeo poa tu tena mpe ushirikiano ila mapenzi yawe motomoto as long as sio la kukudhuru kiafya au kuondoa uhai
      ni mimi wa tanga handeni,nawakilisha

    8. #8
      Pengo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th October 2009
      Posts : 581
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Pole sana,ukiona hivyo jua tayari ameshaliwa na wajanja ndio maana anatafuta njia ya kukudhibiti wewe,loh maskini tunda lako limemegwa na wakwale!

    9. #9
      Lukolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2009
      Location : Iringa
      Posts : 4,104
      Rep Power : 7086
      Likes Received
      2267
      Likes Given
      1706

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Quote By Pengo View Post
      Pole sana,ukiona hivyo jua tayari ameshaliwa na wajanja ndio maana anatafuta njia ya kukudhibiti wewe,loh maskini tunda lako limemegwa na wakwale!
      Acha kumpanikisha mwenzio bwana! Wakati mwingine hapa JF si pazuri kuomba ushauri, maana unaweza kupotoshwa kabisa. Kwa ushauri kama huu wako Pengo, unamtaka mwenzio avunje ndoa yake? Inawezekana pengine kuna vitu walipishana naye humo ndani, jamaa akaonyesha kuwa yeye ni kichwa kwa hiyo hakuna mwingine wa kuongea, au inawezekana jamaa huwa anarudi usiku na mke ana wasi wasi kwamba jamaa anamega kwingine kwa hiyo anataka amtulize nyumbani.

      Mkuu usimsikilize Pengo, muamini mkeo na tafuta namna ya kuyamaliza na mrekebishane pale ambapo mwenzako aliona panapelea na akataka aparekebishe kwa limbwata.
      Mtaji mkubwa kabisa wa CCM katika chaguzi zake ni umaskini na ujinga wa watanzania. CCM haitafanya kosa la kuyamaliza matatizo hayo kwa kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wamehatarisha nafasi yao ya kuendelea kutawala

    10. #10
      Nyani Ngabu's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,521
      Rep Power : 0
      Likes Received
      9766
      Likes Given
      696

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Mapenzi hayana dawa....

    11. #11
      Tall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2010
      Location : Tandale kwa mtogole
      Posts : 1,431
      Rep Power : 763
      Likes Received
      142
      Likes Given
      245

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      1.HAYA MAMBO SI YA KUYAOGOPA SANA.........HUKUWA NA HAJA YA KUTEMBEZA KIKARATASI ILI UKA TAFISIRIWE.
      2. SIO SIRI HUAMINIKI KABISA KWA MKEO.
      3.TATIZO KUBWA KABISA LA USHIRIKINA NI KIFO AU KILEMA.........KAMA WEWE NI MWANAMKE NA UNAENDA KWA MGANGA...NA MGANGA MWENYEWE KWA MFANO AWE MWANAMME,SIKU AKIKUPENDA HAWEZI KUKUPA DAWA YA MAPENZI....BALI KUMMALIZA MMEO,,,,KAMA SI KUMUUA MUMEO BASI KUMFANYA ******* WA KUDUMU ILI AKUCHUKUE WEWE UWE WAKE.
      4.HAKUNA UJINGA NA HATARI KWA MWANAMME AU MWANAMKE KWENDA KUTAFUTA DAWA YA MAPENZI KWA MGANGA TENA MGANGA MWENYEWE AKIWA NI OPPOSITE SEX.
      5.DAWA UNAYO MWENYEWE.BORESHA KAULI YAKO KWA MWENZIO NA AVOID KUMUUDHI...USIMUUDHI KABISA NA MWISHO FANYA VILE ANAVYOTAKA. HIYO NI ZAIDI YA LIMBWATA TENA NI FREE OF CHARGE.
      UMEMUULIZA, KAKANA BASI ENDELEA NA MAISHA...AFTERALL UMESHABUGIA SANA MIDAWA YA MKEO,
      MSAMEHE,MWONYE ASIRUDIE.
      Mwisho kabisa kuna umuhimu wa kukiombea chakula ulichotayarishiwa kwa nguvu zote.PIGA SARA YA UHAKIKA......HADI ASHINDWE KUSEMA AMINA. aaaaah na maji ya kuoga uliyoandaliwa,mmmmh,?? hayo akili kichwani mwako..............NILIKUWEPO.
      always use low profile........ajikwezae atashushwa.

    12. #12
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,731
      Rep Power : 1295
      Likes Received
      512
      Likes Given
      178

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      huo ndio mzigo mmoja tu uliuona, nadhani hapo nyuma ulishakula sana limbwana na kunywa maji ya maiti, haya mapenzi ni noma, Mungu kakufunulia hilo, nadhani hilo lilikuwa la kukumaliza, Mzee ungekuwa bone la zuzu

    13. #13
      Tall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2010
      Location : Tandale kwa mtogole
      Posts : 1,431
      Rep Power : 763
      Likes Received
      142
      Likes Given
      245

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Quote By Kigogo View Post
      piga chini huna mke hapo mjukuu wangu
      Ataacha wangapi? anaweza akamwacha huyu pasipokujua akaja kuoa mwenyekiti wa wachawi.Wala usimwache mkuu....endelea nae.
      always use low profile........ajikwezae atashushwa.

    14. #14
      ChiefmTz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2008
      Posts : 1,504
      Rep Power : 871
      Likes Received
      112
      Likes Given
      38

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Quote By tanga kwetu View Post

      Nilipowauliza, eti shemeji yangu anasema mzigo ni wa kwake ambapo kwa mimi naamini kaamua kuji-sacrifice. Wife yeye ameendelea kuukana katkata ule mzigo.

      My take:
      Kama ameshaanza biashara ya waganga wa kienyeji, leo kwa hilo, next time ataniendea kwa lipi? Mke wangu hakuwa mshabiki kabisa wa mambo kama hayo, sasa hofu yangu ni kwamba ameshaanza mambo ya mjini likely kudanganywa na wanawake wa mjini (Tanga) maana ni mambo common.
      What should I do?
      Sina uhakika na umri wa Shemejio, lakini usije shangaa ikawa ni kweli kwamba Shemeji yako ndiye mwenye huo mzigo anataka kuwadhibiti wewe na mkeo ili kila atakachosema mumkubalie.

    15. #15
      AK-47's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2009
      Location : Abbottabad
      Posts : 1,366
      Rep Power : 761
      Likes Received
      149
      Likes Given
      80

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Pole sana ndugu nimeshindwa hata pa kuanzia nikushauri vipi maana inahitaji hekima mno na mie leo hekima zangu zipo katika mgomo
      An Eye for an Eye Makes the whole World Blind

    16. #16
      Remmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2009
      Location : home
      Posts : 4,388
      Rep Power : 7781
      Likes Received
      1560
      Likes Given
      1826

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Pole sana mkubwa.haya ndo ya ulimwengu. sina comment zaidi ya kukupa pole.

    17. #17
      cheusimangala's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2010
      Posts : 2,597
      Rep Power : 1000
      Likes Received
      442
      Likes Given
      608

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      mmh pole.
      A baby is something you carry inside you for nine months, in your arms for three years and in your heart till the day you die

    18. #18
      Ngala's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th September 2009
      Posts : 160
      Rep Power : 527
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      nikupe pole kisha niwakumbushe kuwa ajapomwacha huyu ajaye anajua atakuwa wa aina gani? pengine atakuwa zaidi ya huyu na akaongeza ufanisi na umakini zaidi hivyo kusudio likakamilika? limbwata usijeliona ni balaa kubwa mno.waweza kuwa zezeta ghafla mno kila atakalo unamtimizia bila mjadala.aweza kukwambia lala mii natoka mzee utajikunja ye anakwenda na mambo yake.kimsingi nyumba za hivyo sii za kupigiwa mfano. na mara nyingi maendeleo ni ziro.zungumza nae kwa upendo mweleweshe madhara ya hayo ayatafutayo

    19. #19
      KAPERO's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th July 2010
      Posts : 46
      Rep Power : 462
      Likes Received
      8
      Likes Given
      0

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      Pole sana. usihofu juu tunguri. wala huna haja ya kumwogopa mwenzio. kwa vile umesha gundua kuwa yeye anakutafutia dawa umpende! hapo ni dhahiri kuwa ameona mapungufu kwako.
      la kufanya sasa jitahidi kumweka karibu sana mkeo na umwambie awe huru kukueleza yale yote angependa umtendee. kama yanatekelezeka mkubalie.
      tena usisahau kumwelimisha juu ya matapeli wa kiganga! jamani watakumalizieni hela zenu na mwisho wa yote watamharibia ndoa yake. awe makini sana na mashoga na hata kama ni dada yake,, huenda wamekwisha ona mnaishi vizuri sana sasa donge limewashika.

      mkuu jitahidi sana huyo anae taka umpende ujue kwako kafika.

      wahenga husema!!! Heri akupendaye, kuliko unae mpenda!

      nakutakieni heri na baraka. Mungu akujalie hekima na busara tena akujaze roho ya upendo.

    20. #20
      Lady N's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2009
      Location : Dar es salam
      Posts : 1,905
      Rep Power : 871
      Likes Received
      97
      Likes Given
      84

      Default Re: Nimekamata tunguri za limbwata za mke wangu, nimfanyaje?

      mnunulie cd ya kekundu ya AIC makongoro kwaya, asikilize wimbo wa Kekundu
      "BUSINESS FOR FRIENDSHIP IS BETTER THAN FRIENDSHIP FOR BUSINESS"

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Keko: Umbea,na Temeke: Tunguri
      By trachomatis in forum JF Chit-Chat
      Replies: 3
      Last Post: 31st October 2011, 21:51
    2. Keko: Umbea,na Temeke: Tunguri
      By trachomatis in forum JF Chit-Chat
      Replies: 10
      Last Post: 29th October 2011, 16:53
    3. Nimfanyaje huyu house girl wangu
      By Nduka Original in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 143
      Last Post: 8th August 2011, 18:32
    4. Nimekamata vitabu vya NDOA YANGU, NINGEJUA - vilivyoibwa
      By kautipe in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 26th July 2011, 23:08

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...