Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

    Report Post
    Results 1 to 6 of 6
    1. #1
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,319
      Rep Power : 3453
      Likes Received
      1334
      Likes Given
      863

      Default Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      Nimeachwa, nimechanganyikiwa, sina mwelekeo!



      Kuvunjika moyo, kukatishwa tamaa, upweke, nk ni maneno yanayoelezea feelings za uzoefu ambao binadamu hupitia pale mahusiano yanapovunjika iwe urafiki wa kawaida, uchumba au ndoa.


      Wakati mwingine aliyeachwa huamua hata kutishia kwamba atajinyonga wasiporudiana au tishia kufanya kitu chochote au kujitoa hata kuhonga chochote anachoweza na bado juhudi zote huzaa nothing na hali kuwa mbaya zaidi.

      Kuachwa hasa uchumba huumiza sana wakati mwingine kwa sababu aliyekuacha (dump, abandon) anaweza kumuoa/olewa rafiki yako au ndugu yako au mtu kwa karibu na wewe unayemfahamu na zaidi unakutana nao mitaani na inaawezekana wewe ni mzuri zaidi yake.

      Kila survivor wa kuvunjika kwa mahusiano huendelea kuwindwa na mabaki ya hofu na mashaka ya mahusiano yatakayofuata.

      Wapo ambao baada ya mahusiano kuvunjika huanza mahusiano mapya ambayo huvunja moyo tena kama mara ya kwanza na hawakati tamaa na hujifunza kwa kuondoa hofu na mashaka na kujenga trust upya na kuendelea kufurahia mahusiano mapya tena.

      Wengine huruhusu vidonda (emotional) kuendelea kuwatawala na wanakuja wamejifungia (locked) kutoruhusu kupenda na kupendwa upya.

      Jambo la msingi ni kwamba maumivu ya kupotelewa au kuachwa na mtu unayempenda ni moja ya maumivu makali sana na baada ya kuachwa kupenda tena huwa ni moja na hofu kubwa sana mtu anapitia katika maisha yake kwani wengi hujikutana wanakutana na walewale.

      Unapompenda mtu kwa moyo wako wote na hisia zako zote na kwa mapenzi yako yote, mahusiano yanapovunjika maisha hubadilika na kuathiriwa kiasi cha kusimama ghafla.
      Kuna usemi kwamba
      “Usually the first love lost is the most painful”

      Jambo linalostua zaidi ni kwamba wale wanauumia zaidi ni mwanaume au mwanamke ambaye hata baada ya mahusiano kuvunjika (mfano uchumba) bado hung’ang’ania au kuendelea kutaka warudiane kwa kuwa walikuwa deep na attached kwenye hilo penzi, hujisikia bila huyo mtu hupo desperate na hana control.

      Na wakati mwingine hufikiria mbali zaidi kwa kuamua kufanya kitu chochote kuhakikisha wanarudiana kibaya zaidi partners wao huwa walishafanya maamuzi na hawawezi kurudi tena.

      Pia unapoachwa na mpenzi feelings zako hujigawa pande mbili, upande wa kwanza unakwambia unaweza kuanza mahusiano mapya sasa na upande mwingine unakwambia usifanye na ukifanya au jiingiza kwenye kupenda tena utaishia kuumizwa kama mwanzo.

      Pia kuacha au kuachwa hujenga kujisia hatia (guilt) bila kujalisha wewe ni uliyeachwa au uliyeacha, rejected au rejecting, dumped au dumper wote huwa na hisia za kujiona ni failure.

      Kujisikia hatia hujenga hali ya kujisikia kutojiamini na kutojiamini huzaa hofu ambayo huendelea kukuwinda kila mara unapokumbuka mahusiano yalivyovunjika.

      Hiyo hofu huingia akilini na kugonga kama nyundo kukumbushia machungu na makali ya kuachwa hadi unafikia hali unajikuta kuchanganyikiwa kama si kupaniki.

      Vilevile hofu hii huweza kupooza hatua yoyote unayotaka kuchukua ili kuanza mahusiano mapya na unajikuta huwezi kuwekeza tena kwenye kupenda na kupendwa upya, unakuwa mwoga kupenda upya na unaogopa pia kukaa mwenyewe bila mtu wa kukupenda, ni kizunguzungu tu.

      Jambo la kujiuliza kwa nini unajisikia hatia je, ni kweli ni wewe uliyesababisha mahusiano kuvunjika au ni illusions tu?

      Je, ni kweli ulivunja kiapo (vow/covenant) ulichoahidiana na mpenzi wako?

      Je, ni kweli hukuwa responsible kwenye mahusiano hadi hajavunjika?

      Kama si kweli basi unajichukulia lawama ambazo hustahili.

      Je, ni hatua ngapi mtu aliyeachwa anaweza kutumia ili kuponya maumivu yake na kurudi kwenye maisha ya kawaida?



    2. #2
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,348
      Rep Power : 3064
      Likes Received
      3109
      Likes Given
      4229

      Default Re: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      kuna mtu alisema mapenzi ni kama daladala, unapanda unashuka na mwingine anapanda nawe unapanda kwenye daladala nyingine! no hard feeling man!
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    3. #3
      PakaJimmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 14,896
      Rep Power : 22566
      Likes Received
      6515
      Likes Given
      2929

      Default Re: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      Kuna Msanii mmoja sijui ni wa asili ya Congo anaimba..."Mbaya zaidi ni vile yule aliyekuacha ananenepa wakati wewe unayempenda unaendelea kukonda!"

      Ndugu yangu haya mambo ni mazito!...Usiombe ukaachwa kama bado unapenda, maana utaona dunia inakuchapa fimbo za ugoko!

      Dawa ya haraka ya kuponya jeraha la kuachwa haipo. maana utaendelea kuwaza saana, na mtu akikwambia "usiwaze ndo anakuchochea kuwaza zaidi!

      Muda huwa unaongea!
      Baada ya kipindi fulani automatically mawazo yanaanza kupungua! Dawa ni hiyo!....MUDA!
      "The only thing that walks back from the tomb with the mourners and refuses to be buried is the character of a man.
      What a man is, survives him... it can never be buried"
      (GENEKAI-Jamiiforums, 4th November 2010 07:32PM).
      [email protected]

    4. #4
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,348
      Rep Power : 3064
      Likes Received
      3109
      Likes Given
      4229

      Default Re: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      so they say PJ, its about time............But I wonder why people are scared to death of kuachwa/kuachika even if they are not madly in love. watu wanasahau kuna mazoea na mapenzi. kama mmezoeana tu hakuna kuchanganyikiwa,sana sana yatakuwa mawazo ya siku mbili tatu then kwishinei.

      ISSUE NI KWAMBA, UNATAKIWA USIFANYE MAAMUZI YOYOTE NDANI YA HIZO SIKU CHUNGU, UTAHARIBU!!
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    5. #5
      nestory's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st July 2008
      Location : dar es salaam
      Posts : 22
      Rep Power : 561
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      dawa ni kama alivyo jamaa yangu hapo juu,dawa ni muda lakini pia nataka kuongezea kitu:pia tafuta msicahana mwingine haraka ambaye mda mwingiutakua naye inaweza kukusaiia kupunguzza mawazo.kama utapata huyo mtu na akaweza kukubali vitu unavyompa,automatically utaona no need kuendelea kusumbua kichwa kumuwazahuyo mwanadada.najua mda unajiona kama hauwezi kitu,and u know nothing about love.....NO.is just that hukumpata yule aliye wako wa ukweli


    6. #6
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 15,043
      Rep Power : 3720
      Likes Received
      3614
      Likes Given
      5861

      Default Re: Kuponya Maumivu ya Kuachana (4)

      inabidi kuwa mtulivu na kufanya maumuzi ya yasiyokuwa na papara unaweza jikuta unaruka mkojo unakanyaga mavi
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..
      Hadi tufike 2015 tutakuwa tumekoma

    Similar Topics

    1. Mke anakwepa sana tendo la ndoa, nini kifanyike?
      By prosperity93 in forum JF Doctor
      Replies: 169
      Last Post: 20th March 2013, 21:05
    2. Kuachana
      By Felixonfellix in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 6
      Last Post: 30th October 2011, 15:45
    3. Kuponya maumivu ya kuachana part-1
      By Pdidy in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 5
      Last Post: 9th October 2011, 08:27
    4. Kuponya maumivu ya kuachana part-2
      By Pdidy in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 0
      Last Post: 14th September 2011, 21:18

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...