Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: jitahidi ujiamini mwenyewe

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      Pdidy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 12,283
      Rep Power : 3443
      Likes Received
      1322
      Likes Given
      855

      Default jitahidi ujiamini mwenyewe

      Nini maana ya kujiamini au staha?
      Kujiamini au Staha (self esteem) ni jinsi unavyojiona mwenyewe, ni image yako mwenyewe, kama una staha ya juu (high self esteem) maana yake unajiona mzuri kila eneo na kama una staha ya chini maana yake unajiona mbaya katika maeneo yote ya maisha yako.
      Kuwa na staha ya chini (low self esteem, low self image) ni ugonjwa unaowasumbua wanawake wengi sana katika jamii yetu ya sasa kuliko wakati wowote katika historia ya dunia.

      Tunaposema mwanamke fulani ana low self esteem au low self image tuna maana gani?
      Hii ina maana kwamba mwanamke anakaa mwenyewe na kuanza kujishangaa kwa nini hana marafiki wa kweli.
      Anakuwa na hamu ya kuongea na mtu ana kwa ana na anajua huyo mtu hayupo.
      Ni mwanamke anayejisikia kwamba wengine hawawezi kumpenda wakigundua kwamba ni yeye halisi so anajitahidi kujifanya fulani ili watu wampende.
      Ni mwanamke anayeogopa kuongeea na wanawake wenzake wa rika moja kwa maana kwamba yeye hayupo smart kama wao.
      Ni mwanamke anayeamini wafanyakazi wa kike wa ofisini kwa mume wake ni wazuri zaidi kuliko yeye hivyo kila siku mume akirudi anaonywa na kwamba ajihadhari na hao wanawake.


      Ni mwanamke anayejisikia mjinga fulani au maskini fulani au failure fulani hasa akiwa nyumbani kwake peke yake akifikiria maisha.
      Ni kujishangaa kwa nini watu wengine wana uwezo na talents nyingi kuliko yeye.
      Ni mwanamke anayejisikia hapendezi na havutii tena kimapenzi (sexually unattractive).
      Ni mwanamke kujisikia ameshindwa kuwa mke na mama.
      Ni mwanamke ambaye hapendi kitu chochote kuhusu yeye na kutamani ingekuwa vile na vile kama wengine.
      Ni mwanamke kutamani muda wote angekuwa Fulani au angekuwa mtu mwingine.
      Ni mwanamke anayejisikia hapendwi na hapendi mtu na matokeo yake anafunikwa na huzuni na upweke.

      Ni mwanamke anayejisikia moyoni yupo empty hasa kwa kukosa upendo wa kweli.
      Ni mwanamke ambaye anahisi wanawake ambao mume wake anaongea nao ni wazuri kuliko yeye hivyo wanaweza kumchukua au kutembea naye.
      Ni mwanamke anayesubiri kuwe kweusi aanze kutoa machozi mazito kwa kujihurumia kwa hali aliyonayo na amefunikwa na msongo wa mawazo.
      Ni mwanamke anayejiangalia kwenye kioo na kujiona hafai na kutamani sura yake ingekuwa kama ya fulani au angekuwa kijana zaidi.
      Ni mwanamke anayejiangalia mwili wake na kujiona amenenepa na kwamba hakuna mtu atampenda tena na kwamba maisha yake ya kimapenzi na mumewe mwisho kwa kuwa amenenepa mno.
      Na mengine mengi yanayofanana na hayo!

      Je, low self esteem huwapata wanawake tu?
      Kuwa na staha ya chini au ndogo si kwa wanawake tu bali huwapata zaidi wanawake.
      Low self esteem ni tishio la dunia nzima hakuna cha motto, kijana mzee, rangi, tamaduni au jamii au kabila wote hukumbana na kuwa na staha ya chini.
      Hili dubwana huweza kummeza mtu yeyote pale tu akianza kujisikia hayupo respected na mwingine.

      Asilimia 90 ya wazo la low self esteem au low self image hyujengwa kwa kuwaza kuhusu wengine wanavyowaza kuhusu wewe.
      Kawaida huwa inakuwa ngumu sana kujiamini mwenyewe kama the rest of the world wanaamini wewe ni dumb, ugly, mvivu, boring, uncreative, undesirable nk.

      “No one can stand the awful knowledge that he/she is not needed”

    2. Miaka 50

    3. #2
      4X4byfar's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Mwanza
      Posts : 134
      Rep Power : 565
      Likes Received
      3
      Likes Given
      9

      Default Re: jitahidi ujiamini mwenyewe

      Je, dawa yake nini sasa. Maana yaelekea wengine tunahiyo low.
      Every beginning has an end

    Similar Topics

    1. Replies: 74
      Last Post: 18th November 2011, 06:27
    2. Kwa mnaoenda baa baada ya kupata kinywaji jitahidi kurudi nyumbani
      By Dr Kingu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 4
      Last Post: 28th September 2011, 00:29
    3. Ipe title mwenyewe....
      By Bushbaby in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 8
      Last Post: 24th September 2011, 15:18
    4. Kipipa, kula ule mwenyewe tabu upate mwenyewe....
      By Pomole in forum Jamii Photos
      Replies: 1
      Last Post: 25th February 2011, 09:44
    5. Jionee mwenyewe!..
      By BelindaJacob in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 10
      Last Post: 18th July 2009, 17:29

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...