Mahusiano, mapenzi, urafikiTubadilishane mawazo kuhusu mahusiano, mapenzi, urafiki, n.k na kushauriana. TAFADHALI: Hii si sehemu ya kuweka picha chafu ama kutumia lugha kali sana. Zitafutwa!
Hey wana Jf,
Katika utamaduni wetu kama waafrika/ watanzania, mwanaume ndio wa kwanza siku zote kueleza hisia zake kwa binti kama anamuhitaji kimahusiano. Hivi sasa imekuwa tofauti kidogo, kuna baadhi ya wasichana wanaanza kueleza hisia zao kwa mvulana/Mwanaume kama anampenda au anahisia nae kimapenzi. Lakini hapa nchini kwetu inaonekana kama vile msichana anayemtaka kimapenzi mwanaume ni muhuni/ mapepe/malaya, majina yote hayo anapewa. Hii tabia ya msichana kumtongoza mwanaume hapa Tanzania kwa sasa bado watu wanaona kama msichana mwenye tabia hiyo ni muhuni au malaya, imekuwa tofauti na developed country hao hii tabia ni ya kawaida tu na wal si ajabu.
Je wewe kama mwanaJF na Mtanzania unalionaje hili, je ni sawa kwa msichana kumtongoza mwanaume? Au bado tubaki na mila/utamaduni wetu wa mwanaume kumtongoza mwanamke?
__________________ "The great pleasure in life is doing what people say you cannot do."
Hii ya kutongozwa si jipya wengine tumezoea ndo maana suala la kuowa lipo kando kabisa, wake za watu ndo kabisa wanakuambia live....mkienda semina hasa nje ya nchi ni kumegana kwenda mbele mradi utunze siri.
Nakubaliana na wewe mkubwa kwa asilimia kubwa maana hata mimi nayaona. Mambo yamebadilika sana siku hizi.Kumegana imekuwa sio issue tena
Wanawake hasa walioolewa wako juu sana kutongoza wanaume hasa wenye ndoa. Yamenikuta hivi karibuni, nikawaeleza jamaa zang wakaniambia mbona hiyo ni kawaida sana siku hizi? Nilishangaa sana. Mwanamke mke wa mtu, wana ndoa; yuko bize kichizi eti ananipenda hawezi kuishi bila mimi.
Dah! inapendeza wanaume kutongoza tu. Wanawake wasubirie kuimbiwa hayo mashairi, wayasikilize na vile aibu aibu mambo yanapendeza. Mambo gani mwanamke ameshupaa anasukuma ajenda ya kumtaka men! Hapana, sioni kama inanoga mie. Labda ajilengeshe tu lakini asianze yeye kuwa mwongoza mada.
Hii ni maada/mjadala tu, haimanishi hivyo kama ulivyofikiri.
usijipe presha mammy kwani ujawazoea tu wanaume wa JF??? utani ni tamaduni yaoo
but back to the point ni kwamba what matters ni jinsi gani unamuapproach huyo mwananume unaweza ukamuaproach as a woman au ukamuapproach as a hooker, u know wat i mean? usiende kwa mwanaume ukaanza kumwachia kifua wazi, mapaja wazi unag'ta ng'ata vidole utegemeee akuelewe kwamba unampenda kidhati ... atajua may be unamtamani na unajua kuna tofauti ya kumpenda mtu na kumtamani which is temporary its like asking someone do you feel like having sex na akisema yeah you do it en no string attached no hard feelings. but unaweza ukamuonyesha mwanaume kwamba nakupenda na kuact as a woman na akakuelewa bilieve me i know what am talkin about...
Wanawake hasa walioolewa wako juu sana kutongoza wanaume hasa wenye ndoa
Si kweli hawapendi sana walioowa maana hawapatikani kiurahisi kama sisi Mabachela....maana mwenye mke wakati mwingine anakuwa hana nafasi....mabachela unapatikana anytime ......nakuambia maofisini tunaona mengi....
__________________
To be able to do everything by knowing nothing is dangerous
Wanawake hasa walioolewa wako juu sana kutongoza wanaume hasa wenye ndoa. Yamenikuta hivi karibuni, nikawaeleza jamaa zang wakaniambia mbona hiyo ni kawaida sana siku hizi? Nilishangaa sana. Mwanamke mke wa mtu, wana ndoa; yuko bize kichizi eti ananipenda hawezi kuishi bila mimi.
Dah! inapendeza wanaume kutongoza tu. Wanawake wasubirie kuimbiwa hayo mashairi, wayasikilize na vile aibu aibu mambo yanapendeza. Mambo gani mwanamke ameshupaa anasukuma ajenda ya kumtaka men! Hapana, sioni kama inanoga mie. Labda ajilengeshe tu lakini asianze yeye kuwa mwongoza mada.
labda sugarmummy hilooo au mdada kaolewa na kizeee anataka damu changa inayochemka hahhahahaha kazi unayo........
Si kweli hawapendi sana walioowa maana hawapatikani kiurahisi kama sisi Mabachela....maana mwenye mke wakati mwingine anakuwa hana nafasi....mabachela unapatikana anytime ......nakuambia maofisini tunaona mengi....
Dah kwa jinsi navyo kujua wewe huachi kitu hapo lazima ukandamiza mkuu kwi kwi na unavyo jua wanajua sana neno kupenda dah we acha tu watu tunaogopwa kufumwa maana ukifumwa utakacho kipata hehehe.
__________________ Ukiuza utumbo usiogope nzi. Chuda Raha