Mahusiano, mapenzi, urafikiTubadilishane mawazo kuhusu mahusiano, mapenzi, urafiki, n.k na kushauriana. TAFADHALI: Hii si sehemu ya kuweka picha chafu ama kutumia lugha kali sana. Zitafutwa!
Hey wana Jf,
Katika utamaduni wetu kama waafrika/ watanzania, mwanaume ndio wa kwanza siku zote kueleza hisia zake kwa binti kama anamuhitaji kimahusiano. Hivi sasa imekuwa tofauti kidogo, kuna baadhi ya wasichana wanaanza kueleza hisia zao kwa mvulana/Mwanaume kama anampenda au anahisia nae kimapenzi. Lakini hapa nchini kwetu inaonekana kama vile msichana anayemtaka kimapenzi mwanaume ni muhuni/ mapepe/malaya, majina yote hayo anapewa. Hii tabia ya msichana kumtongoza mwanaume hapa Tanzania kwa sasa bado watu wanaona kama msichana mwenye tabia hiyo ni muhuni au malaya, imekuwa tofauti na developed country hao hii tabia ni ya kawaida tu na wal si ajabu.
Je wewe kama mwanaJF na Mtanzania unalionaje hili, je ni sawa kwa msichana kumtongoza mwanaume? Au bado tubaki na mila/utamaduni wetu wa mwanaume kumtongoza mwanamke?
__________________ "The great pleasure in life is doing what people say you cannot do."
Mara nyingi sana huwa najaribu kujiuliza kama kuna ubaya wwt kwa mtu kuwa muwazi kwa hisia zake,hapa ndipo utata unapokuja hasa ktk suala zima la hisia za mapenzi kwa wanawake kwamba hatuna haki ya kupenda ama kuvutiwa kwa sababu tu ni mwanamke au tuendelee tu kunyamaza kwa kuogopa kuitwa malaya na hatimae tufe na maumivu ya moyo ukisubili huyo unaempenda roho mtakatifu amshukie nae avutiwe nawe ki2 ambacho wakati mwingine ni nadra sana kutokea na maranyingine isitokee kabisa au tufanye nini ili kuwatendea haki wanawake wengi wanaoteseka ktk hili,naomba tusaidiane mawazo wanakijiji.
what i think on this is that we expecially tanzanians men we are very mean, in other contries even kenya women do approch men and it is fair, i think this culture of self expression is good and i ask all women to express what they feel to men, let the man think what he thinks but atleast you have say what you feel