Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mwanamke: Unajua ni kwanini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao?

    Report Post
    Page 1 of 4 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 66
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Mwanamke: Unajua ni kwanini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao?


      Inatokea unapata mtoko na mpenzi mpya na baada ya kubadilishana anuani za mawasiliano zikiwemo zile za mtandaoni unapata tashwishwi ya kuingia katika ukurasa wake wa facebook. Lahaula, huko unakutana na picha kedekede za wanawake warembo hasa na wenye sifa za kugombea mashindano ya ulimbwende.

      Unashikwa na udadisi na siku mnapokutana swali lako la kwaza ni kutaka kujua wale ni akina nani. Na yeye bila ya wasiwasi anakujibu kwamba ni marafiki zake tu wa mtandaoni na wala hajawahi kukutana nao zaidi ya kuwasiliana kwa njia hiyo ya mtandaoni.

      Lakini kama mjuavyo wanawake walivyo, majibu hayo hayaoneshi kumridhisha, hivyo anaendelea kudadisi zaidi ili kujiridhisha, na si ajabu maswali yakawa mengi kulingana na namna majibu yatakavyokuwa.................

      Ukweli ni kwamba ni vigumu kwa mwanamke kupokea majibu mepesi hasa pale linapotokea jambo analolitilia mashaka, ni lazima atahisi kuna kitu kinaendelea..............

      Wakati mwingine inaweza kutokea mwanamke yuko na mpenzi wake wamekaa mahali au wako kwenye mtoko, mara akapita mwanamke, na ghafla akamuona mpenzi wake anageuza shingo na kumkodolea macho, wakati mwingine mwanamke anaweza kupuuza, lakini inaweza kutokea kila anapokatiza mwanamke katika eneo hilo, mwanaume anageuza shingo na kumkodolea macho.................

      Kitendo hicho kinaweza kuibua maswali kutoka kwa mwanamke. Na kama mwanaume asipotoa majibu ya kuridhisha kwamba ni kwa nini macho yake yako juu juu kutazama wanawake, kuna uwezekano wa kuzuka tafrani.

      Hebu ngoja niwamegee siri, sababu inayotufanya tuwe tunawaangalia wanawake hususan wanawake warembo ni kwa sababu wanaume wanapenda kuangalia wanawake warembo. Wanaume huwa tunapenda kuangalia picha za wanawake warembo, senema zinazoonyesha wanawake warembo, mashindano ya ulimbwende yanayoshirikisha wanawake warembo, yaani tumezaliwa na kukuzwa kwa umri na kimo katika mazingira hayo....

      Wanawake, kamwe msidhani kwamba kuwakodolea macho wanawake warembo na labda kutokwa na udenda ndio tunataka kulala nao..... La hasha, tunasafisha kiwi cha macho tu na maisha yanaendelea…………..

      Ni vyema jambo hilo mkalichukulia kama kitu cha kawaida. Kama utakuwa na mpenzi ambaye haangalii wanawake warembo wapitao mbele yake. Bila shaka utakuwa una mpenzi au mume mwenye kasoro.... huyo hatakuwa ni mtu wa kawaida.........!

      Hatuna mawasiliano nao, wala hatufanyi kitu chochote na wao, zaidi ya kuwaangalia tu na kuwaacha kama walivyo, sasa ya nini mpate jakamoyo na kujipa presha.

      Wanaume tunapenda kuangalia wanawake, yaani hilo halina mjadala, inabidi tu mkubaliane na hali halisi kwa hiyo siku nyingine ukimuona mpenzi wako au mumeo anaangalia wanawake warembo wala usijisumbue kugombana naye kwa maswali kwani hali hiyo itamfanya wakati mwingine awe anakandamiza hisia hizo za kuangalia wanawake wengine na kama mjuavyo mtu akikandamiza jambo kwa muda mrefu mwishowe hulipuka na ushawishi wa kwenda mbali zaidi unakuwa ni mkubwa. (kukandamiza maana yake ni kujizuia kwa nguvu zote kufanya jambo au kitu ambacho unatamani sana kukifanya kwa kuhofia kama watu waliokuzunguka watakuonaje, kwa mfano kufanya ngono, kunywa pombe, kuvuta sigara, nk).

      Hivyo basi msije tutoboa na vidole vya macho, kwani mwanaume anapowaangalia wanawake warembo huwa anaishia kuangalia kwa macho tu, lakini moyo wake uko kwako...............LOL

      Last edited by Mtambuzi; 20th August 2012 at 18:16.

    2. Study Abroad

    3. #2
      Purple's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Location : mjini
      Posts : 1,795
      Rep Power : 726
      Likes Received
      607
      Likes Given
      415

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Hata kama ndo mmeumbwa hivyo kwa nini usimuheshimu mpenzi/mke wako japo kwa huo muda ambao upo nae? Hivi kweli umekaa na mpenzi wako halafu unageuza shingo kumsindikiza mwanamke aliyepita kwa macho?tabia mbaya! Muwe mnawaheshimu mlio nao!

    4. #3
      Arabela's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th July 2012
      Posts : 2,256
      Rep Power : 13605
      Likes Received
      1398
      Likes Given
      5

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Kweli si sahihi kukaa na umpendae then ikipita skirt umegeuka eti kwasababu mmeumbwa kuangalia warembo
      Mtambuzi and MadameX like this.

    5. #4
      Kimbweka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th July 2009
      Posts : 7,875
      Rep Power : 7239
      Likes Received
      1281
      Likes Given
      105

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Unajua tunataka kuona kaficha nini hapo juu ya skirt, huwa tunawaza kuna kitu tofauti na cha uliye naye na ukiniachia tu lazima nikachungulie mgodi.....
      Mtambuzi likes this.
      "Life comes once only: No retake/replay/rewind/once-more. One should enjoy it, be happy & keep happy others too."

    6. #5
      Thomas Odera's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Location : Karachuonyo - Kisumu
      Posts : 508
      Rep Power : 534
      Likes Received
      58
      Likes Given
      70

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Ni vigumu kwa binadamu kukubali ukweli laikini kwa hili la wanaume kuwaangalia wanawake wanapokuwa na wenzi wao halina ubishi. Hata wewe mwanamama ukipita na mumeo halafu wanaume wengine wasikuangalia lazima utakuwa na kasoro
      Baba_Enock and Mtambuzi like this.
      Waovu wakitawala maovu huongezeka, lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao. ( Meth 29: 16 )

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      NyotaMalaika's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th August 2012
      Posts : 103
      Rep Power : 361
      Likes Received
      42
      Likes Given
      14

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      loading.....subiri kwanza...
      Mtambuzi likes this.

    9. #7
      jeneneke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2012
      Posts : 705
      Rep Power : 487
      Likes Received
      289
      Likes Given
      263

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Halafu kinachonikera unakuta jianaume linakuangalia kifuani bila hata aibu
      Mtambuzi and MadameX like this.

    10. #8
      mito's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th June 2011
      Posts : 1,028
      Rep Power : 605
      Likes Received
      432
      Likes Given
      1315

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Mtambuzi hii ni ngumu sana kueleweka kwa wanawake. Hii inatokana na ukweli kwamba hata wewe huyo uliye naye kabla ya kumtongoza ulianza kwa kumwangalia kwanza, so it's the way towards.........
      Mtambuzi likes this.
      Haki ya mtu haipotei, inacheleweshwa tu!

    11. #9
      snowhite's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd August 2012
      Location : nyumbani
      Posts : 7,649
      Rep Power : 19921
      Likes Received
      7677
      Likes Given
      7175

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Quote By jeneneke
      Halafu kinachonikera unakuta jianaume linakuangalia kifuani bila hata aibu
      Sasa mnapoacha matiti wazi huku mmeyapaka mafuta yang'ae kabisa mnategema nini?waacheni waangalie!WANAUME ANGALIENI MWAYEGO!
      lakini hata sisi tunawaangalia kwa kijicho pembe bila wenyewe kujua kwa hiyo ngoma droo!
      Mtambuzi likes this.
      IT TAKES A MAN TO CONSTRUCT A HOUSE BUT IT NEEDS A WOMAN TO MAKE A HOME!

    12. #10
      SnowBall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th September 2011
      Location : Amsterdam, Nertherlands
      Posts : 2,628
      Rep Power : 24024
      Likes Received
      2399
      Likes Given
      3298

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Macho yanafanya kile moyo unachoelekeza
      Ni kweli Mtambuzi ni ngumu sana kukutana na demu mkali as mwanaume halaf usimwangalie..
      Kujizuia usiangalie ni kuiumiza nafsi tu..
      Sometimes we should let ourselves listen to our heart!
      Mtambuzi likes this.
      ..''I wasted time, and now those time waste me''...Shakespear

    13. #11
      SnowBall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th September 2011
      Location : Amsterdam, Nertherlands
      Posts : 2,628
      Rep Power : 24024
      Likes Received
      2399
      Likes Given
      3298

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Quote By snowhite
      Sasa mnapoacha matiti wazi huku mmeyapaka mafuta yang'ae kabisa mnategema nini?waacheni waangalie!WANAUME ANGALIENI MWAYEGO!
      lakini hata sisi tunawaangalia kwa kijicho pembe bila wenyewe kujua kwa hiyo ngoma droo!
      duh maskini! umekosa like yangu kwa sababu ya mchina!
      well said either!
      Mtambuzi likes this.
      ..''I wasted time, and now those time waste me''...Shakespear

    14. #12
      matumbo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 9th July 2011
      Posts : 2,321
      Rep Power : 0
      Likes Received
      647
      Likes Given
      485

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Kumwangalia demu mwingine mara nyingi inatokea involuntary...yani wadada haswa wazuri wanakuwa kama wanasumaku vile unajishtukia umekodoa tu mimacho..kama ni demu then ukipita kwa ma-meni alafu wakaushe kama vile ajapita mtu,inabidi ujiulize mara sita sita.
      Mtambuzi likes this.

    15. #13
      jouneGwalu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : Studio
      Posts : 2,340
      Rep Power : 968
      Likes Received
      1311
      Likes Given
      1755

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Ah Bro, ndio umeamua kuja kujitetea kwa stahili hii? Lol......
      Mtambuzi likes this.

    16. #14
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Huu uzi ushaniletea matatizo..............!
      Niliuacha wazi kwa PC yangu na mama Ngina keshauona, nishatwangwa na SMS kali, kabla sijafika home...............
      Nitawasimulia yaliyojiri kesho.

    17. #15
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Quote By jouneGwalu
      Ah Bro, ndio umeamua kuja kujitetea kwa stahili hii? Lol......
      Mie nawatetea wanaume tu, na wala sina mpango huo wa kando........... Duh, na uzee huu.............!

    18. #16
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,531
      Rep Power : 1262
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Quote By Purple
      Hata kama ndo mmeumbwa hivyo kwa nini usimuheshimu mpenzi/mke wako japo kwa huo muda ambao upo nae? Hivi kweli umekaa na mpenzi wako halafu unageuza shingo kumsindikiza mwanamke aliyepita kwa macho?tabia mbaya! Muwe mnawaheshimu mlio nao!
      Nyie mnasema nyie... Kuna wakati uko na mamaa demu anapita
      ana ushape mpaka wife mwenyewe anageuka anaangalia yaani mnakuta wote mnaangalia alafu we unarudisha shingo lakini unakuta bado wife anaangalia ushepu afu akimaliza anaguna.. Jamani kuna vitu vimeumbwa dunia hii msifanye mchezo
      Mtambuzi likes this.
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    19. #17
      jouneGwalu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : Studio
      Posts : 2,340
      Rep Power : 968
      Likes Received
      1311
      Likes Given
      1755

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Quote By Mtambuzi
      Mie nawatetea wanaume tu, na wala sina mpango huo wa kando........... Duh, na uzee huu.............!
      Pamoja Bro....!
      Mashosti wataelewa naamini.
      Mtambuzi likes this.

    20. #18
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2305
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3969

      Default Re: Mwanamke: Unajua ni kwa nini wanaume hupenda kuangalia wanawake hata wawapo na wapenzi wao......

      Kama mie navyopenda kuangalia movie za ma handsome boy tu. (Wapi The Boss.Lol)
      Mtambuzi and christmas like this.

    21. #19
      mopaozi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Posts : 2,446
      Rep Power : 757
      Likes Received
      258
      Likes Given
      49

      Default Reply With Quote


    22. Mtoto halali na hela's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2012
      Location : Himo, Kilimanjaro.
      Posts : 1,887
      Rep Power : 2813
      Likes Received
      461
      Likes Given
      220

      Default

      Quote By jeneneke
      Halafu kinachonikera unakuta jianaume linakuangalia kifuani bila hata aibu
      c unakuta umeacha waz ili kitazamwe?
      Mtambuzi and MCHINESE like this.

    23. Miaka 50
    Page 1 of 4 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...