Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 96
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?


      Kuna jambo ambalo nimekuwa nikijiuliza mara nyingi sana. Nakumbuka katika kipindi changu cha mpito wakati natafuta jiko, nilibahatika kuwa na mitoko (dates) na wadada kadhaa…….. Naam, kipindi hicho nilikuwa katika pilika za kutafuta ni nani atakayenifaa kwa ajili ya kujenga familia.

      Kama mjuavyo mtoko ni gharama na gharama hizi mara nyingi huzibeba mwanaume, ambaye ndiye anayetoa mwaliko. Ni vigumu kutabiri gharama za mtoko na hiyo ni kutokana na kutojua kama mwenzako anapendelea aina gani ya vinywaji au vyakula. Hivyo inabidi kabla ya mtoko basi ujikague kama mfuko unakidhi usije ukaumbuka bure.

      Lakini pia inategemea ni sehemu gani mtakwenda kwa ajili ya mtoko wenu, kwani kila sehemu ina gharama zake. Kwa mfano, kuna kwenda sinema, kuna kutoka kwenda kupata chakula cha jioni na hii inategemea mnakwenda wapi, kwani kuna mighahawa ya inayouza vyakula vya kitalii, kuna hoteli za nyota tatu, nne mpaka tano, maeneo yote hayo yanatofautiana bei, na ndio maana nikasema mtoko ni gharama.

      Swali kwa wanawake:

      Inaweza kutokea baada ya mtoko wa kwanza mwanaume akavutiwa na wewe akiamini kwamba, mnaweza kujenga familia. Lakini ili kufahamiana zaidi akawa anakualika kwenye mtoko mara kwa mara ili mpate fursa ya kufahamiana zaidi.

      Kwa kuwa mara nyingi hutokea wanaume ndio hubeba gharama za mitoko (dates) kwa sababu wao ndio waalikaji, Je mnadhani ni wakati gani mnapaswa kuanza kulipa gharama za mtoko…………?

      Niliwahi kuzungumza na baadhi ya wafanyakazi wenzangu wa jinsia ya kike kuhusu jambo hili. Baadhi walisema wanaweza kutoa mwaliko wa mtoko wa tatu na kubeba gharama. Wengine walisema mtoko wa pili wanaweza kulipa gharama za matumizi ya mtoko huo, hata na kama wao ndio wamealikwa na ikitokea mwanaume analazimisha kulipa, basi watajaribu japo kuchangia gharama za vinywaji. Lakini wapo waliodai kwamba wao wataanza kulipa pale tu ambapo mwanaume huyo ataonyesha dalili zote za kuwavisha pete za uchumba au kufunga nao ndoa…………………..

      Naomba kupata mtazamo wenu juu ya jambo hili, Je nyie mnasemaje?.

    2. Miaka 50

    3. #2
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2306
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3980

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Kibongo Bongo aliyepropose kutoka ndiye anayepaswa kulipa...maana mtu akikwambie twende Serena maanake amejiandaa asitegemee mualikwa atalipa. Lol.

      Wanawake tulivyo bahili...sana sana utaishiwa kualikwa dinner nyumbani kusave budget.

      Kwa experience yangu toka nimemjua baba nanii analipia mitoko yote anayopropose na ninayopropose...kwanza nazani ana enjoy kulipia gharama..si mwanaume bana. ila we have a joint account hivyo it does not matter nani kalipa...ila ni heshima akiendelea ku foot bills mbele za watu.
      BAK, Mtambuzi, mito and 2 others like this.

    4. #3
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By nyumba kubwa
      Kibongo Bongo aliyepropose kutoka ndiye anayepaswa kulipa...maana mtu akikwambie twende Serena maanake amejiandaa asitememee mualikwa atalipa. Lol.

      Wanawake tulivyo bahili...sana sana utaishiwa kualikwa dinner nyumbani kusave budget.
      Duh...!
      nyumba kubwa likes this.

    5. #4
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,618
      Rep Power : 5626
      Likes Received
      6217
      Likes Given
      2308

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Hahahahahaa Mtambuziiiiiiiiiiiiiii loh..... Mie binafsi baada ya ndoa ndo nalipa vidate na hubby, nayo ni pale ninapomwalika out......

      Frankly speaking Kipindi nikiwa single nikikutoa out ujue umeumia ipo siku utagharamia mara tatu ya ninavyotoa hapo, tena bila ya mwenyewe kujua..........loh nashukuru ufisadi huo sina tena siku hizi
      Mtambuzi and nyumba kubwa like this.

    6. #5
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By BADILI TABIA
      Hahahahahaa Mtambuziiiiiiiiiiiiiii loh..... Mie binafsi baada ya ndoa ndo nalipa vidate na hubby, nayo ni pale ninapomwalika out......

      Frankly speaking Kipindi nikiwa single nikikutoa out ujue umeumia ipo siku utagharamia mara tatu ya ninavyotoa hapo, tena bila ya mwenyewe kujua..........loh nashukuru ufisadi huo sina tena siku hizi
      Basi sina haja ya kujuta kumbe wanaume wengi tumeumia katika kipindi hicho cha kutafuta jiko, na wengine huenda mida hii wanaumia ..................LOL
      Nadhani kuna haja sasa mbadilike maana hali ya uchumi imekuwa tete kwa kila mtu.....
      andybird314 likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2306
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3980

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Mi sipendi tabia ya kuomba omba wanaume ela...sijuhi vocha ...sijuhi viatu etc.

      Lakini kimbelembele cha kulipa mkitoka out akyanani kinaweza kumfanya binti adode...kweli vile. Mwanaume wa Kiafrika sidhani kama anapenda kushushwa adharani...na uanaume ni kuhudumia bana.
      Mtambuzi, mito and Neylu like this.

    9. #7
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,444
      Rep Power : 13325
      Likes Received
      7672
      Likes Given
      6911

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Jamani mualikaji si ndio analipa bill?
      Wanaume wengine hawapendi hasa kwa huu mfumo jike unaoanza.

      Ila kiukweli inapendeza mwanaume ndio alipie, naweza compasate kinamna nyingine; kama kununua kitu cha thamani kwa ajili ya nyumbani!

      Raha ya mtoko, hubby atoboke! LOL

    10. #8
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By Kaunga
      Jamani mualikaji si ndio analipa bill?
      Wanaume wengine hawapendi hasa kwa huu mfumo jike unaoanza.

      Ila kiukweli inapendeza mwanaume ndio alipie, naweza compasate kinamna nyingine; kama kununua kitu cha thamani kwa ajili ya nyumbani!

      Raha ya mtoko, hubby atoboke! LOL
      Ni kweli inapendeza mwanaume kulipa lakini ndio iwe ni kila siku........! Hata hakuna kulipa nusu hasara.............?

    11. #9
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,293
      Rep Power : 13091
      Likes Received
      14163
      Likes Given
      15016

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      mie silipii hadi tuambizane uhusiano wetu ni wa kimagaharibi au wa kiafrika?

      Kama ni wa kimagharibi, inayomaanisha nitapata haki zote kulingana na makubaliano ya Beijing, basi kila mtoko nitagharimia nusu kwa nusu.

      Ila kama anataka mahusiano ya kiafrika ambayo mwanamme ana sauti kama kiongozi wa kundi la wanawake anaowaongoza, basi sitalipia asilani.

      Mie hapa huwa naona wanamme wanajikanganya, anataka um-treat kama african king halafu kwenye cost sharing anataka twende kimagharibi, hii haiwezekani na haikubaliki.

    12. #10
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By nyumba kubwa
      Kibongo Bongo aliyepropose kutoka ndiye anayepaswa kulipa...maana mtu akikwambie twende Serena maanake amejiandaa asitegemee mualikwa atalipa. Lol.

      Wanawake tulivyo bahili...sana sana utaishiwa kualikwa dinner nyumbani kusave budget.

      Kwa experience yangu toka nimemjua baba nanii analipia mitoko yote anayopropose na ninayopropose...kwanza nazani ana enjoy kulipia gharama..si mwanaume bana. ila we have a joint account hivyo it does not matter nani kalipa...ila ni heshima akiendelea ku foot bills mbele za watu.
      Halafu ndio imetokea umempeleka binti Hoteli kama Kilimanjaro Grand Hyatt, pale soda tu shilingi 5,000, bado hujasoma menu, ikitokea kaagiza Lobuster, mai weee..........!

    13. #11
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,444
      Rep Power : 13325
      Likes Received
      7672
      Likes Given
      6911

      Default

      Quote By Mtambuzi
      Ni kweli inapendeza mwanaume kulipa lakini ndio iwe ni kila siku........! Hata hakuna kulipa nusu hasara.............?
      Hasara tena Mtambuzi? What is the use of money then?
      Jamani nitachangia kwenye Ada za watoto, ujenzi na maendeleo mengine; lkn mtoko akuuu!
      Mtambuzi and nyumba kubwa like this.

    14. #12
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By Kongosho
      mie silipii hadi tuambizane uhusiano wetu ni wa kimagaharibi au wa kiafrika?

      Kama ni wa kimagharibi, inayomaanisha nitapata haki zote kulingana na makubaliano ya Beijing, basi kila mtoko nitagharimia nusu kwa nusu.

      Ila kama anataka mahusiano ya kiafrika ambayo mwanamme ana sauti kama kiongozi wa kundi la wanawake anaowaongoza, basi sitalipia asilani.

      Mie hapa huwa naona wanamme wanajikanganya, anataka um-treat kama african king halafu kwenye cost sharing anataka twende kimagharibi, hii haiwezekani na haikubaliki.
      Mkuu unatisha, nafurahi sana kusoma comments zako....................
      Kongosho likes this.

    15. #13
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17379

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By Kaunga
      Hasara tena Mtambuzi? What is the use of money then?
      Jamani nitachangia kwenye Ada za watoto, ujenzi na maendeleo mengine; lkn mtoko akuuu!
      Kaunga sasa hapo si mpaka iwe mmefunga ndoa na mnayo familia tayari...! what if jamaa ndio anafanya michakato ya kuelekea kwenye uhusiano kamili ambapo hapo ndipo mitoko inakuwaga kwa sana, ndio utamuachia gharama zote za kila mtoko alipe yeye...... Kumbuka kwamba na wewe unafanya kazi.....?

    16. #14
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2306
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3980

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Tatizo si Binti wala Hotel, ila kiherehere cha kumpeleka sehemu usoweza ku afford, lol.

      Quote By Mtambuzi
      Halafu ndio imetokea umempeleka binti Hoteli kama Kilimanjaro Grand Hyatt, pale soda tu shilingi 5,000, bado hujasoma menu, ikitokea kaagiza Lobuster, mai weee..........!

    17. #15
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6889
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Namkumbuka sana marehemu bibi yangu alivyonihadithia jinsi babu alivyompata . . . !!

    18. #16
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,777
      Rep Power : 27111
      Likes Received
      10116
      Likes Given
      14052

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By nyumba kubwa
      Kibongo Bongo aliyepropose kutoka ndiye anayepaswa kulipa...maana mtu akikwambie twende Serena maanake amejiandaa asitegemee mualikwa atalipa. Lol.

      Wanawake tulivyo bahili...sana sana utaishiwa kualikwa dinner nyumbani kusave budget.

      Kwa experience yangu toka nimemjua baba nanii analipia mitoko yote anayopropose na ninayopropose...kwanza nazani ana enjoy kulipia gharama..si mwanaume bana. ila we have a joint account hivyo it does not matter nani kalipa...ila ni heshima akiendelea ku foot bills mbele za watu.
      sijui nikuite dada ila almost age mates eeh! nyumba kubwa, yaani tutatofautiana padogo sana na mimi.

      miye huwa naona furaha kumtoa hubby na wala sitak aguse mfuko wake and to me this started since we were wachumba. haina maana kwamba halipi no kuna siku tunakwenda analipa na kuna siku tunatoka hata kama kapropose yeye kama niko njema nalipia.

      ila kuna siku nilimshangaa sana srafiki yangu, tumetoka kwenda for fun as families sasa hubbies waka save round kama 5 hivi ilipokuja ya 6 na 7 niasave mimi just kwamba wao waone kuwa hatuko wanawake fenicha lol! shostito alinisema kweli eti hata siku moja usikae ukamlipia mr outing kisa eti akitoka hapo anazo baki nazo anapeleka kwa mwajuma lol! mpaka leo huwa simwelew na niliacha urafiki nae manake nilihofia kulishwa kasa.
      nyumba kubwa and SnowBall like this.
      "thought takes man out of servitude into freedom"
      'daima tudumu katika upendo'

    19. #17
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2306
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3980

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Ndio maana nikasema analipa kwa sababu ya PR tu maana ela yetu tunachanga Lol.
      Ukizingatia tayari niko powerful nsipojishusha kwenye kadamnsasi kwa mila za kiafrika mume anaweza kudharauliwa. Lol.


      Quote By gfsonwin
      sijui nikuite dada ila almost age mates eeh! nyumba kubwa, yaani tutatofautiana padogo sana na mimi.

      miye huwa naona furaha kumtoa hubby na wala sitak aguse mfuko wake and to me this started since we were wachumba. haina maana kwamba halipi no kuna siku tunakwenda analipa na kuna siku tunatoka hata kama kapropose yeye kama niko njema nalipia.

      ila kuna siku nilimshangaa sana srafiki yangu, tumetoka kwenda for fun as families sasa hubbies waka save round kama 5 hivi ilipokuja ya 6 na 7 niasave mimi just kwamba wao waone kuwa hatuko wanawake fenicha lol! shostito alinisema kweli eti hata siku moja usikae ukamlipia mr outing kisa eti akitoka hapo anazo baki nazo anapeleka kwa mwajuma lol! mpaka leo huwa simwelew na niliacha urafiki nae manake nilihofia kulishwa kasa.
      gfsonwin likes this.

    20. #18
      Neylu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2012
      Posts : 1,495
      Rep Power : 651
      Likes Received
      632
      Likes Given
      617

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Mmmh... Mtambuzi umenikumbusha mbali kidogo.... Nilikuwa na mpenzi wangu, mara nyingi tukitoka out mie ndie nilikuwa nalipa gharama zooote kisa, nilikuwa nampenda hata sikutaka aingie gharama za aina yeyote... Alivyokuja kunitenda nikapata somo.... Mimi kulipa gharama za outing kwa boyfriend sijui mpenzi, mchumba ni MARUFUKU!! Mpaka hapo nitakapokuwa wake rasmi ( Ndoa) hapo ndio nitagharamia outing..
      We must either find a way or make one. - Hannibal

    21. #19
      gfsonwin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th April 2012
      Posts : 10,777
      Rep Power : 27111
      Likes Received
      10116
      Likes Given
      14052

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      Quote By Kongosho
      mie silipii hadi tuambizane uhusiano wetu ni wa kimagaharibi au wa kiafrika?

      Kama ni wa kimagharibi, inayomaanisha nitapata haki zote kulingana na makubaliano ya Beijing, basi kila mtoko nitagharimia nusu kwa nusu.

      Ila kama anataka mahusiano ya kiafrika ambayo mwanamme ana sauti kama kiongozi wa kundi la wanawake anaowaongoza, basi sitalipia asilani.

      Mie hapa huwa naona wanamme wanajikanganya, anataka um-treat kama african king halafu kwenye cost sharing anataka twende kimagharibi, hii haiwezekani na haikubaliki.
      i bet to differ with you ma honey hivi kweli, hata kama mmedefine uwe ni wa kiafrika hivi utakuwa mnyimi kisa the man wants to be treated like african king? hii naona haijakaa vyema kwangu.

      btw mimi huwa nauamini sana mfuko wangu aisee manake kama hauko poa hata uniambie tutoke nachomoa lol!, kama vipi tupige stail ya kila mtu anunue kinywaji chake but tutashare sigara tu.
      Kongosho likes this.
      "thought takes man out of servitude into freedom"
      'daima tudumu katika upendo'

    22. #20
      telitaibi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd May 2012
      Posts : 459
      Rep Power : 447
      Likes Received
      83
      Likes Given
      79

      Default Re: Wanawake: Ni wakati gani mnadhani ni muafaka kuanza kulipa gharama za mtoko (dates)........?

      hapa napo pagumu jamani, so dad nani akiwa mtupu hatutoki tena? ila kuna wanaume ukianza kugaramia mtoko basi ndo umekuwa mtumwa kila akitoka atajichekelesha ulipe wewe wakati nyumba ndogo na matusi juu atapewa kwa kushindwa kulipa mi na wanaume lo siwapendi kwani hawajitambui hukawi kusikia akikuita shuga mami.

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...