Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 47
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,182
      Rep Power : 27036
      Likes Received
      8457
      Likes Given
      17777

      Default Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!


      Hii picha haihusiani na habari hii.....................

      Inaniumiza
      sana kuikumbuka, hasa kuisimulia, lakini nimeambiwa kuwa, kwa kusema jambo hili wazi, naweza kupata nafuu. Hata hivyo naamini nitapata thawabu kwa kuwasaidia wengine kujua tatizo na kuweza kuliepuka wakimudu. Mimi na mke wangu tulioana mwaka 1974 jijini Dar es salaam, mimi nikiwa na miaka 32 na yeye akiwa na miaka 24 wakati huo. Mke wangu ni mwenyeji wa Iringa na mimi ni mwenyeji wa Lushoto, mkoani Tanga. Tulikutana hapa Dar es salaam, mimi nikiwa mfanyabiashara naye akiwa amemaliza kozi ya ualimu daraja ‘A’ akisubiri kwenda kufundisha.

      Tulianza uhusiano na alipopangiwa kituo cha kazi Kyela, nilimwambia asiende. Alisema ni lazima aende akaonje ualimu ambao aliusomea kwa miaka miwili. Alikwenda, lakini baada ya miezi sita alirudi akidai hawezi. Nilimwomba aache ualimu na kufanya biashara. Tulikubaliana. Tulioana wakati huohuo na kuanza maisha ya mke na mume. Tulikuwa tukiishi Mburahati wakati huo, ambapo baadae hata hivyo tulihamia Sinza. Tulikaa kwa miaka mitatu bila mke wangu kupata ujauzito. Ndugu walianza maneno na mke wangu alianza kubabaika. Nilimtuliza na kumwambia, angekuja tu kupata ujauzito.

      Hadi mwaka 1980 yaani miaka sita baadae, mke wangu alikuwa bado hajapata ujauzito. Ndugu zangu walianza kelele na vurugu za kila aina, wakidai nioe mke mwingine. Nilipuuzia maneno yao, ingawa yalianza kuniingia kidogokidogo. Mwaka 1981 niliwaza njia ambayo niliona ingesaidia kuondoa kero zote. Nilimwambia mke wangu afunge maguo tumboni na kuonekana kama ana ujauzito. Aliponiuliza sababu , nilimwambia afanye tu hivyo. Alibishabisha awali, lakini nilipomuuliza kama haniamini, aliamua kunikubalia ombi langu.

      Alipovaa maguo hayo na kuonekana kama mwenye ujauzito nilianza kutangaza kwamba mke wangu ni mjamzito. Nilitangaza kwa ndugu, jirani na hata kwa jamaa zangu wa karibu. Ilipofika miezi saba baada ya kutangaza hivyo nilimwambia mke wangu ni muda mzuri sasa wa kuaga kwamba anaenda kwao. Nilikuwa wakati wote huo nahangaika kutafuta namna ya nitakavyoweza kuwezesha kile nilichokuwa nimekibuni. Ni kweli aliondoka kwenda kwao. Wiki ile ile aliyoondoka, nilifanikiwa kupata nilichokuwa nataka.

      Nilikuwa nimezungumza na wahusika wengi sana wa maeneo mbalimbali ambao wangeweza kunipatia mtoto mchanga. Mama mmoja ambaye naomba nisimtaje jina alipata mtoto mchanga. Mtoto huyo alikuwa amezaliwa hospitalini {naomba nisiitaje} na mama yake akafariki. Hakutokea mtu kumdai mtoto, wala maiti ya mama yake na huyo mama alijifanya ni ndugu wa marehemu, mara tu alipofariki. Kwa kutumia fedha kidogo nilizokuwa nimempa aliruhusiwa kumchukua mtoto yule akamlee. Ukweli ni kwamba hakuna ndugu wa yule msichana aliyejitokeza hapo hospitalini………….

      Kwa kusindikizana na mama huyu, tulisafiri kwenda Iringa kwa mke wangu. Mke wangu hakuwa ameenda kuishi kijijini bali alikuwa akikaa hotelini, pale Iringa mjini. Tulipofika pale hotelini, nilimkabidhi mke wangu kachanga kale nakusema ni kake kuanzia wakati ule. Kalikuwa ni katoto ka kike kazuri. Kwa mara ya kwanza mke wangu alijua mpango wangu. Ilibidi niondoke na mke wangu kwenda naye kijijini kwao, ambapo tulipofika tuliwaambia alikuwa amejifungua njiani. Nilimwacha kule na kurudi Dar es salaam, kutangaza kwamba mke wangu amejifungua mtoto wa kike. Siwezi kusema furaha iliyokuwepo kwa ndugu zangu na wa mke wangu. Tukawa wanandoa wenye mtoto mmoja kwa njia hiyo.

      Mwaka 1987 ndipo tulipoanza kushangazwa na binti huyu, akiwa na miaka sita wakati huo. Kwanza, alikuwa ni binti mkatili sana, tangu akiwa mdogo tu wa miaka mitatu. Alikuwa anapenda sana kukwangua wengine tukiwemo sisi. alipoanza kuzungumza, alikuwa akizungumza maneno ya ajabu, lakini ya kutisha pia. Mara nyingi alikuwa akipenda sana kutaja kufa, kuumwa na nyoka, kupanda mlimani, kufukiwa gizani na mengine ya aina hiyo. Alikuwa akipenda sana kusikiliza kwa makini watu wanapokuwa wakizungumzia mambo ya uasi kuliko mambo mazuri. Hii tabia tuliigundua alipokuwa na miaka mitano.

      Akiwa na miaka sita, tukio la kwanza lililotushtua ni lile la kumwambia mama yake, hana adabu, alimwambia hivyo kufuatia kumwambia , akinywa chai awe anaondoa kikombe chake mezani na kukipeleka jikoni. Mama yake alimchapa. Kwa kawaida mtoto wa miaka sita akichapwa, mtu anategema akiona akilia. Huyu hakulia, bali alimwangalia tu mama yake vibaya na kuondoka. Siyo siri, niliogopa sana. Mwaka 1994 alipokuwa darasa la saba alifanya vituko vingi sana na tulihangaika sana kutafuta suluhu. Ili kupunguza maumivu, tuliamua kumpeleka shule ya sekondari ya bweni mikoani. Tulimpeleka. Lakini hata mwezi haukuisha alikuwa amerudishwa kutokana na kushindikana.

      Alikuwa na kila aina ya visa. Alikuwa akitukana waalimu, kupiga wanafunzi wenzie na kuanzisha vurugu za aina mbalimbali. Ajabu ni kwamba, ukiwa umekaa naye na kuzungumza naye, anakuwa mtoto mzuri na msikivu sana. Anaweza hata kulia, kujutia makosa yake. Lakini baada ya hapo ndio anakuwa ametiwa moto. Kwa mwaka mmoja wa kidato cha kwanza, tulimbadilisha shule kiasi cha sita. Alipoingia kidato cha pili ndio vurugu zikawa kubwa zaidi. Lakini sasa hapa akawa ameanza tabia za uhuni, yaani kushiriki ngono.

      Hali hii ya kupenda kushiriki mapenzi ilitukera sana na tulijua kwamba tumeshapoteza mtoto tayari. Lakini katikati ya tatizo hili, likazuka lingine. Hili ndilo lilikuwa kubwa zaidi. Alikuwa mara nyingi akidai kwamba ana hamu na mama yake. Tulipokuwa tukimwambia kwamba mama yake yupo hapo nyumbani, yaani mke wangu, alikuwa akisema hana uhakika sana kama hadanganywi. Kusikia hivyo, nilijua yule mama aliyenisaidia kumpata alikuwa amemwambia siri yote. Nilipomwendea na kumuuliza alisema asingeweza. Lakini alisema hata mama yake halisi na yule mtoto, kabla hajafa alikuwa akiropoka mambo mengi makubwa na ya kutisha. Ilibidi sasa niombe ushauri kwa watu mbalimbali, kuanzia kwa mashehe, mapadri, waganga na madaktari, lakini hakuna kilichobadilika.

      Kila mmoja alijaribu kumsaidia kwa namna yake lakini, bila mafanikio. Pamoja na Vituko vyake na kauli za kutisha, hasa hizo za kumtaka mama yake na kusema anahisi haambiwi kweli, bila kufafanua, alimaliza kidato cha nne mwaka 1999. Wakati huo alikuwa anaumwa
      sana hata hivyo. Tulijaribu kumsaidia sana kwa matibabu na kumtunza.

      Tulikuwa tunampenda sana pamoja na visa na vituko vyake. Mwaka 2000 alizidiwa sana na maradhi na tulilazimika kumfanyia vipimo zaidi na alibainika kwamba ameathirika kwa ukimwi. Hatukumpa matokeo ya vipimo hivi awali,lakini alitushangaza aliposema, 'mnanificha kitu gani, siogopi kama mnavyofikiria. Kwani mtu kwenda kuungana na mama yake kuna tatizo?' Kwa kuwa nilishamzoea kwa visa vingi lukuki, sikustuka sana, ingawa mke wangu alishtuka kupindukia.

      Mwaka 2001 alizidiwa kabisa na sasa alikuwa akikaa nyumbani tu. Siku moja mwezi wa Juni aliomba apewe jina la ukoo wa mama yake, kabla hajafa. Hapo tuliogopa vizuri sana kwa kweli na siwezi kuisahau siku hiyo. Tulimpa jina la ukoo wa kwa mke wangu, alikasirika sana na kusema anataka jina la ukoo wa kwao. Alisema akifa bila jina hilo, mambo yasiyopendeza yangetokea na kwamba asingepaswa kulaumiwa kwa hilo, kwani kazi tuliyofanya ingekuwa imepotea bure.

      Tuliogopa sana na ilibidi niende kwa yule mama aliyenifanyia mpango wa kumpata binti huyu na nilizungumza naye. Alisema, ingekuwa ni vigumu kwake kupata taarifa za yule mama yake. Lakini kwa bahati alikumbuka jina na ubini na kwamba, yule mama alimwambia alikuwa ametokea kijiji cha Puge, Nzega, Tabora. Alimwambia alifika Dar es salaam kwa kudanganywa na mtu ambaye alimleta Dar na kumtelekeza baada ya ujauzito.

      Nililazimika kusafiri hadi huko Puge, nilipofika hapo kijijini {Ni kijiji lakini ni
      kama kamji kadogo} nilidadisi na kupata taarifa kumhusu yule mama. Sikusema chochote, zaidi ya kurejea Dar es salaam. Nilivyoambiwa kule ni kwamba, yule mama wa mtoto wetu alikuwa apewe kitu walichoita Mkoba {Uganga bila shaka} ya bibi yake mzaa baba, lakini akakataa na kukimbilia kusikijulikana.

      Huku Dar es salaam alikuja mwenyewe na kukutana na huyo tapeli aliyempa ujauzito. Inaelezwa kwamba, bibi yake alikufa akiwa hajakabidhi mikoba ya uganga kwa yeyote. Hayo niliyaamini ingawa kabla ya tukio hili, kama ungenitajia jambo kama hilo, ningekutemea. Nilirudi Dar na nilipofika nyumbani, hali ya binti yetu ilikuwa mbaya sana. Nilimsalimia na kumwambia kwamba tunampa jina {Naomba nisilitaje}. Aliposikia jina hilo aliinua kichwa, jambo ambalo alikuwa hajawahi kulifanya tangu kuzidiwa kwake na ugonjwa.

      Halafu alirudisha kichwa kwenye mto na kufariki hapohapo. Naomba uniamini kwa faida yako, kwani hilo, lilitokea mbele ya macho yangu. Sioni faida ambayo mimi au wewe utaipata kwa uongo ambao nitaufanya katika suala hili. Mwaka huo huo akiwa na miaka 41 mke wangu alijifungua mtoto wa kike. Ilikuwa kama ajabu kwetu na mshangao huo hauwezi kututoka hata siku moja. Lakini hata kama atakuja mtu gani tukubali kuwa hakuna miujiza na nguvu za ajabu kwenye maisha, tutambishia hata kwa thamani ya damu yetu, kwa sababu tumeona kwa macho yetu.

      Mimi na mke wangu tumeumizwa sana na kilichotokea na hasa matukio ya yule binti yetu ambaye tulimlea kwa upendo. Tumekuwa tukijiuliza kilichotokea bila kupata jibu.
      Last edited by Mtambuzi; 7th August 2012 at 12:08.


    2. #2
      cmoney's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2011
      Posts : 374
      Rep Power : 462
      Likes Received
      74
      Likes Given
      56

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Duh.....ebana sijui ubarikiwe au uende kanisani kupata maombezi..sema hongera mzee hii stori inafaa kuwekwa kwe shuhuda za makanisani..
      Mtambuzi likes this.

    3. #3
      Nambe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2011
      Location : Kwa Bi Nyau
      Posts : 835
      Rep Power : 594
      Likes Received
      264
      Likes Given
      260

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      duh, yaan mpaka mwili umenisisimka, dah ila nampongeza hy baba alikuwa na mapenz ya dhat kwa mke wake

      Wakati mwingine ndg, majiran marafiki na jamii kwa ujumla wanaweza kutufikisha kufanya maamuz ajab sana

      hope wengine wanajifunza ki2 kwenye story hii
      Mtambuzi and sakapal like this.
      Happiness is not a reward it is a consequence









    4. SMU is offline
      SMU
      #4
      SMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th February 2008
      Location : Mavurunza
      Posts : 4,604
      Rep Power : 3828
      Likes Received
      1350
      Likes Given
      1987

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Inatisha!
      Mtambuzi likes this.
      "Rather than love, than money, than fame, give me truth" ----Thoreau

    5. #5
      SURUMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2011
      Posts : 1,577
      Rep Power : 733
      Likes Received
      382
      Likes Given
      485

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Duu Mtambuzi hii kitu imenistua sana!!! Kweli maishani kabla hujafa hujaijua sawasawa!!!!!

      Shukuru MUNGU kama binti yenu mliyepata anaendelea vizuri na shikeni sana MAISHA YAFUATAYO NJIA SAFI ZA MUNGU
      Mtambuzi likes this.


    6. #6
      SnowBall's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th September 2011
      Location : Amsterdam, Nertherlands
      Posts : 2,628
      Rep Power : 24029
      Likes Received
      2400
      Likes Given
      3298

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Mtambuzi nitakuwa wa mwisho kuamini hii stori..lol!
      Mtambuzi likes this.
      ..''I wasted time, and now those time waste me''...Shakespear

    7. #7
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,182
      Rep Power : 27036
      Likes Received
      8457
      Likes Given
      17777

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Quote By SnowBall View Post
      Mtambuzi nitakuwa wa mwisho kuamini hii stori..lol!
      Haya bwana......................... ..........!
      SnowBall likes this.

    8. #8
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,182
      Rep Power : 27036
      Likes Received
      8457
      Likes Given
      17777

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Quote By SURUMA View Post
      Duu Mtambuzi hii kitu imenistua sana!!! Kweli maishani kabla hujafa hujaijua sawasawa!!!!!

      Shukuru MUNGU kama binti yenu mliyepata anaendelea vizuri na shikeni sana MAISHA YAFUATAYO NJIA SAFI ZA MUNGU
      Hii hainihusu mimi mkuu.................

    9. #9
      pointers's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2011
      Location : DAR
      Posts : 729
      Rep Power : 561
      Likes Received
      62
      Likes Given
      117

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      kweli hii ni changamoto kali sana kwenye maisha kwa kweli............unaweza ukapata kichaa bure
      Mtambuzi likes this.

    10. #10
      PetCash's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th March 2012
      Location : searching....
      Posts : 642
      Rep Power : 562
      Likes Received
      351
      Likes Given
      104

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Interesting- And I'm speechless!
      Mtambuzi likes this.
      You are what you eat

    11. #11
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,643
      Rep Power : 1230
      Likes Received
      1553
      Likes Given
      1026

      Default re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Duu hii jaijakaa vizuri sana, Duniani kuna mambo
      Mtambuzi likes this.
      Haiwezekani Kabisa Twiga kupakiwa ndani ya ndege tayari kupelekwa nje ya nchi bila Polisi na Usalama wa Taifa kujua....

    12. #12
      Katufu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th May 2012
      Posts : 187
      Rep Power : 396
      Likes Received
      77
      Likes Given
      7

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Hizo ni nguvu za giza ungepata akili ya kumpeleka kwa watumishi wa Mungu kama Kakobe na wengine matatizi yangeisha na sasa hivi ungekuwa na binti yako. Ila baadae ingebidi utubu na kumweleza ukweli
      Mtambuzi likes this.

    13. #13
      Kaunga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Wild wild west
      Posts : 8,725
      Rep Power : 13386
      Likes Received
      8056
      Likes Given
      7426

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      I am glad haikuhusu wewe, naweza iamini kwani nimejifunza there is a lot going on kwenye hii ardhi. The fact kwamba hujashuhudia does not mean kuwa hayapo.

      Kuna issue imetokea recently hapa Kigoma,
      Anakuja mdada nyumbani kwako, na kujiintroduce as a distance relative na kukutajia maisha yako na ya watu wako wa karibu wote (anavaa uhusika kisawa sawa), anakaa siku kama mbili halafu anaondoka na mtoto wako wa kike less than 2 yrs. Baada ya muda (hadi miezi) unakuja mpata wilaya au mtaa mwingine kabisa unharmed.

      Amefanya hivyo kwa familia moja ninayo ifahamu, over the course ya kuhangaika wakakuta hiyo story kwa watu wengine kama 6 hivi (police kituo cha mjini Kigoma wanaifahamu). Huyo dada anajulikana kwao kama Kabula (jini Kabula), na inasemekana anawapeleka hao mabinti ziwani God knows nini kinafanyika huko.

      Kwa kweli mambo mengine yanatisha sana, usiombe kukutana nayo!
      Mtambuzi, Lokissa and gfsonwin like this.
      ..........When you run out of rope; grab onto faith.......... T.B Joshua

    14. #14
      NATA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2007
      Posts : 4,258
      Rep Power : 8420
      Likes Received
      1135
      Likes Given
      390

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Mh kwa kweli huyo baba alinifurahisha sana kwa jinsi alivyokuwa na upendo na mkewe.
      Mh PIA YAWEZEKANA huyu baba alijijua yeye ndiye mwenye mapungufu so kumtema mkewe isingekuwa suluhisho na ndio maana alifight kufunika kombe.

      Mh now a new baby girl!
      Mtambuzi and sausage like this.

    15. #15
      NATA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2007
      Posts : 4,258
      Rep Power : 8420
      Likes Received
      1135
      Likes Given
      390

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Quote By Kaunga View Post
      I am glad haikuhusu wewe, naweza iamini kwani nimejifunza there is a lot going on kwenye hii ardhi. The fact kwamba hujashuhudia does not mean kuwa hayapo.

      Kuna issue imetokea recently hapa Kigoma,
      Anakuja mdada nyumbani kwako, na kujiintroduce as a distance relative na kukutajia maisha yako na ya watu wako wa karibu wote (anavaa uhusika kisawa sawa), anakaa siku kama mbili halafu anaondoka na mtoto wako wa kike less than 2 yrs. Baada ya muda (hadi miezi) unakuja mpata wilaya au mtaa mwingine kabisa unharmed.

      Amefanya hivyo kwa familia moja ninayo ifahamu, over the course ya kuhangaika wakakuta hiyo story kwa watu wengine kama 6 hivi (police kituo cha mjini Kigoma wanaifahamu). Huyo dada anajulikana kwao kama Kabula (jini Kabula), na inasemekana anawapeleka hao mabinti ziwani God knows nini kinafanyika huko.

      Kwa kweli mambo mengine yanatisha sana, usiombe kukutana nayo!
      Makubwa haya tena!
      Kaunga likes this.

    16. #16
      BornTown's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2008
      Location : ???
      Posts : 1,484
      Rep Power : 867
      Likes Received
      283
      Likes Given
      104

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      mwili wote umenisismka! hapo ndipo unaamini kuwa hakuna linalomshinda mungu baada ya mateso na tabu zote mlizopitia hatimae amewafuta machozi na jasho lenu..."kweli nani kama yeye aliye juu...sifa na shukrani apewe mungu"
      Mtambuzi and nemic4u like this.
      "DONT BE A WOMAN THAT NEEDS A MAN BE A WOMAN A MAN NEEDS!!!!"

    17. #17
      WALIMWEUSI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2011
      Location : DSM
      Posts : 1,000
      Rep Power : 585
      Likes Received
      297
      Likes Given
      375

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Quote By SnowBall View Post
      Mtambuzi nitakuwa wa mwisho kuamini hii stori..lol!
      SnowBall naamini hii story ila nitakuwa wa mwisho baada yako kuamini kama ilimtokea Mtambuzi, nilishasikia ushuhuda huu kwenye redio fulani ya kidini mkoani Arusha
      Mtambuzi likes this.
      The best mind-ultering drug is truth.

    18. #18
      Ngongoseke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Posts : 1,171
      Rep Power : 611
      Likes Received
      279
      Likes Given
      238

      Default

      Mtambuzi hii story nimewahi kuisoma kama sio marehem munga basi kwenye blog yako'hongera sana kwa kutunza kumbukumbu za marehem munga'na vile visa jinsi nilivyofedheheka unavyo?
      Mtambuzi likes this.

    19. #19
      Nivea's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 5,986
      Rep Power : 16312
      Likes Received
      3401
      Likes Given
      4347

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      Mtambuzi dunia hii iache kama ilivyo baba macho yetu huona pafupi sana sana nasikiaga huko njiani tunatembea ila tunapishana na watu tusiowaona du huwezi jua ila afadhali alikufa angefunua masiri yasiofunulika maana kimbembe kingerudi kwa yule dada du!
      Mtambuzi likes this.

    20. #20
      Triple G's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2011
      Posts : 327
      Rep Power : 1187
      Likes Received
      70
      Likes Given
      7

      Default Re: Binti aliyeitoa jasho familia kwa visa....!

      mkuu inatisha sana.daah poleni sana.
      Mtambuzi likes this.

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...