Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

    Report Post
    Results 1 to 9 of 9
    1. #1
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,205
      Rep Power : 19214
      Likes Received
      8165
      Likes Given
      26639

      Thumbs up Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      UNAHISI mwenzi wako anakusaliti kwa maana kwamba anafanya ngono na wanawake au wanaume wengine? Fahamu kuwa wapo wengi wenye kulalamikia hilo.

      Kuna baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza kwanini hasa anatoka na wengine ikiwa aliahidi kwamba atakuwa ananipenda milele? Wengine wanakwenda mbali zaidi na kufikiri kila kitu ambacho anakifanya kwa mwenzi wake kitakuwa ni chenye kumpendeza mwingine.


      “Mimi najitahidi kumfanyia mambo mengi mazuri, bado anaonekana haridhiki,” ndivyo baadhi ya watu wanavyojisemea.

      UKWELI UKOJE?: Ni vizuri katika mapenzi kupata muda wa kuzungumza mwenzangu unapendelea nini na usingependa ufanyiwe nini.

      KUAMINI KUWA UNAYOFANYA NI MAZURI, BILA KUAMBIWA NA UNAYEMFANYIA, SIO SAHIHI.
      Maisha ya raha katika uhusiano ni kuhakikisha kunakuwa na fursa ya wapendanao kukaa na kujadili namna gani wamekuwa wakiishi na nini cha kufanya ili waweze kuwa na maisha bora zaidi.


      KUKWAZANA NI MAMBO YA KAWAIDA KATIKA MAPENZI. IKIWA UMEKAA KWENYE TUMBO LA MAMA YAKO NA BADO KUNA WAKATI MNAKWAZANA, IWE MTU AMBAYE MMEKUTANA TU MITAANI?
Jambo muhimu katika ndoa ni kuhakikisha kunakuwa na nafasi ya wanandoa kujadili hali ya ndoa yao.


      Kama ilivyo katika biashara kwamba wafanyabiashara wakati fulani wanajadili hali ya maendeleo ya biashara ili kujua kama kuna matatizo gani nk, ni muhimu sana wanandoa kutenga muda wa kujadili hali ya uhusiano wao.

      SABABU ZA WATU KUSALITI
Wakati fulani nimekuwa nikiongea na watu wanaosaliti ndoa...baadhi yao ukiwauliza unaonaje sasa ukaondoa

      kwenye ndoa na kuoana na huyo wa nje, jibu ni kwamba hawezi kwa sababu anasaliti si kwa sababu hampendi aliyenaye, bali wakati mwingine ni kutofautiana.


      Kwa mfano katika utafiti wangu nimegundua kwamba idadi kubwa ya wanandoa waume, hawana uhakika wa kupata tendo la ndoa kwa wakati wanaotaka, kama ilivyo kwa baadhi ya wanawake.


      Tafiti ambazo nimekuwa nikifanya pia nimegundua kuna tofauti ya mahitaji katika ndoa, kwa mfano wakati wanaume ni wenye kuhitaji mno tendo la ndoa, furaha ya wanawake walio wengi sio hilo wakati fulani ni uhakika wa kupatikana kwa mahitaji ya ndani na amani.


      *Kutopata mapenzi ya kweli katika ndoa hasa ikiwa Kijana/Binti alilazimishwa kuoa/kuolewa na mtu ambaye hakumpenda.
-Wengine

      hawapata mapenzi ya kweli kwa sababu tu mwanaume au mwanamke hamjali, kitendo ambacho kinasababisha baadhi yao kuona kwamba suluhu pekee ni kwenda nje ya ndoa.


      *Uchafu, kutojijali au kujipenda kwa mwanaume na mwanamke
-Wapo wanaume na wanawake ambao wamekuwa wachafu wa mwili na kutojipenda, kiasi kwamba ukiwa nae unahisi kichefuchefu. Kuna wanaume na wanawake kwa mfano wanalala bila kuoga, wengine unakuta

      mwingine mlevi, mwingine hanywi, kisha anarudi nyumbani anaomba abusiwe...mhh! raha iko wapi hapa?

      *Kutotosheka/kuridhika katika tendo la ndoa

      -Ingawa wakati mwingine huwa ni uroho wa mtu, mara nyingi hata majumbani watoto kama hawajashiba, baadhi yao hukimbilia kudowea chakula kwa jirani.


      *Ubize wa kazi kupita kiasi/Kusafiri 
-Kuna watu wako bize kila kukicha, wakati mwingine si kweli kwamba wako bize bali ni unafiki au labda kutojua namna ya kupangilia mambo. Wengine ni watu wa safari kila mara, hiyo ni mbaya kwa wanandoa.


      *Tamaa ya mali: Kuna wengine wako tayari kufanya ngono hovyo ili wapate mali. Huu ni ujinga, badala ya mtu kufanya kazi, anafikiri kwamba njia rahisi ni kubabaikia wanaume wenye magari, wenye fedha nk.


      *Kujifunza mambo au mitindo mipya 
-Wakati mwingine kuna wengine wanatoka nje ili kusaka miondoka mipya...kuna wengine wamekuwa waoga wa kusema ukweli kwa wenzi wao juu ya yale ambayo wanayataka, matokeo yake wanaona wafanye hiyo ‘dawa mbadala’.


      *Kutopata tendo la ndoa muda mrefu, labda kwa sababu mume ana matatizo au mke ana uja uzito mkubwa ama amejifungua n.k
-Hata hivyo kitaalam kuna njia za kuridhishana si lazima tendo la ndoa la aina moja, bali wapenzi wanaweza kuchezeana na kila kitu kikawa chenye kuwafurahisha wote au kumfanya mwenzi wake afurahie.
      MAGISAC and kapistrano like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    2. Miaka 50

    3. #2
      jeneneke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2012
      Posts : 714
      Rep Power : 489
      Likes Received
      297
      Likes Given
      269

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      ndefu ntasomae usingizi ukiisha

    4. #3
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,525
      Rep Power : 1798
      Likes Received
      655
      Likes Given
      0

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      Wivu katika mapenzi ni ugonjwa mpana sana na hauna dawa halisia,na hisia ni mbaya unaweza ukapata ugonjwa wa moyo kama hutajiangalia na ku control hisia zinazoendana na wivu!!!

    5. #4
      Purple's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Location : mjini
      Posts : 1,795
      Rep Power : 727
      Likes Received
      607
      Likes Given
      415

      Default §§

      Well said MziziMkavu...Lakini nionavyo mie TAMAA is the source of all evils, waweza kuta mke/mume anampenda mwenza wake,anamjali,walioana kwa mapenzi yao bila kulazimishwa na mtu lakini baada ya miezi kadhaa au mwaka mmoja wanaanza kucheat. Nilishawahi kushuhudia familia flani mke anamjali mume kiasi kwamba hata usiku anaamka kumchemshia maziwa kama mtoto lakini mume alikua hashikiki mtaani. Kuna wengine ni tabia yao tu, hawezi kutulia na partner mmoja na watu wa namna hii hata ufanyeje hua hawabadiliki. Kumridhisha binadamu ni kazi ngumu sana.

    6. #5
      Sizinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2007
      Location : Mars
      Posts : 3,949
      Rep Power : 1434
      Likes Received
      1512
      Likes Given
      1619

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      Hii dunia hii...waliiweza akina Abrahamu tu...
      GESI KWANZA KOROSHO BAADAE!!

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      mdida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2011
      Location : Middle East
      Posts : 442
      Rep Power : 486
      Likes Received
      198
      Likes Given
      97

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      okay! nionavyo mie kuna haya mazoea katika wapenzi au mume/mke, yale ulokuwa unamfanyia wakati mkiwa gf & bf mkishaona kama alikuwa anakubusu kabla hajaenda kazini basi anapuuza na kuacha, mke pia kama alikuwa na kawaida ya kupiga goti wakati wa kukaribisha chakula mezani sasa ataanza hivi: chakula kipo mezani tayari, n.k so kuna vitu mke/mume wanaona ni vidogo au wanavipuuza ila vinadumisha mapenzi.

    9. #7
      Asabaya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2012
      Posts : 619
      Rep Power : 490
      Likes Received
      127
      Likes Given
      21

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      Ntairejea baada ya Iftar.....hii ukisoma lazima uwe unatafuna kaimati...

    10. kbz
      #8
      kbz's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th July 2012
      Posts : 20
      Rep Power : 349
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      Mi nijuavyo ni hulka ya mtu mwenyewe

    11. #9
      MAGISAC's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th September 2011
      Posts : 96
      Rep Power : 409
      Likes Received
      25
      Likes Given
      47

      Default Re: Sababu za watu kusaliti katika mapenzi

      Kweli kumridhisha mtu ni kazi sana.Sometimes unaweza juta kwa nini uliingia kwenye ndoa.
      SG8 likes this.

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...