Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

    Report Post
    Results 1 to 13 of 13
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,098
      Rep Power : 27015
      Likes Received
      8249
      Likes Given
      17377

      Default Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?


      Kama mvi ni kipimo cha busara.......... Kwa nini zifichwe?

      Kwa zamani ingekuwa ni muhali mkubwa mtu kuuliza swali la aina hii, kwa sababu mvi zinahesabiwa kama dalili ya busara, bila shaka zikihusianishwa na kuona mengi ambayo ni wenye umri mkubwa tu waliokuwa na nafasi hiyo. Lakini leo, mvi ni kisirani na karibu kila mtu anajaribu kuzikimbia, kwani kuendalea kuwa kijana ni sifa kubwa. Kwa sasa uzee unanuka na kila mmoja anajaribu kuukimbia kwa njia mbalimbali ikiwemo ya kukana umri na kujirudisha nyuma kimatendo. Kwa kifupi hii ndiyo historia ya mvi, usiziogope bure!

      Karibu rangi zote asilia za nywele zinatoka kwenye kitu kiitwacho melanin, ambacho huzalishwa na mwili kutokana na seli zinazofahamika kama melenocytes. Nywele zinapobadilika na kuwa nyeupe ina maana kwamba, melenocytes haizalishi tena melanin. Mabadiliko haya ya nywele kutoka rangi nyeusi na kukosa rangi (mvi) siyo hatua ya siku moja bali mwaka na miaka, kwani nywele moja hubadilika baada ya muda mrefu na nyingine na nyingine. Siyo hatua ya siku moja tu. Kwa kadiri mtu anavyozeeka ndivyo ambavyo uwezo wa mwili kuzalisha melanin unavyopungua.

      Uwezo huu huanza kupungua mtu anapofikia umri wa miaka 35 au 40. Lakini watu wengine huanza kuota mvi wakiwa na umri wa miaka hata 20 tu. Je, hii nayo inatokana na nini?
      Pengine ni jambo la ajabu kwamba kuvuta sigara kunatajwa kama sababu ya kuchochea mtu kupata mvi akiwa na umri mdogo. Ukiwachunguza wavuta sigara wazuri, utagundua kwamba wameanza kuota mvi mapema kuliko umri wa miaka 35 au 40. Matatizo kwenye kiungo kinachodhibiti ukuaji mwilini, yaani thyroid huweza pia kusababisha mtu kupata mvi kabla ya kufikisha umri wa miaka 35. Pia ukosefu wa vitamin B12 unatajwa kwa sababu nyingine.Kuna watu ambao hata kama wana umri wa miaka 60 bado hawataki kuona nywele nyeupe vichwani mwao .

      Watu hawa huangaika huku na kule kutafuta dawa kuondoa mvi na pengine kutumia rangi ya nywele ili kufanya rangi ya nywele nyeupe zisionekane. Huu ni kama mwendawazimu kwa kiasi fulani. Kwanini? Kwanza kuna ukweli kwamba nyingi kati ya hizo zinazodaiwa kuwa rangi za kuondoa mvi, zina athari katika mwili wa mtumiaji. Lakini wendewazimu mkubwa zaidi ni kitendo chao cha kukataa ukweli ambao inabidi wajivunie.
      Mvi bado ni dalili ya busara. Kama umefikia umri wa kuota mvi na hujafanya jambo lolote la maana na hujatoa mchango wowote wa maana kwa familia yako au jamii unamoishi ni lazima utaficha mvi zako. Kwanini? Kwa sababu utaona haya sana kuonekana kwamba umri wako ni mkubwa lakini hujafanya lolote.

      Ninaposema mchango wa maana sina maana ya fedha au mali, bali zaidi nina maana ya mawazo ya kujenga na pengine kuandaa misingi ya kujenga kwa nia ya kuleta maendeleo baadaye.
      Hebu chunguza kwa makini, utagundua kwamba watu wote wanaojaribu kuficha mvi ni wale watu ambao wametawaliwa sana na vionjo na tamaa ya miili yao kuliko maendeleo ya binadamu. Ni wale watu ambao hata kama wana fedha, hawajajua hasa wako hapa duniani kwa sababu gani. Hivi ndivyo ilivyo kwa sababu watu wa aina hii huhofia sana umri, huhofia sana kufa kwa sababu hawajakamilisha walichokuja kukifanya duniani kwasababu hawajajua bado.
      PUNJE and Boflo like this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      fazaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2009
      Posts : 2,985
      Rep Power : 1107
      Likes Received
      971
      Likes Given
      770

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Mvi ni dalili ya ujinga unakaribia kufika.
      Mtambuzi likes this.

    4. #3
      Ngekewa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 4,488
      Rep Power : 1452
      Likes Received
      388
      Likes Given
      181

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Mara nyingi huwa hivyo!
      Mtambuzi likes this.

    5. #4
      papag's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Posts : 228
      Rep Power : 545
      Likes Received
      31
      Likes Given
      93

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Mvi ni dalili ya ujinga unakaribia kufika.
      ​basi mimi ni mjinga namba moja kwa sababu umri nilionao na mvi zilizokuwepo kichani na kwenye ndevu ni balaa
      Mtambuzi and fazaa like this.
      I don’t know what the key to success is, but the key to failure is trying to please everyone.
      - Bill Cosby

    6. #5
      kamwendo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Location : Dar es salaam,Tanzania
      Posts : 83
      Rep Power : 374
      Likes Received
      42
      Likes Given
      150

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      ni kweli ndugu Mtambuzi...binafsi nilikuwa na rafiki O-level ambaye alikuwa na mvi kichwan lakin alikuwa na matendo yenye busara ingawa sijui ni kwa nini akawa na ilhali ni under 20 inawezekana ni urithi.
      Mtambuzi likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      kamwendo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Location : Dar es salaam,Tanzania
      Posts : 83
      Rep Power : 374
      Likes Received
      42
      Likes Given
      150

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      ni kweli ndugu Mtambuzi...binafsi nilikuwa na rafiki O-level ambaye alikuwa na mvi kichwan lakin alikuwa na matendo yenye busara ingawa sijui ni kwa nini akawa na mvi ilhali ni under 20 inawezekana ni urithi.

    9. #7
      fazaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2009
      Posts : 2,985
      Rep Power : 1107
      Likes Received
      971
      Likes Given
      770

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Quote By papag
      ​basi mimi ni mjinga namba moja kwa sababu umri nilionao na mvi zilizokuwepo kichani na kwenye ndevu ni balaa
      Sa hata mimi ni kama wewe, ni wachache wenye akili we watazame wengi wao wanazipaka rangi ndevu/nywele zao kua nyeusi huoni kama wajinga.
      Mtambuzi likes this.

    10. #8
      papag's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Posts : 228
      Rep Power : 545
      Likes Received
      31
      Likes Given
      93

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      sasa ile hali ya kupaka dawa au piko ili ziwe nyeusi hapo ndio ujinga unapoanzia.kwa sababu mtu akikuangalia usoni anajua tu hili zee.na kama bado yanki anajua juu huyu bado dogo
      Mtambuzi likes this.
      I don’t know what the key to success is, but the key to failure is trying to please everyone.
      - Bill Cosby

    11. #9
      fazaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th May 2009
      Posts : 2,985
      Rep Power : 1107
      Likes Received
      971
      Likes Given
      770

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Quote By papag
      sasa ile hali ya kupaka dawa au piko ili ziwe nyeusi hapo ndio ujinga unapoanzia.kwa sababu mtu akikuangalia usoni anajua tu hili zee.na kama bado yanki anajua juu huyu bado dogo
      Kwa hio tunakubaliana wengi wao ni wajinga.

    12. #10
      georgeallen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd June 2011
      Location : Seattle, WA, USA
      Posts : 2,055
      Rep Power : 0
      Likes Received
      516
      Likes Given
      260

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Exceptions zipo, lakini mvi ni dalili ya uzee. wanaokuwa na mvi at 20s or 30s, ni matatizo ya genes. Wanaopaka rangi nyewele ili ziwe nyeusi na hivyo waonekane bado vijana -hii ni psychological problem-wanajua umri wao, lakini hawataki kukubaliana na hali halisi. Mimi nilikuwa mmoja wao na pamoja na ku-dye nywele zangu mara kwa mara bado niliendelea kuamkiwa na watoto na vijana: "babu shikamoo". Mwishowe ilibidi niache.
      Last edited by georgeallen; 12th July 2012 at 18:47.
      Mtambuzi and papag like this.

    13. #11
      Purple's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Location : mjini
      Posts : 1,795
      Rep Power : 727
      Likes Received
      607
      Likes Given
      415

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      Basi mie nina upungufu wa vitamini B12 cause nina mvi mbili tatu na umri wangu bado kabisa..
      Mtambuzi likes this.

    14. #12
      MadameX's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2009
      Location : Timbaktu
      Posts : 6,158
      Rep Power : 6555
      Likes Received
      2696
      Likes Given
      1304

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      aisee mimi ni mvivu sana wa kusoma, nitarudi baada kumalizia nilipofika!
      Blessed are hearts that bend but shall never broken

    15. #13
      OGOPASANA's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Posts : 207
      Rep Power : 554
      Likes Received
      65
      Likes Given
      121

      Default Re: Mvi ni dalili ya uzee au ni kitu gani.......................... .......?

      tabasamu ni ishara ya furaha,
      Chozi ni ishara ya kilio,
      Jasho ni ishara ya kuchoka,
      Mvi ni ishara ya ..... : (a) uzee (b) inheritance (c) kuishi miaka mingi (d) U-Lowasa
      " Yesu ni Bwana"

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...