Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

    Report Post
    Results 1 to 11 of 11
    1. #1
      Felixonfellix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th February 2010
      Posts : 1,673
      Rep Power : 805
      Likes Received
      165
      Likes Given
      95

      Default Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!



      Ngoja leo niyadadavue makosa yanayofanywa na wanawake wengi pale wanapoamua ni nani wa kuoana naye:

      1. Kosa la kwanza, unaolewa na mtu ambaye unajua kabisa ni dhaifu na mkorofi, ukitarajia kwamba ataondoa kasoro zake akiwa ndani ya ndoa. Hili ni kosa kubwa. Kama huna furaha sasa na mtu kabla hujaoana naye, usikubali kuingia huo mkenge. Huwezi kutegemea mtu kuadilika aiwa ndani ya ndoa.

      2. Kosa la pili, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu ya msisimko wa mwili kimapenzi lakini si kwa sababu ya tabia zake. Kuwa mwangalifu na neno “Nakupenda” neno hili mara nyingi maana yake ni “Nina uchu nawe.” Ndiyo amevutiwa nawekimaumbile, lakini undani wa tabia yake unaujua? Hapa kuna mambo manne… Kwanza, Je anapenda kutomfanyia binadamu mwenzie mabaya kama mabavyo yeye hataki kufanyiwa? Pili, anaishi vipi na watu wengine? Anaishi vipi na watu ambao ana uadui nao, Anawasamehe au analipiza visasi? Je anatoa misaada kwa masikini? Tatu, je ni mkweli, anachokisema ndicho anachokifanya? Je anaaminika? Majukumu anayoahidi kuyafanya anayatimiza? Nne, je anajipenda? Je ni mtu ambaye yuko imara kimapenzi au ni mtu wa kuyumbayumba na asiye na msimamo? Sio mtu akishauriwa na marafiki zake au ndugu zake huko, anakuja na maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu

      3. Kosa la tatu, unaolewa na mtu ambaye hamna malengo na vipaumbele vya aina moja vya maisha. Je mna utashi wa aina moja? Kwa mfano ni vyema mwanamuziki akaolewa na mwanamuziki mwenzie kwa kuwa anajua mzingira ya kazi ya mwenzie ili kupunguza wivu wa kupindukia usio wa lazima

      4. Kosa la nne, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu mnakutana kimwili mapema mno. Kukutana kimwili kabla ya ndoa kunaweza kuleta matatizo makubwa mno. Tendo la ndoa kabla ya ndoa hufunika uwezo wa mtu kufikiri. Mtu anabaki kufaidi na kubaki kujali mapenzi ya kimwili na kusahau kukuna ubongo juu ya mambo mengine. Ni lazima mwanamke akune ubongo ili kujua kama huyo mpenzi anakidhi vigezo vyote vya mume mtarajiwa.

      5. Kosa la tano, unaolewa na mtu ambaye huna msisimko wa kimwili umwonapo. Kuna uwezekano mkubwa mwanamke akavutiwa na mwanaume kwa sababu ya aina ya gari analomiliki. Hapa hakuna msisimko wa kimwili bali mwanamke kavutwa na gari au rasilimali alizo nazo mwanaume huyo.

      6. Kosa la sita, unaolewa na mwanaume anayependa kudhibiti. kuwa na tabia ya kudhibiti wenzako ni ya dalili za mtu jeuri na mwenye kujisikia na mfujaji. Naomba kutofautisha kati ya “kudhibiti” na “kutoa mawazo.” Mtu anayekupa mawazo ni kwa faida yako, lakini anayekudhibiti ni kwa faida yake.

      7. Kosa la saba, unaolewa na mtu asiye sahihi kwa sababu unakimbia matatizo uliyo nayo. Unaweza kuwa hujaolewa na huna raha wala amani na ukataka kuolewa. Ndo haiwezi kukutatulia matatizo yako binafsi ya kisaikolojia nay a kimapenzi. Badala a kuyapunguza matatizo hayo, ndoa itayaoneza. Kama huna amani na huyafuahii maisha, chukua jukumu la kurekebisha matatizo hayo sasa kabla hujaolewa. Itakuwa ni faida kwako na kwa mmeo mtarajiwa.

      8. Kosa la nane, unaolewa na mtu asiya sahihi kwa kuwa yuko ndani ya pembe tatu. Mtu ambaye anaishi na wazazi wake ni moja ya mfano wa mtu anayeishi katika pembe tatu. Watu wengine wanaoweza wakawa wanaishi ndani ya pembe tatu ni kama wanaofanya kazi saa 24! Huyu mtu halali? Watu wengine walio katika pembe tatu ni watu wanaotumia madawa ya kulevya, mtu anayetawaliwa na “hobbie” zake, anapenda sana michezo (Mpira), kuperuzi mitandao ya kijamii na anapenda sana fedha. Hakikisha kwamba wewe na mpenzi wako , nyote hamtawaliwi na pembe tatu. Mtu ambaye anatawaliwa na pembe tatu hawezi kumtimizia mpenzi wake haja ya upendo atakapokuwa anahitaji. Kama mpenzi wako anatawaliwa na pembe tatu kwa kiasi kikubwa, wewe huwezi kuwa kipaumbele chake.

      Chanzo: utambuzi na kujitambua
      Twimane and miss linga like this.
      Tushirikiane Tutafika Tuendako

    2. Miaka 50

    3. #2
      Gwamahala's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Posts : 501
      Rep Power : 600
      Likes Received
      102
      Likes Given
      124

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Duh hiyo ya pembe tatu imenifurahisha kweli!

    4. BAK
      #3
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,593
      Rep Power : 44963
      Likes Received
      8330
      Likes Given
      8324

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    5. Mbu
      #4
      Mbu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2007
      Location : Stagnant Springs
      Posts : 10,830
      Rep Power : 9991
      Likes Received
      4709
      Likes Given
      6218

      Default

      ....thread yako nzuri sana. Utambuzi na kujitambua. Safi sana. Pamoja na "makosa" yote yanayotokea wakati wa kuchagua mume/mke bado TUNATHUBUTU kutenda kinyume, kwa visingizio "mke mwema" hutoka kwa bwana...

    6. #5
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8230
      Likes Given
      17325

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Quote By Felixonfellix


      Ngoja leo niyadadavue makosa yanayofanywa na wanawake wengi pale wanapoamua ni nani wa kuoana naye:

      Chanzo: utambuzi na kujitambua
      Umekosea chanzo ni hiki hapa:

      http://www.jamiiforums.com/mahusiano...%85%85%85.html

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Mahmetkid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Location : Kagera-Bukoba
      Posts : 414
      Rep Power : 439
      Likes Received
      104
      Likes Given
      8

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Ni vigumu kumpata mwanaume aliyemkamilifu kila idara, ndio maana wanathubuti kwa kutegemea kuwa utabadilika baadae.

      Tusiwaangushe madada zetu, kama yupo free kukwambia tabia hii na hile si nzuri kwako, kuwa tayari kubadilika.
      miss linga likes this.

    9. #7
      Nakshi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Location : any where in this world i am in available
      Posts : 228
      Rep Power : 392
      Likes Received
      92
      Likes Given
      82

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      me mmoja wapo nilivaa mkenge sikumpenda, ila nilipenda pesa zake na kuishi ulaya nikapigwa ndoa huyoo germany sasa simtaki hata kumsikia moyoni hayupo hata kidogo, soon tuna divorce, i can't wait....

    10. #8
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,144
      Rep Power : 21611
      Likes Received
      13485
      Likes Given
      17780

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Quote By Nakshi
      me mmoja wapo nilivaa mkenge sikumpenda, ila nilipenda pesa zake na kuishi ulaya nikapigwa ndoa huyoo germany sasa simtaki hata kumsikia moyoni hayupo hata kidogo, soon tuna divorce, i can't wait....
      he he hee but waonekana hujutii sana
      labda huwa unajiambia 'Lakini Ujerumani nimefika lol'...
      ha ha haa
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    11. #9
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,626
      Rep Power : 1447
      Likes Received
      845
      Likes Given
      347

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      huyo mwenye blog aache kuiba mada za mtambuzi....

    12. #10
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,169
      Rep Power : 13066
      Likes Received
      14101
      Likes Given
      14924

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      i wish maisha yangekuwa marahisi kufanya analysis kama alivyofanya huyu.

      Kusingekuwa na divorse wala kutelekeza watoto.

    13. #11
      Catherine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2012
      Location : Dar
      Posts : 1,241
      Rep Power : 595
      Likes Received
      739
      Likes Given
      208

      Default Re: Wanawake wanavyoivaa mikenge kwenye ndoa..............!

      Dunia ya sahivi full kujilipua. Kuna wanaume washajiwekea malengo kuwa gentlemen ndani ya ndoa. Waweza mpotezea nje kumbe ni mmojawapo wa husband materials.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...