Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

    Report Post
    Results 1 to 18 of 18
    1. #1
      Felixonfellix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th February 2010
      Posts : 1,673
      Rep Power : 805
      Likes Received
      165
      Likes Given
      95

      Default Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!






      Kuna wanaume ambao wametokea kuoa wanawake ambao wana tabia mbaya . ninaposema kuwa na tabia mbaya sina maana ya mwanamke kuwa Malaya, maana hiyo ni fasili rahisi ya tabia mbaya kwa watu walio wengi. Ninaposema tabia mbaya nina maana kwenda kinyume na matarajio ya mume na pengine hata kwenda kinyume na matarajio ya jamii. Mwanamke ambaye ana tabia kama ghubu, mdomo mdomo (mkosoaji), mtapanyaji wa mali, mpenda makuu na tabia nyingine za aina hiyo, ni mwanamke ambaye kwa kiasi kikubwa anaweza kumsababishia mume matatizo ya kimwili na kisaikolojia. Mwanamke wa aina hii anaweza hata kuathiri makuzi ya watoto na kuathiri uhusiano na mume na watu wengine waliyo karibu yake. Kama mwanamke wa aina hii ameolewa na mume mweledi ndoa inaweza isiyumbe sana, lakini hii ina mipaka na kiwango chake.

      Kuna wakati matatizo haya huweza kufika mbali zaidi kiasi kwamba huanza kumwathiri mume. Mwanaume ambaye huchukua kila uamuzi unaohusu maisha yake kwa hadhari kubwa, anaweza kuendelea kuishi na mke huyu. Lakini mara nyingi kuendelea kuishi na mke huyu kuna maana ya matatizo zaidi kuliko ufumbuzi. Bila shaka mmeshawahi kusikia wanaume ambao wanalalamika kuhusu tabia mbaya za wake zao (hata hapa JF wapo wengi sana), lakini huku wakiendelea bado kuwa na wake hao. Ukiacha sababu ya kugawana mali, wanaume wengi huwa wanafikiria mambo mengi ambayo huwazuia kuchukua uamuzi wa kuachana na wake hao.

      Nimeona itakuwa vizuri kuwaambia wanaume hawa kwamba, kama ndoa zao zimefikia mahali ambapo zinataka kuwatia kichaa, wakiwa na uhakika kwamba wake zao ndio wenye matatizo na sio wao, (hili inabidi waliangalie kwa makini) inabidi wafanye uamuzi kwa kujiangalia wao na watoto wao zaidi kuliko watu au vitu vingine. Baadhi ya mambo ya kuangalia ni haya:

      1. Kuathirika kwao: wajiulize wanaumia kiasi gani kimwili na kisaikolojia kwa kuendelea kuishi kwao na wanwake hawa. Kama ni ghubu na kukosolewa, kunawaathiri kiasi gani,? Na kama ni utumiaji mbaya wa mali unawaathiri kwa kiasi gani? Kama athari za tabia mbaya alizo nazo mwanamke zinafaa kudharauliwa na mume anaweza kuzidharau ni vyema akafanya hivyo, na kuendelea na maisha. Na kama akiona kuzidharau tabia hizo itakuwa na maana ya angamio kwake na pengine mbaya zaidi kwa watoto, inabidi hiyo iwe ni sababu ya msingi kuachana na mke huyo.


      2. Ndugu watasemaje: wanaume wengi hukwamia hapo. Kama wake zao wanaelewana vizuri na baadhi ya ndugu, au hata wazazi wao, wanaume hushindwa kutoa maamuzi wa kuwaacha kwa hofu ya kulaumiwa na kushangawa. Wakati mwingine mume huyu anaelewena sana na watu wa upande wa pili, yaani ndugu wa mke na hasa wazazi na pengine wote. Hiki nacho ni kikwazo kikbwa sana, kwani mume hufikiria jinsi atakavyoonekana kwa watu hawa, pale atakapoamua kuchukua uamuzi wa kumuacha mkewe.

      3. Sifa moja nzuri: pamoja na kuwa na matatizo, kila binadamu anaweza kuwa na upande mzuri. Kama mwanamke huyu ana sifa fulani ambayo ni nzuri sana, tuseme ni mpishi hodari sana na mkarinu kwa wageni , au labda ni mwaminifu sana katika ndoa, mwanaume anaweza kukwama kutoa uamuzi kwa kudhani au kujidanganya kwamba huenda anaweza asipate mwanamke mwingine mwenye sifa kama hizo. Huku ni kujidanganya kwa sababu kila sifa aliyo nayo binadamu fulani, ya kitabia, ipo kwa binadamu mwingine hata kama siyo wengi.

      Ukweli ni kwamba mwanaume anaweza kushindwa kumpa talaka mkewe ambaye anakaribia kumuuwa kwa matatizo yake kwa sababu ambazo mtu mwingine anaweza kuzishangaa. Lakini jambo la msingi kwa mwanaume kama huyu ni kujaribu kupima kwa makini, je hizo sababu zinazomfanya asite kuachana na mkewe huyu zina nguvu au maana kuliko maisha yake, hasa mwili na akili yake?.

      Angalizo: Sishauri watu kuachana, lakini nashauri watu kujua kwamba ndoa zenye mashaka makubwa ni hatari kwa afya na maisha yao.

      Chanzo: utambuzi na kujitambua
      mkush likes this.
      Tushirikiane Tutafika Tuendako

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,164
      Rep Power : 21615
      Likes Received
      13492
      Likes Given
      17791

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      mhhhhhhhh
      nyumba kubwa likes this.
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    4. #3
      platozoom's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2012
      Posts : 3,980
      Rep Power : 8270
      Likes Received
      2684
      Likes Given
      3662

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Mara nyingi ukiwasikiliza walioko kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 20 wana mengi ya kuhadithia na ukipiga darubini nyuma na kuzingatia hizo kasoro ulizotaja pengine ndoa hizo zisingekuwepo.

      Angalizo: Simaanishi uishi kwenye mateso ila nimesema tu kutokana na nilichosikia!
      "Education is something that remain in your head after forgeting what you learn at school"

    5. #4
      kashata's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Posts : 64
      Rep Power : 369
      Likes Received
      5
      Likes Given
      2

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Mkuu leta hoja za kuimarisha ndoa hii ya kuvunja ndoa hapana bana hata wazazi wetu wana maogomvi yao but wamedumu kwenye ndoa zao mpaka sasa.

    6. #5
      Kisaka80's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th February 2012
      Location : ARUSHA
      Posts : 96
      Rep Power : 387
      Likes Received
      31
      Likes Given
      142

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      maelezo yako hayaendani na kichwa cha habari .......toa njia za kumpiga chini mke mkorofi ili wadau wakuelewe but sio ngonjera za kizushiii....maelezo kibao bila hizo njia ulizosema!
      Excellent and georgeallen like this.
      'Loving and Being loved brings richness to life - I am looking for someone special to be my Wife!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Chauro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2010
      Location : kidunguche
      Posts : 2,656
      Rep Power : 995
      Likes Received
      1310
      Likes Given
      1524

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Mbona wanawake wote naowafahamu mimi ni wakorofi ukiacha utaoa nani?
      nyumba kubwa likes this.
      Nyumba hujengwa kwa hekima,na kuimarishwa kwa busara.Kwa maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza(mithali 24:3-4).

    9. #7
      HorsePower's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd August 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,649
      Rep Power : 3795
      Likes Received
      1667
      Likes Given
      1485

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Quote By Kisaka80
      maelezo yako hayaendani na kichwa cha habari .......toa njia za kumpiga chini mke mkorofi ili wadau wakuelewe but sio ngonjera za kizushiii....maelezo kibao bila hizo njia ulizosema!
      Mbona mdau umekuwa mkali, ulitaka kukopi njia za kumpiga chini wa kwako nini?
      Don’t judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

    10. SG8
      #8
      SG8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2009
      Location : DSM
      Posts : 2,556
      Rep Power : 4177
      Likes Received
      771
      Likes Given
      730

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Quote By Chauro
      Mbona wanawake wote naowafahamu mimi ni wakorofi ukiacha utaoa nani?
      kweli? Ila niseme ukweli leo hapa sijaambulia kitu.. Sijui ni kwa sababu ya kichwa cha habari...
      sweetlady likes this.
      "Tumefika hapa kutokana na udhaifu wa Rais Kikwete,Uzembe wa Bunge na Upuuzi wa CCM"

    11. #9
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,326
      Rep Power : 36531
      Likes Received
      7479
      Likes Given
      4604

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Quote By Gerrard
      kweli? Ila niseme ukweli leo hapa sijaambulia kitu.. Sijui ni kwa sababu ya kichwa cha habari...
      Tehe ! Pole mwaya......mie nimeishia kusoma heading tu, kiukweli huwa sipatani na mada ndefu!
      Life without problems never make a strong and good person!

    12. #10
      Jestina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 3,627
      Rep Power : 1447
      Likes Received
      845
      Likes Given
      350

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      huyo mwenye blog ndio mtambuzi wa humu JF?

    13. SG8
      #11
      SG8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2009
      Location : DSM
      Posts : 2,556
      Rep Power : 4177
      Likes Received
      771
      Likes Given
      730

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Quote By Neema
      huyo mwenye blog ndio mtambuzi wa humu JF?
      Ha ha ha unamchokoza Mzee wa watu?
      "Tumefika hapa kutokana na udhaifu wa Rais Kikwete,Uzembe wa Bunge na Upuuzi wa CCM"

    14. #12
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,208
      Rep Power : 13074
      Likes Received
      14118
      Likes Given
      14986

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      ndefuuuuuuuuuuu kama . . .

    15. #13
      TAMKO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 11th October 2011
      Posts : 404
      Rep Power : 0
      Likes Received
      219
      Likes Given
      37

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Hapana, Kichwa cha habari hakiendani Na maelezo, hujantendea haki kukata mistari yote bila kuona Hoja.. Ulivyoanza ni Kama unatafuta kuanza kujenga Hoja ila ja Ajabu umepotea..

      Nilidhani unatoa ushauri Kwa wale wenye kinamama korofi wafanyeje ili waendelee kuishi Na moto wao huo..

      Mie ushauri wangu wawapende zaidi, wawe wanawaandikia SMS Mara Kwa mara( ingawa hawatajibiwa) Kama wana Usafiri Basi wawe wanawapakia Na kuwapeleka kazini kwao, ni wazi kwamba Usiku mambo ya kiafrika zaidi yanaweza yasiwepo kajibisa, mkorofi hadi sex all time anasema amechoka.. Jenga Mazoea ya KUMBAKA..

      Sijui niendelee.. Wacha Niachie hapo.. Ila mwisho usiwasimulie wanawake wengine kazini au somewhere jehanam uliyonayo@ home.. Vumilia Songa mbele, nje utatengeneza watoto wasielewa chini ya usimamizi wako Kama baba, utakoma siku wakiwa wakubwa kisha wanakupigia cm "Dady Mbona hauko Na mama, au yeye ni mbaya, naskia inaishi Na mama mwingine, Dady hunipendi Mimi Na mama.." ..

    16. #14
      nyumba kubwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 4,047
      Rep Power : 2305
      Likes Received
      2874
      Likes Given
      3980

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Huu uzi ushindwe na ulegee!!!

      Quote By The Boss
      mhhhhhhhh

    17. #15
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27014
      Likes Received
      8230
      Likes Given
      17325

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Quote By Neema
      huyo mwenye blog ndio mtambuzi wa humu JF?
      Neema sio huyo mwaya aliyeandika huo uzi ni huyu hapa chini:

      http://www.jamiiforums.com/mahusiano...ya-hivi-2.html
      Neema likes this.

    18. #16
      Purple's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Location : mjini
      Posts : 1,795
      Rep Power : 726
      Likes Received
      607
      Likes Given
      415

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Sasa hua mnaoa ili iweje??kama mnapanga mikakati ya kuwaacha wake zenu bora msingeoa kwani mlilazimishwa??khaaa!

    19. #17
      SILVANUS NJENGA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th February 2012
      Posts : 60
      Rep Power : 380
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Alichokiunganisha Mungu, Mwanadamu hasikitenganishe
      Quote By Felixonfellix





      Kuna wanaume ambao wametokea kuoa wanawake ambao wana tabia mbaya . ninaposema kuwa na tabia mbaya sina maana ya mwanamke kuwa Malaya, maana hiyo ni fasili rahisi ya tabia mbaya kwa watu walio wengi. Ninaposema tabia mbaya nina maana kwenda kinyume na matarajio ya mume na pengine hata kwenda kinyume na matarajio ya jamii. Mwanamke ambaye ana tabia kama ghubu, mdomo mdomo (mkosoaji), mtapanyaji wa mali, mpenda makuu na tabia nyingine za aina hiyo, ni mwanamke ambaye kwa kiasi kikubwa anaweza kumsababishia mume matatizo ya kimwili na kisaikolojia. Mwanamke wa aina hii anaweza hata kuathiri makuzi ya watoto na kuathiri uhusiano na mume na watu wengine waliyo karibu yake. Kama mwanamke wa aina hii ameolewa na mume mweledi ndoa inaweza isiyumbe sana, lakini hii ina mipaka na kiwango chake.

      Kuna wakati matatizo haya huweza kufika mbali zaidi kiasi kwamba huanza kumwathiri mume. Mwanaume ambaye huchukua kila uamuzi unaohusu maisha yake kwa hadhari kubwa, anaweza kuendelea kuishi na mke huyu. Lakini mara nyingi kuendelea kuishi na mke huyu kuna maana ya matatizo zaidi kuliko ufumbuzi. Bila shaka mmeshawahi kusikia wanaume ambao wanalalamika kuhusu tabia mbaya za wake zao (hata hapa JF wapo wengi sana), lakini huku wakiendelea bado kuwa na wake hao. Ukiacha sababu ya kugawana mali, wanaume wengi huwa wanafikiria mambo mengi ambayo huwazuia kuchukua uamuzi wa kuachana na wake hao.

      Nimeona itakuwa vizuri kuwaambia wanaume hawa kwamba, kama ndoa zao zimefikia mahali ambapo zinataka kuwatia kichaa, wakiwa na uhakika kwamba wake zao ndio wenye matatizo na sio wao, (hili inabidi waliangalie kwa makini) inabidi wafanye uamuzi kwa kujiangalia wao na watoto wao zaidi kuliko watu au vitu vingine. Baadhi ya mambo ya kuangalia ni haya:

      1. Kuathirika kwao: wajiulize wanaumia kiasi gani kimwili na kisaikolojia kwa kuendelea kuishi kwao na wanwake hawa. Kama ni ghubu na kukosolewa, kunawaathiri kiasi gani,? Na kama ni utumiaji mbaya wa mali unawaathiri kwa kiasi gani? Kama athari za tabia mbaya alizo nazo mwanamke zinafaa kudharauliwa na mume anaweza kuzidharau ni vyema akafanya hivyo, na kuendelea na maisha. Na kama akiona kuzidharau tabia hizo itakuwa na maana ya angamio kwake na pengine mbaya zaidi kwa watoto, inabidi hiyo iwe ni sababu ya msingi kuachana na mke huyo.


      2. Ndugu watasemaje: wanaume wengi hukwamia hapo. Kama wake zao wanaelewana vizuri na baadhi ya ndugu, au hata wazazi wao, wanaume hushindwa kutoa maamuzi wa kuwaacha kwa hofu ya kulaumiwa na kushangawa. Wakati mwingine mume huyu anaelewena sana na watu wa upande wa pili, yaani ndugu wa mke na hasa wazazi na pengine wote. Hiki nacho ni kikwazo kikbwa sana, kwani mume hufikiria jinsi atakavyoonekana kwa watu hawa, pale atakapoamua kuchukua uamuzi wa kumuacha mkewe.

      3. Sifa moja nzuri: pamoja na kuwa na matatizo, kila binadamu anaweza kuwa na upande mzuri. Kama mwanamke huyu ana sifa fulani ambayo ni nzuri sana, tuseme ni mpishi hodari sana na mkarinu kwa wageni , au labda ni mwaminifu sana katika ndoa, mwanaume anaweza kukwama kutoa uamuzi kwa kudhani au kujidanganya kwamba huenda anaweza asipate mwanamke mwingine mwenye sifa kama hizo. Huku ni kujidanganya kwa sababu kila sifa aliyo nayo binadamu fulani, ya kitabia, ipo kwa binadamu mwingine hata kama siyo wengi.

      Ukweli ni kwamba mwanaume anaweza kushindwa kumpa talaka mkewe ambaye anakaribia kumuuwa kwa matatizo yake kwa sababu ambazo mtu mwingine anaweza kuzishangaa. Lakini jambo la msingi kwa mwanaume kama huyu ni kujaribu kupima kwa makini, je hizo sababu zinazomfanya asite kuachana na mkewe huyu zina nguvu au maana kuliko maisha yake, hasa mwili na akili yake?.

      Angalizo: Sishauri watu kuachana, lakini nashauri watu kujua kwamba ndoa zenye mashaka makubwa ni hatari kwa afya na maisha yao.

      Chanzo: utambuzi na kujitambua

    20. #18
      SILVANUS NJENGA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th February 2012
      Posts : 60
      Rep Power : 380
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Unataka kumuacha mke mkorofi? Fanya hivi.........!

      Ndoa ndoano xo ndoa inajengwa na uvumilivu no way out any more

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...