Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini..?

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 42
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8228
      Likes Given
      17325

      Default Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini..?


      Mnaweza kufikia umri huu bila mtoto na ndoa ikaendelea kuwa ya upendo.......


      Inaelezwa kwamba wanawake huwa wanavurugikiwa sana kiakili pale wanapogundua kwamba hawana kizazi au hawawezi kupata watoto.

      Kuna ukweli kwamba mwanaume kama mwanamke huwa anasikitishwa na kukosa mtoto katika ndoa lakini kwa bahati mbaya tafiti mbalimbali zinaonyesha kwamba mwanamke huathirika zaidi kwa kujaribu kwake kuikataa hali hiyo. Wanawake huchukulia suala la kukosa mtoto au watoto kama ndio mwisho wa maisha yao.

      Sio kwamba wanaume hawaumii kwa tukio kama hilo, la hasha huumia sana, lakini kinachotokea ni kwamba wao hulichukulia kwa uzito wa kawaida na hii husaidia kupandisha kiwango cha uwezekano kwao kupata ufumbuzi au suluhu ya tatizo hilo.

      Wanawake mara nyingi wamekuwa wakihesabiwa kama ndio chanzo cha matatizo ya ndoa zisizo na watoto na kwa bahati mbaya wanawake wameonekana kwa kiasi kikubwa kuamini lawama hizo. Jambo hili huenda ndilo ambalo linawafanya wanawake kukosa raha kabisa pale wanapokuwa hawana watoto ukilinganisha na wanaume. Wanawake huogopa kwamba kwa kukosekana watoto ndani ya ndoa waume zao wanaweza kuchukua uamuzi wa kuoa wake wengine na kuwaacha wao au wao kuwa wake wakubwa wasio na thamani.

      Hii ni njia ambayo imekuwa ikitumika sana katika mila karibu zote za Kiafrika. Lakini jambo kama hili halipaswi kuogopwa sana na mwanamke kwa sababu mume anayeamua kwenda kuoa mke mwingine kwa sababu mkewe wa awali hakubahatika kupata mtoto, huyo ni mwanaume asiye na upendo. Kwa nini basi mwanamke asione hiyo ni nafuu kwake ya kuachana na mtu ambaye alikuwa akiishi naye bila upendo.

      Kwanza siku za nyuma wakati wa ujima mwanamke angeweza kulalamika sana kukosa mtoto, kwani mtoto alikuwa ni rasilimali. Lakini siku hizi mtoto ni sehemu ya ukamilisho wa jukumu la kimaumbile la mtu kulea kama alivyolelewa. Kama mwanamke anajikuta hana mtoto anaweza kwenda kuchukuwa mtoto kwenye nyumba za watoto yatima au kuomba ustawi wa jamii ili apewe mtoto aliyetupwa au kutelekezwa na wazazi. Huyu naye ni mtoto sawa au kumzidi yule wa kumzaa kama atapata malezi mema.

      Imefika wakati ambapo inabidi wanawake wajue kwamba kukosa mtoto au watoto siyo mwisho wa dunia na wala haiwapunguzii hata chembe ya utu wao.
      NATA, Bishanga, Mkirua and 5 others like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Blaine's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 11th January 2012
      Location : on hiatus
      Posts : 1,482
      Rep Power : 3775
      Likes Received
      1038
      Likes Given
      369

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      they feel incomplete. its psychological and unless u're in the same boat u can't really understand.
      Mtambuzi likes this.
      on jf hiatus

    4. #3
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,414
      Rep Power : 1033
      Likes Received
      1170
      Likes Given
      598

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Uyasemayo ni kweli mkuu lakini tatizo ni jamii inayomzunguka pia (Mume, wakwe, mawifi nk) hawa huchangia sana matatizo kw ndoa ya aina hii...Mume anaweza kuwa undestanding na wapo hata waliokubalia wenzi wao kutafuta mtoto nje kisha akalelewa kwenye familia lakini hao nilowataja hapo juu bado watakuwa na wataendelea kuwa tatizo na sio kwa Tanzania peke yake bali karibu nchi zote za dunia ya 3 tunashea utamaduni huo.
      Mtambuzi likes this.
      The world suffers a lot. Not because of the violence of bad people, but because of the silence of good people!

    5. #4
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,407
      Rep Power : 711
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      katika majaribu yoote duniani, omba Mungu wako jaribu hili lisikupitie.....
      Mtambuzi and Mama timmy like this.
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    6. #5
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,564
      Rep Power : 5615
      Likes Received
      6211
      Likes Given
      2281

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      hizi extended family zetu hizi...
      ukichelewa kupata mtoto wanaweka midomo juu utafikiri uliolewa na ukoo mzima...

      uombe upate mume mwenye msimamo, kama mumeo bendera fuata upepo.....lazima uwe stressed!!!!!!!!!!!
      Mtambuzi and UPOPO like this.
      "Behind every great fortune there is a crime."
      - Honore de Balzac (1799-1850)

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8228
      Likes Given
      17325

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Mkirua
      Uyasemayo ni kweli mkuu lakini tatizo ni jamii inayomzunguka pia (Mume, wakwe, mawifi nk) hawa huchangia sana matatizo kw ndoa ya aina hii...Mume anaweza kuwa undestanding na wapo hata waliokubalia wenzi wao kutafuta mtoto nje kisha akalelewa kwenye familia lakini hao nilowataja hapo juu bado watakuwa na wataendelea kuwa tatizo na sio kwa Tanzania peke yake bali karibu nchi zote za dunia ya 3 tunashea utamaduni huo.
      Kuna msemo mmoja unasema ndoa ni ya watu wawili.......... hilo ndilo la muhimu kulizingatia.
      mawifi, wakwe, majirani, na watu wengine haiwahusu, nyie wanandoa ndio mnatakiwa kuwa na msimamo juu ya ndoa yenu.

    9. #7
      sanjo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th October 2010
      Posts : 861
      Rep Power : 606
      Likes Received
      219
      Likes Given
      33

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Hute
      katika majaribu yoote duniani, omba Mungu wako jaribu hili lisikupitie.....
      Mkuu ni kweli uliyosema. Ni mzigo mkubwa sana kwa mume na mke huubeba kila siku ya maisha yao.
      Mtambuzi likes this.
      Whatever exists is already becoming obsolete.

    10. #8
      Kingmairo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 778
      Rep Power : 514
      Likes Received
      234
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By Hute
      katika majaribu yoote duniani, omba Mungu wako jaribu hili lisikupitie.....
      Ndugu Hute wewe hili ndo umeliona jaribu baya kuliko yoote humu duniani? Hakika kama ndivyo, hujatembea ukaona majaribu ya magonjwa mengine. Hili ambalo unapumua, unaenda popote utakapo, kazi unafanya na starehe zingine zozote wewe ndio unaliona jaribu baya kuliko? Kuna watu hata kunyanyua mguu kwenda haja ndogo hawawezi, na sio mapenzi yao!
      Mtambuzi likes this.

    11. #9
      Rev. Damasus Mkenda's Avatar
      Member Array
      Join Date : 22nd December 2011
      Posts : 60
      Rep Power : 386
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Hatuoani ili kupata watoto, bali tunaoana kusaidiana, watotoni zawadi toka kwa Mungu aliyetuumba. Sasa kwanini wanawake au wanaume wanavurugukiwa??? Shida yetu wengi tunaoa on behalf of the family as a result if we can not fullfill their desires they will intimidate us and will not be able to bounce back.

      Mungu awabariki.

    12. #10
      Masuke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2008
      Posts : 2,171
      Rep Power : 1007
      Likes Received
      382
      Likes Given
      81

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Mkuu Mtambuzi hayo uliyosema ni rahisi kuyatimiza kinadharia lakini kihalisia ni mtihani mkuu sana tena sana, wanawake wanapata taabu ndugu yangu we acha tu, pole kwa wanawake wote wenye matatizo kama hayo, wanaitwa majina ya kila namna hasa na mawifi zao na ukikuta mwanamme ndo anafanyia kazi kila anachoambiwa ndoa huwa ni ya matatizo na matokeo yake wanaishia kuachana, lakini vile vile hata kama mwanamme atakuwa ni mwelewa bado mwanamke huathirika tu kutokana na maneno ya majirani, ndugu wa mmewe hufikia hata wanawake wenye matatizo kama haya huogopa kwenda kwenye mikusanyiko kama misiba, harusi.
      Mtambuzi and BADILI TABIA like this.

    13. #11
      nisha's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 350
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Jamani ndugu zangu Shikamooni na kwa vijana wa rika langu Mambo!

      Nimekuelewa sana,na umeelezea vya kutosha,ni wajibu nikusifu.
      Unajua kila kitu kina chanzo,ndiyo!! sikatai kuna wengine ni kwa sababu ya kibiologia lakini wengine wanajitakia eidha kwa kutoa mimba ambapo hapo tukiongelea zaidi hawa kaka zetu wanaotamani tu mwanamke kimapenzi utadhani wakioa hawatafanya mapenzi na hata wengine wana wake zao lakini sijui kwanini wanatamani vya nje tena.
      Na zaidi kaka'ngu kitu cha ziada ni kwamba kuna methali isemayo:uchungu wa mwana haujuaye ni mzazi:Je kakangu labda sijazaa na nina tatizo hiyo la kutokuzaa ikafikia pahala nikasema niende kwenye mashirika ya watoto yatima hili nikafate utaratibu na hatimaye nipate mtoto.
      Swali ni kwamba je nitajua uchungu wa mamaye?au ilikuwaje mpaka akafika hapo?zaidi watakwambia walimuokota,sikatai kabisa kaka yangu hila bado chanzo cha huyo mtoto akijafahamika vizuri.
      Kaka kweli kuna mtu amesema maji ya bomba yakatike kwa mwenzio lakini yakikatika kwako ndo utajua faida ya maji,Na msiba usikilizie kwa mwenzio hila ukija kwako hayo ni mengine.
      Cha muhimu tuwape vijana elimu ya kutosha kuhusu hasara ya kutoa mimba,na pia zaidi tumuamini Mungu kuwa anaweza yote na ipo siku hatasikia sala kwa Waja wake hasa kwa wale ambao ni matatizo ya kibiologia tu hili suala limewakumba tu na tujihadhari zaidi na tamaa kwani ni mbaya sana ndugu zangu.
      Mtambuzi likes this.

    14. #12
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,407
      Rep Power : 711
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Kingmairo
      Ndugu Hute wewe hili ndo umeliona jaribu baya kuliko yoote humu duniani? Hakika kama ndivyo, hujatembea ukaona majaribu ya magonjwa mengine. Hili ambalo unapumua, unaenda popote utakapo, kazi unafanya na starehe zingine zozote wewe ndio unaliona jaribu baya kuliko? Kuna watu hata kunyanyua mguu kwenda haja ndogo hawawezi, na sio mapenzi yao!
      ninasema hivi kwasababu ninao ndugu zangu kama wawili hivi wamepitia jaribu hilo na sasa karibia wanapita muda wa kuzaa kwa mwanamke....stress inavyowasumbua pamoja na kwamba wana hela nyingi wana pesa nyingi sana, ni kubwa mno, pressure wanayopata toka kwa ndugu upande wa mume ni kubwa mno, pressure wanayopata toka kwa majirani ni kubwa mno kiasi kwamba mwanamke hana hata raha ya kutembea mtaani au kutembelea vikao mbalimbali vya ukoo au arusi, kwasababu kila mtu anamnyoshea kidole kuwa huyo ni tasa, akigombana na mtu tu anaimbiwa taarabu ya majungu hadi anachoka....ni mateso makubwa sana, unajua kuteseka kisaikolojia ni mbaya kuliko kuteseka na jambo ambalo dawa ipo.....najua kweli kuna matatizo makubwa kuliko hilo lakini hili nalo ni moja wapo ya matatizo makubwa mno....cha kuelewa ni kwamba, mtoto ni zawadi toka kwa Mungu, si zawadi toka kwa mganga au kwa shetani, Mungu awweza kumpa mtu mtoto katika umri wowote ule na wakati wowote ule....na nyie wanawake mnavosemana? na kuimbiana nyimbo za taarabu? mnatiaga aibu.
      Mtambuzi likes this.
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    15. #13
      nisha's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 18th June 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 350
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Ndugu hatuendi hivyo,Kila kitu kina malengo,unakula hili ushibe,unavaa hili kuficha uchi,una panda mimea hili ukifika muda uvune na zaidi Hata Mungu aliyeumba dunia yeye kama yeye aliwaumba wanadamu hili waongeze nchi hata ukisoma neno lake kwenye biblia.

      Hivyo basi ndo maana kuna faida na hasara.Anayepata faida na abarikiwe na kuweka mbinu zaidi na kukitunza kitu hicho Mfano: mwanamke anayezaa naye anayo budi kukitunza zaidi kiumbe hicho na kukipa malezi bora.

      Je yule ambaye hana na hawezi kuwa naye unamshaurije wewe kama wewe?Swali kwako.

      Sorry kama nimekukwaza?
      Mtambuzi and Hute like this.

    16. #14
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8228
      Likes Given
      17325

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Hute
      ninasema hivi kwasababu ninao ndugu zangu kama wawili hivi wamepitia jaribu hilo na sasa karibia wanapita muda wa kuzaa kwa mwanamke....stress inavyowasumbua pamoja na kwamba wana hela nyingi wana pesa nyingi sana, ni kubwa mno, pressure wanayopata toka kwa ndugu upande wa mume ni kubwa mno, pressure wanayopata toka kwa majirani ni kubwa mno kiasi kwamba mwanamke hana hata raha ya kutembea mtaani au kutembelea vikao mbalimbali vya ukoo au arusi, kwasababu kila mtu anamnyoshea kidole kuwa huyo ni tasa, akigombana na mtu tu anaimbiwa taarabu ya majungu hadi anachoka....ni mateso makubwa sana, unajua kuteseka kisaikolojia ni mbaya kuliko kuteseka na jambo ambalo dawa ipo.....najua kweli kuna matatizo makubwa kuliko hilo lakini hili nalo ni moja wapo ya matatizo makubwa mno....cha kuelewa ni kwamba, mtoto ni zawadi toka kwa Mungu, si zawadi toka kwa mganga au kwa shetani, Mungu awweza kumpa mtu mtoto katika umri wowote ule na wakati wowote ule....na nyie wanawake mnavosemana? na kuimbiana nyimbo za taarabu? mnatiaga aibu.
      Dawa ya mjinga ni kumpuuza, hiyo ndio kiboko ya mambo, kama wanaimba taarabu sijui na mafumbo mengine kama ukiwapuuza watafika mahali watazoea na watajiona wao ndio wajinga. Kumbuka mtu kuathiriwa kisakolojia na watu baki ni kutaka mwenyewe, kama kila jambo utalipuuza hakuna kitakachoakuathiri......

      Mimi ninachosema hapa ni wanandoa kukubalia matokeo na kutafuta namna nzuri ya kuimarisha ndoa yao kwa jinsi watakavyoona inafaa na sio jamii au ndugu wawapangie namana ya kuishi.

      Kuna wanandoa wana watoto, lakini kutokana na watoto hao kuwayumbisha kutokana na kuwa na mienendo isiyofaa, wanatamani hata wasingezaa, kuzaa sio ishu siku hizi kama ilivyokuwa zamani.

    17. #15
      Hute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 1,407
      Rep Power : 711
      Likes Received
      354
      Likes Given
      23

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By nisha
      Ndugu hatuendi hivyo,Kila kitu kina malengo,unakula hili ushibe,unavaa hili kuficha uchi,una panda mimea hili ukifika muda uvune na zaidi Hata Mungu aliyeumba dunia yeye kama yeye aliwaumba wanadamu hili waongeze nchi hata ukisoma neno lake kwenye biblia.

      Hivyo basi ndo maana kuna faida na hasara.Anayepata faida na abarikiwe na kuweka mbinu zaidi na kukitunza kitu hicho Mfano: mwanamke anayezaa naye anayo budi kukitunza zaidi kiumbe hicho na kukipa malezi bora.

      Je yule ambaye hana na hawezi kuwa naye unamshaurije wewe kama wewe?Swali kwako.

      Sorry kama nimekukwaza?
      sijajua hili swali umeelekeza kwa nani, manake hapa tumechangia wengi kwelikweli, ni mtoa mada au sisi wengine ambao tumejaribu kuchangia? nisha
      Mtambuzi likes this.
      Kama huna meno,usile bisi, kula Bwimbwi yaani kimbugi. Uongozi ukikushinda waachie wanaoweza!

    18. #16
      HorsePower's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd August 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,649
      Rep Power : 3795
      Likes Received
      1665
      Likes Given
      1485

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Mtambuzi
      Mnaweza kufikia umri huu bila mtoto na ndoa ikaendelea kuwa ya upendo.......

      ...... Imefika wakati ambapo inabidi wanawake wajue kwamba kukosa mtoto au watoto siyo mwisho wa dunia na wala haiwapunguzii hata chembe ya utu wao.
      Thanks Mtambuzi kwa hii mada yako na hasa kwenye sentensi yako ya mwisho umezungumza vzr sana! Naamini maneno haya yatawatia moyo wanawake wote ambao hawaja jaaliwa kupata watoto ....

      Asante,

      HorsePower
      Don’t judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

    19. #17
      UPOPO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2010
      Posts : 343
      Rep Power : 455
      Likes Received
      104
      Likes Given
      45

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Hebu tusaidiane ,kifanyike nini kwenye jamii hali hii ieleweke .Kwani tayari tunaissu kama hizo nyingi tu

    20. #18
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8228
      Likes Given
      17325

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By nisha
      Ndugu hatuendi hivyo,Kila kitu kina malengo,unakula hili ushibe,unavaa hili kuficha uchi,una panda mimea hili ukifika muda uvune na zaidi Hata Mungu aliyeumba dunia yeye kama yeye aliwaumba wanadamu hili waongeze nchi hata ukisoma neno lake kwenye biblia.

      Hivyo basi ndo maana kuna faida na hasara.Anayepata faida na abarikiwe na kuweka mbinu zaidi na kukitunza kitu hicho Mfano: mwanamke anayezaa naye anayo budi kukitunza zaidi kiumbe hicho na kukipa malezi bora.

      Je yule ambaye hana na hawezi kuwa naye unamshaurije wewe kama wewe?Swali kwako.

      Sorry kama nimekukwaza?
      nisha ............ muuliza swali, wewe unadhani suluhisho ni nini, maana mimi nimehatoa suluhisho katika maelezo yangu hapo juu, labda kama hujasoma maelezo yangu yote.

    21. #19
      HorsePower's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd August 2008
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,649
      Rep Power : 3795
      Likes Received
      1665
      Likes Given
      1485

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By Rev. Damasus Mkenda
      Hatuoani ili kupata watoto, bali tunaoana kusaidiana, watotoni zawadi toka kwa Mungu aliyetuumba. Sasa kwanini wanawake au wanaume wanavurugukiwa??? Shida yetu wengi tunaoa on behalf of the family as a result if we can not fullfill their desires they will intimidate us and will not be able to bounce back.

      Mungu awabariki.
      Asante Mtumishi kwa ufafanuzi. Sikutegemea kugongana na mtumishi wa Bwn hapa jukwaani, ila nimefurahi. I hope kusikia mengi mazuri toka kwako.
      Don’t judge each day by the harvest you reap but by the seeds that you plant.

    22. #20
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27013
      Likes Received
      8228
      Likes Given
      17325

      Default Re: Mwanamke: Hata kama huzai kinakuuma nini………………..?

      Quote By UPOPO
      Hebu tusaidiane ,kifanyike nini kwenye jamii hali hii ieleweke .Kwani tayari tunaissu kama hizo nyingi tu
      UPOPO jamii inatakiwa kuelewa kwamba tatizo la kukosa mtoto au watoto katika ndoa sio tatizo la mwanandoa mmoja, inawezekana akawa mume ndio mwenye tatizo au mwanamke.
      Inatakiwa jamii ikubali kwamba tatizo hilo lipo na jamii iwakubali wanandoa wasio barikiwa kupata watoto kutokana na matatizo yaliyo nje ya uwezo wao. kwani kila jambo ni majaaliwa na kama imeshindikana hakuna haja ya kuwanyanyapaa au kumnyanyapaa mwanandoa mwenye tatizo hilo, bali ni kujaribu kumsaidia kuondokana na dhana iliyojengeka katika jamii kwamba kukosa mtoto kwa wanandoa ni tatizo kubwa...........

      Inashasngaza mwanaume anaweza kuwa ndiye mwenye tatizo lakini bado jamii ikamuona mwanamke kuwa ndiye mwenye tatizo, wakati mwingine mwanamke hulazimika kutoka nje ya ndoa ili kutafuta mtoto, ili kumfichia mume aibu! je akileta UKIMWI ni nani wa kulaumiwa.....?

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...