Mke wangu ni mwalimu wa sec, ana mtoto mdogo wa miezi 6, toka ajifungue vituko vilikuwa haviishi....kuninunia daily sometimes hadi 3 weeks or mwezi. Nilipoona mambo yanazidi nilimrudisha kwao kwa muda kama wa mwezi mmoja hivi kwa sababu alikuwa ana maternity leave. Hata hivyo nilijua huenda postnatal period ndio inamfanya awe vile hivyo kwangu nikaona ni busara kuwa mpole ili kuepusha shari.
Aliporudi kutoka kwao tuliishi kwa maelewano mazuri kwa muda wa wiki moja tu, then yakarudi yale yale...ful mnuno kwangu lakini stori nyingi tu kwa mashost zake na majirani.
Mke wangu anafundisha kibaha, na tulikuwa tunaishi sote Dar sababu ndiko nilikojenga kibanda chetu cha kuishi na pia mimi ndiko ninakofanyia kazi. Mwezi uliopita nilishangaa mke wangu kuniambia kuwa yeye anataka kuhamia kibaha ili awe karibu na kituo cha kazi, pili ili aweze kupunguza gharama za usafiri za kila siku. Ikumbukwe kuwa ameanza kazi toka February 2011 na mimi siulizii mshahara wake anafanyia nini yeye ndiye ajuaye....but baada ya hoja yake hiyo nikajiuliza apunguze gharama za nauli....? je hela anafanyia nini? sikutaka ugomvi nikamruhusu lakini nikamuuliza vipi kuhusu maandalizi akasema kila kitu kipo sawa...chumba, kitanda+godoro na mahitaji mengine yote.
Ameondoka tarehe 04 June kuhamia kibaha, nikamwambia nitampeleka na gari hadi kibaha alikataa kata kata na kusema nimuache tu ubungo atapanda bus. Pia aka-haidi weekend atarudi lakini hakurudi na bila kutoa sababu. Ijumaa ya juzi amerudi home but still hakuwa mchangamfu, pia kuonekana kama ana chuki nami.
Kwa kuwa ni muda mrefu sijapata unyumba na yeye ndio mke wangu usiku wa kuamkia leo nikaomba haki yangu,.....WANA JF HAMUWEZI KUAMINI LAKINI NAWAAMBIA UKWELI....Nimekuta ikulu ya mke wangu imetumika kiasi cha kutosha saana hadi kiasi kwamba nilipatwa na mshangao wa ajabu....hiyo ilikuwa round ya kwanza, nilipojaribu ya pili...nilishindwa kumaliza game...coz sio K bali ni hatari. NILIUMIA SANA.
Toka saa 8.30 usiku sijalala hadi saa 10.30 usiku/alfajiri, niliamua kumuuliza tena kwa upole huku nimemkumbatia....kuwa huko kibaha ana wanaume ana-do nao!Alikataa kata kata....but alipoona naongea kwa upole sana akaingia kingi na kusena ndio anakiri ...lakini ni mwanaume mmoja tu ndio anatembea nae lakini sio wengi. Nikahoji ni nani huyo? nikaambiwa ni mfanyabiashara, anakaa kimara baruti, mmeanza toka lini mahusiano yenu....akasema toka...mwezi uliopita, mlifahamiana wapi.....tulifahamiana kwenye bus wakati naenda kazini.
Baada ya hapo akaanza kuliaaa.....na kusema anaomba nimsamehe!Nikamuuliza uliomba ruhusa ya kuhamia kibaha ili uwe huru? Je umekosa nini kwangu au mimi nilikuwa sikutoshelezi? akajibu hapana!
......WANA JF am so sorry kwa maelezo marefu but nimechanganyikiwa na simuelewi mke wangu. Anataka nimsamehe, but kabla sijachukua maamuzi nimeona ni vema niwashirikishe nyie ndugu zangu ili niweze kujiridhisha kwa uamuzi nitakao uchukua baada ya kupata maoni yenu.
NARUDIA TENA.....SAMAHANI KAMA MTAKWAZIKA KWA KUSOMA MAELEZO MAREFU...!
UPDATES
1. mke wangu ana miaka 32 na wala sio mtoto wa under 20!
2. UKIWA MAKINI NA MKEO/MPENZI WAKO NI RAHISI SANA KUJUA KAMA K IMETUMIKA....believe my words plse.
Huo ni mtihani mkubwa! Mwanamke anatembea na Mfanyabiashara huo ni mtandao ambao hatima yake ni Ngoma ni kifo! Kwa vile ameamua kusema ukweli huenda bila kushurutiswa may be anaweza kuwa amejutia kile alichofanya, nenda ukapime kabla hamjaendelea na mambo mengine angalia mwenendo wake kwa kipindi hiki LAKINI HAKIKISHA HICHO KI NYUMBA KIDOGO CHA KIBAHA KINAKOMA MARA MOJA!!!!
uko sahihi..hawa wafanyabiashara sio wa kuwaamini kabisa aise..
....kaka, unajua wakati unakula kiapo cha ndoa...kuna kipengele uliulizwa "unakubali kumuoa kwa shida na raha"..... ....kitendo cha wewe kushindwa kumstahmilia "shida." Mpaka ukaamua kumpeleka "ukweni" tayari ulishazua mazingira ya kushindwa kutekeleza kiapo chako cha ndoa. ....wewe ulichangia yeye kujiskia mpweke, na kujiskia hana thamani kwako. Nakuomba zingatia kwamba mpaka yeye afikie hayo, kuna mengine mengi umechangia. Msamehe mkeo, muweke karibu akueleze shida ni nini. Wewe umeumia tangu saa nane mpaka saa kumi, yeye alikuwa anakosa raha siku, wiki na miezi.....mpaka ulipoamua kumuuliza "kulikoni" ..... Msamehe, mfungue kurasa mpya wa maisha. Ila, jipimeni kama hamjaathirika na STD au hata HIV ...
Bora hata Mbu umeliona hilo maana, sometimes( not all the times) wanawake wengi wanaotoka nje ya ndoa zao sababu kubwa huwa ni kulipiza kisasi ,unakutwa keshatendwa vya kutosha na mumewe kavumilia wee mpaka akachoka na yanini kujipa shida ilhali kuna watu wanampenda huko nje anaona bora akasuuze roho yake kidogo! Cha msingi huyu kaka ni kukaa chini na kuangalia wapi penye mapungufu wayamalize mana kuna uwezekano mkubwa u hata yeye huwa anatoka nje ya mahusiono yao!
Mimi nimeshindwa hata kushangaa? Una uhakika mtoto huyo wa miezi sita ni wako au wa huyo jamaa? Maana sisi wanawake tunavyoweka kipaumbele kwa watoto iweje yeye achiti huku ananyonyesha? Alikuwa haoni kuwa anaweza kwaa HIV na kumwambukiza mtoto??
Sina cha kukushauri maana mwanamke anachiti si kwa mhemko ni kwa sababu; cheating ni kama 'tip of the iceberg'. Anaweza kweli kuchiti na huku anakupenda? Na kama penzi limeisha, je mnaweza lirudisha? Au ulimchiti akiwa na mimba na yeye ameamua kulipiza kisasi; there must be a reason si mhemko, aweje na mhemko wakati wewe upo?
By georgeallen
Mke wa ndoa mwenye mtoto wa miezi 6 hawezi kusamehewa kosa la hilo alilokiri mwenyewe kwa kinywa chake. Alichofanya hakisameheki, ni dharau na uamuzi sahihi ni kumuacha tu.
Pole sana ndugu,
Hizo ndizo changamoto za mahusiano. Najua hapa kila mmoja atashauri la kwake lakini wewe ndiye unayepaswa kutafakari na kufanya uamuzi unaoona ni wa faida kwako, mwanao na mkeo. Pamoja na faida uamuzi huo ukuwezeshe kupata suluhisho la kudumu. Binafsi nakushauri ufanya haya:
1. Zungumza na mkeo; kwa kuwa amekiri kosa na kuomba msamaha ahame Kibaha na arudi home (Dar). Mara nyingi kuishi mbali na mwenzi kuna vishawishi vingi sana. Hili mnalifanya kutokana na kuwa dalili zimejionesha wazi kuwa kua udhaifu. Kuishi pamoja kutakuondolea wasiwasi wa kuwa "huenda anakusailiti" pindi akiwa Kibaha.
2. Mkiwa na mkeo fanyeni ibada ya toba kwa pamoja (kama mtaona vema mnaweza kumshirikisha kiongozi wenu wa dini)
Binafsi ninaamini kuwa ni Mungu pekee aletaye msamaha wa dhati na ujasiri wa kushinda dhambi.
3. Ni vema mkashauriana na mkeo mkaenda kupata ushauri na kupima VVU ; utaniuliza why? Kupima VVU hakuna maana kuwa baada ya kukuta majibu tofauti na matakwa yenu muachane, la! Kupima kutawawezesha kufahamu hali yenu ya maambukizo na kuamua ni kwa namna gani mtaishi bila kuambukizana na kama wote mko salama kufahamu namna gani mtaishi bila kupata maambukizi.
4. Fanya utaratibu wa mkeo kupata kituo cha kazi hapo Dar; najua itachukua muda lakini ni vema kushughulikia uhamisho huo.
Hili la mwisho ni ushauri kwako; si vema sana kuanika madhaifu ya mwenzanko hadharani. ninaposema hadharani naamanisha mahali kama jukwaa hili. Ni rahisi kudhani hakuna anayekufahamu kwa kuwa wengi tunatumia majina bandia; ukweli ni kuwa yamkini wawili watatu wanakufahamu na huenda wakamfahamu hata mkeo. Unaongeza watu wa kumdharau mkeo na kutomuamini. Najua haya ni maumivu makali sana; lakini ni vema kuwashirikisha aidha wadhamini wenu wa ndoa, kiongozi wa dini au wazazi (kama unaona vema na unawaamini watakushauri vema); kinyume cha hapo mara zote jaribuni kumaliza tofauti zenu kwa kutafuta suluhisho ninyi wenyewe!
mchana mwema
EJL
Umemshauri vizuri sana huyu mtu, hasa la kumuanika mkewe hapa jamvini! Ndoa yao imekuwa na nyufa toka wanaoana, akiwa mjamzito na sasa ameshajifungua na hatua zote jamaa anaanikaga hapa jamvini na kila kitokeacho. I thnk the guy has played a great role kuufikisha unyumba wake hapo ulipo kwani Huwa nahsi jamaa ni immature au mtoto wa mama sana kwani malalamishi yake juu ya ndoa yanakera kweli na ni ya kila siku na humlaum mkewe tu bila kufikiria pande ya pili amecheza role gani mpaka mambo yakawa km yalivyo. Am sory 4 that lady and ths guy too cuz walioana hawapendani, wamebaki wanatesana tu. Ebu Kina baba wa humu..Bishanga, Mtambuzi, Aspirin na wengneo wenye busara mvuteni mwenzenu chemba mpeni ushauri wa kiume manake ameshapotea, amepoteza mwelekeo, hana tumaini na mkicheza anaweza jidhuru! Msaidieni mawazo maana dhuu...!
Sina cha kukushauri maana mwanamke anachiti si kwa mhemko ni kwa sababu; cheating ni kama 'tip of the iceberg'. Anaweza kweli kuchiti na huku anakupenda? Na kama penzi limeisha, je mnaweza lirudisha? Au ulimchiti akiwa na mimba na yeye ameamua kulipiza kisasi; there must be a reason si mhemko, aweje na mhemko wakati wewe upo?
Hizi ndizo talalila nisizozikubali mimi. Kwani mhemko siyo sababu? Au sababu ni nini?
Na kusema kwamba "mwanamke anachiti si kwa mhemko ni kwa sababu" ni sweeping generalization ambayo pia ni dhana potofu.
Mtu unaposema hivyo ni kana kwamba wanawake wote hapa duniani wamekuambia na kukuthibitishia hivyo na wakakuteua wewe uwe msemaji wao jambo ambalo haliwezekani.
Wapo wanawake wengi tu ambao wanacheat kwa sababu tu ya kuvutiwa na hao wanaume wanaocheat nao. Wapo wanawake ambao wanacheat kwa sababu wana 'loose morals'. Kwa ujumla sababu zinazopelekea wanawake kucheat ni nyingi na "mhemko" ikiwa ni mojawapo.
Wanaume msibweteke na kuikubali hii dhana potofu. Inapotosha.
Ni kweli GALIMA Jamaa alikuwa mpole sana ,hawa wanawake wa siku hizi ukiwa mpole sana watakuita shost then utasaidiwa majukumu mengine kama Unyumba.Mimi mwenzenu jana usiku Nimemchapa makofi my wife maana alileta ushost na mimi siko kivile ,Mwanaume lazima ujipambanue nyumbani kwako Maana wewe ndio Commanda in chief sasa kama mke anahama tena anakwambia kila kitu kipo sawa unakubali tu bila kufikiri kuhoji na kutafutia majibu wakati unajua tabia ya mkeo haikuwa sawa ,hapo ulikosea sana Bro.Kumbuka hawa wakina mama inatakiwa tuishi nao kwa akiri sana .na ndio maana wakati mwingine lazima uwe mkali kama pilipili lakini unaongeza hamu ya kula .Think twice uamuzi ni wako !
Hili hii mada iwe nzuri, nina appointment na mke wa mtu jioni hii, nitarudi hapa kutoa ushuhuda hasa ni kwa nini hawa Wanawake huwa wanatuonjesha na sisi hata baada ya kuolewa.
Nitarudi hapa usiku na nitajitahidi nielewe mawili matatu ni kwa nini jioni hii asijoin familia yake na ananihitaji mimi instead.
Mie nimeblow na nimeshindwa kukushauri..... Kama hujaua kuku toka amejifungua yawezekana sababu kubwa ni recovery ya machine imekua ngumu afta kujifungua.
ushauri katika ukubwa wa mbunye
Inaonekana uke wake ni too alkalinity thats y umeshindwa kurudi sawa sawa mkuu.
kama ungekua ni acidic unge recover very early na kurudi kama original. Ndo maana wadada wengine wanaopenda kuurudisha tight huwa wanatumia ndimu au limao
....kaka, unajua wakati unakula kiapo cha ndoa...kuna kipengele uliulizwa "unakubali kumuoa kwa shida na raha".....
....kitendo cha wewe kushindwa kumstahmilia "shida." Mpaka ukaamua kumpeleka "ukweni" tayari ulishazua mazingira ya kushindwa kutekeleza kiapo chako cha ndoa.
....wewe ulichangia yeye kujiskia mpweke, na kujiskia hana thamani kwako. Nakuomba zingatia kwamba mpaka yeye afikie hayo, kuna mengine mengi umechangia.
Msamehe mkeo, muweke karibu akueleze shida ni nini. Wewe umeumia tangu saa nane mpaka saa kumi, yeye alikuwa anakosa raha siku, wiki na miezi.....mpaka ulipoamua kumuuliza "kulikoni" .....
Msamehe, mfungue kurasa mpya wa maisha. Ila, jipimeni kama hamjaathirika na STD au hata HIV ...
Hata mimi mtizamo wangu ni huo hapo red. Simtetei mkeo lakini kiukweli wewe mwenyewe umechangia kwa kiasi kikubwa sana mke wake kutembea na huyo 'mfanyabiashara mchaga'. Tena ni kwamba amekuta alivyotarajia sivyo ndo maana amerudi, vinginevyo usingemuona tena.
Yaani kitendo cha yeye kununa muda wote huo halafu we unatake easy tu - ni mbaya sana kwa mwanamke. Alitegemea umbembeleze akueleza kwanini ananuna nuna, we hukujali. Halafu ume-assume mshahara wake unamtosha kwa matumizi yake kazini (yaani nauli, chakula, maji, soda n.k). Mbaya zaidi anakuomba ahamie karibu na kazini kwake pia unakubali tu, tena unaona sawa tu kuambiwa tayari ana godoro, kitanda n.k. Kwa jinsi wanawake walivyo ni wazi kuwa alijenga mawazo kuwa humpendi, humjali na humthamini, ndo maana kila kitu kwake unatake easy tu!
Kifupi ni kwamba ulimjengea mazingira hatarishi, na ndo maana huyo jamaa akampata kwa ku-take advantage ya hii weakness. Usiishe na mke hivyo aisee. Yaani hata ukioa mwingine, usipobadilika naye atakuwa kama huyu uliye naye. Binafsi nashauri umpe second chance, halafu na wewe ubadilike usim-treat tena hivyo, utaona atakavyobadilika na kuwa mwanamke mzuri zaidi. Kweli inauma lakini ndo hivyo inabidi uwe na moyo mkuu. Uzuri hiyo kitu haina makombo, ni perception tu lakini hakunaga alama, au mzee ulimkuta bikira?
Angalia vizuri kaka, inawezekana hiyo tabia hajaanza leo wala jana...Umchunguze vizuri na huyo mtoto si ajabu umeibiwa Kaka... Na utahakikisha vipi kama ameachana na huyo jamaa yake?? Pole sana...
.....story zote zina pande tatu,...His-story, Her-story, and The Truth.....naamini huyu mama nae akija jitetea humu, upepo utageuza tanga...
.....huyu mama ambaye taaluma ni mwalimu halafu atembee na mfanyabiashara...pia, lile tamko la awali kwamba "hajatembea na mkewe siku nyingi"...maswali yanaongezeka kwa ndugu yangu Ngoswe hapa.
Mimi nadhani Ngoswe usiyumbishwe na michango ya humu. Akili kichwani mwako, madhali umelileta humu bda ya kukuuma...inathibitisha bado unampenda mkeo. Hiyo ni hatua nzuri ya kwanza.
Sasa basi, akili za kuambiwa...changanya na zako, kisha kumbukia hata ukimuacha mkeo, sio kigezo kwamba utaishi kwa furaha na amani mbele ya safari. Tatua tatizo hili kiume, wewe mwanaume bana, usijikubalishe kusaidiwa na mwanaume mwenzako.
Ondosha mapungufu atayokwambia mkeo. Ndoa si lelemama jamani. Ndoa ni kazi. Msidhani ukishaoa/ukishaolewa kazi imekwisha. Mnajukumu la kuendelea kujenga, kuboresha, kulinda na hata kujishusha pale mkeo atapokuwa anakukosoa kwa yale unayovuka mpaka wa makubaliano yenu ya ndoa...
Sasa basi, akili za kuambiwa...changanya na zako, kisha kumbukia hata ukimuacha mkeo, sio kigezo kwamba utaishi kwa furaha na amani mbele ya safari
Hata asipomuacha si kigezo kwamba ataishi kwa furaha mbele ya safari maana kuwa cheated on ni traumatic experience vilevile.
Uwezekano wa kupatwa na flashbacks ni mkubwa sana na hizo flashbacks zinaweza kabisa zikawa source ya simanzi na matatizo mbele ya safari.
Akibaki na mkewe sidhani kama maisha yatakuwa kama yalivyokuwa huko nyuma maana wingu la mkewe kumegwa lazima litakuwepo tu kichwani mwake.
I just can't envision life being the same again with someone who has cheated on me multiple times. Maybe others can but I just can't. I'll bring it up over and over again and she'll never be able to hear the end of it.
But maybe dude can forgive and forget and move on happily ever after. Maybe.....
"naahidi kuwa mwaminifu kwako na nitakupenda hadi kifo kitakapo
tutenganisha".
Kama alizungumza haya maneno huyo fukukuza kabisa!
Mkuu wewe ni kijana kbs chukua mtoto wako lea mwenyewe huyu
lazima atakuja kukusumbua tu na kwa weakness alizo onyesha huyu
kuna siku atashauriwa hata aku ue ili warithi mali tumeshuhudia
na tumeona shtuka na chukua hatua brooooo....!
Follow Us Here