Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 23
    1. #1
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!


      Wanawake hawahitaji ufumbuzi wanapoeleza madhila yao, shiriki nao kwenye hisia zao inatosha
      (Picha haihusiani na habari hii)

      Tafiti nyingi zilizofanywa kwa muda mrefu zinaonyesha kwamba wanawake hutofautiana kabisa kimaumbile na wanaume kiasi kwamba inakuwa kama vile ni viumbe wawili tofauti. Mtaalamu mmoja wa mahusiano ya watu John Gray anamuelezea mwanaume kuwa anatoka sayari ya Mars na mwanamke anatoka kwenye sayari ya Venus, akiwa na maana kwamba hawa ni viumbe wawili tofauti kabisa kimaumbile.

      Kimaumbile mwanamke na mwanaume hutofautiana katika kufikiri, hisia, kuyatazama mambo, kupokea taarifa, upendo, utashi na shukurani. Mwanamke hujali sana upendo, yaani kupendwa kuliko ilivyo kwa wanaume. Mwanamke huridhika na yuko tayari kuvumilia ‘yasiyovumilika’ kama anahisi kwamba anapendwa na mwanaume. Ni jambo la kushangaza sana kwamba, mwanamke anapoambaiwa ‘nakupenda’ huwa amepewa zawadi kubwa sana na kujisikia kuwa mshindi katika mahusiano.

      Wanawake huwa wanaamini katika kusikilizwa zaidi kuliko kupewa ufumbuzi. Ndio maana wanawake wanapokuwa pamoja wakipeana ushauri na kupeana moyo kuhusu matatizo ya kimahusiano yanayowakabili, hawatafuti ufumbuzi bali kutaka wenzao wawasikilize na kuwa pamoja nao katika madhila yao.

      Mwanamke anaposema jambo ambalo linamkera kumwambia mumewe au mpenzi wake, sio kwamba anataka apatiwe suluhisho, la hasha. Anaposema jambo hilo anategemea kusikia mume au rafiki akionesha kusikiliza au kujali na sio ufumbuzi. Kwa bahati mbaya wanaume huwa wanadhani wanawake hao wanatafuta ufumbuzi kwa yale wanayoyaeleza.

      Kwa mfano:

      Mwanamke anapomwambia mumewe au rafiki yake, “siku hizi naona kazi zimenizidi sana” hategemei kupewa ufumbuzi wa hilo, badala yake anataka kusikia mwanaume aua rafiki yake akichangia katika hisia (Kumbuka mwanamke hujali zaidi hisia). Katika hili kwa bahati mbaya mwanaume atasema, “punguza baadhi ya kazi” au “labda utafute msichana wa kazi” au “na wewe unajiumiza bure, kazi nyingine hazina hata maana…..”

      Kwa kuwa mwanaume ni mtu wa ufumbuzi tu atadhani ndicho mkewe anachohitaji, wakati ukweli ni kwamba, mkewe anahitaji kusikilizwa tu- anahitaji mawasiliano. Mwanamke hapa angefurahi kusikia, “pole sana mke wangu, hebu njoo nikukumbatie kidogo….” Angefurahi kwa sababu anachotaka ni kusikilizwa ambapo kwake ndio thamani yake.

      Wakati mwanamke anapozungumzia matatizo yenye kumtanza, mwanaume kwa bahati mbaya hudhani kwamba mwanamke huyo anamlaumu yeye au anatafuta ufumbuzi wa matatizo hayo kutoka kwake. Kwa hiyo kwa kadiri mwanamke anavyokuwa na matatizo zaidi ndivyo ambavyo mwanaume anajihisi kulaumiwa. Mwanaume hajui kwamba kimaumbile mwanamke anapozungumzia matatizo au hofu zinazomkabili huwa anataka kusikilizwa zaidi kuliko kutafuta ufumbuzi.

      Mwanaume hajui kwamba mwanamke hujisikia ahueni kubwa kusikia tu jibu la ‘ahaa’ au ‘oh, kumbe’ kutoka kwa mwanaume, linatosha kabisa kumpa ahueni mwanamke.

    2. Study Abroad

    3. #2
      Purple's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2012
      Location : mjini
      Posts : 1,795
      Rep Power : 726
      Likes Received
      607
      Likes Given
      415

      Default §§

      Natamani huu mchinese wangu ungekua na kitufe cha 'like' however pokea like 100 kutoka kwangu!
      Women are emotional oriented while men are physical oriented.,when a woman approaches you with her propblems it doesn't necesarily mean she wants solutions,she just want sympathy and understanding!
      HorsePower and Mtambuzi like this.

    4. #3
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6888
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Najua kuna ukweli hapo tena mkubwa sana.Lakini hapo kwenye kupendwa nina doubt,inawezekana binadamu wote wawili yaani mwanamke na mwanaume hatujijui vyema au tunabadilika kimtazamo na kihisia kulingana na mazingira au kuna tofauti kati ya binadam mmoja mpaka mwingine jambo linalopelekea hizi tafiti zisiwe za jumla au haziaply kwa kila mtu.Nimesema hivyo nikiwa ninamaana kuwa siku hizi sidhani kama ukimwonesha mwanamke UPENDO anakuelewa,nazungumza hayo kutokana na uzoefu.Huenda kila mwanamke ana jambo lake tofauti linalomvutia tofauti na mwanamke mwingine!

    5. #4
      HEART's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th November 2011
      Location : kijitonyama
      Posts : 1,202
      Rep Power : 2732
      Likes Received
      462
      Likes Given
      128

      Default

      Quote By Purple
      Natamani huu mchinese wangu ungekua na kitufe cha 'like' however pokea like 100 kutoka kwangu!
      Women are emotional oriented while men are physical oriented.,when a woman approaches you with her propblems it doesn't necesarily mean she wants solutions,she just want sympathy and understanding!
      So so truue..ndo hapo utakuta mwanaume anasema wanawake ni head ache na walalamishi kumbe wala..kinacho hitajika ni kitu kdh tu.Sympathy..

    6. #5
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6888
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default

      Quote By HEART
      So so truue..ndo hapo utakuta mwanaume anasema wanawake ni head ache na walalamishi kumbe wala..kinacho hitajika ni kitu kdh tu.Sympathy..
      Hawa wanawake wanaozungumza haya ni tofauti sana na tunaokutana nao mtaani!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Kunta Kinte's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 2,560
      Rep Power : 2533
      Likes Received
      595
      Likes Given
      760

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Mkuu Mtambuzi, nakubaliana na wewe kwa baadhi tu ya wanawake, wengi wao, narudia tena, wengi wao, wanachopenda kusikia toka kwako ni kitu gani utamfanyia- siku hizi wenyewe wana msemo wao 'hapendwi mtu, pochi lako tu', ni ATM kwa kwenda mbele. Sasa wewe akueleza tatizo lake umuambie ‘ahaa’ au ‘oh, kumbe’ uone kama kesho atatokea
      Mtambuzi likes this.
      Have patience with all things, but chiefly have patience with yourself.- Saint Francis de Sales

    9. #7
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By Kunta Kinte
      Mkuu Mtambuzi, nakubaliana na wewe kwa baadhi tu ya wanawake, wengi wao, narudia tena, wengi wao, wanachopenda kusikia toka kwako ni kitu gani utamfanyia- siku hizi wenyewe wana msemo wao 'hapendwi mtu, pochi lako tu', ni ATM kwa kwenda mbele. Sasa wewe akueleza tatizo lake umuambie ‘ahaa’ au ‘oh, kumbe’ uone kama kesho atatokea
      Kunta Kinte kwa bahati mbaya sana kama unasoma makala zangu juu ya ndoa huwa sizungumzii wanawake wanaowapenda wanaume kwa kuangalia wanachomiliki, hapa nazungumzia wanawake wanaoingia kwenye ndoa bila kuangalia kile mwanaume anachomiliki. Kama ningekuwa nawazungumzia hao wanaosema 'hapendwi mtu, pochi lako tu', basi lugha isingekuwa hii niliyoizungumza hapa.....................
      Kunta Kinte and Yummy like this.

    10. #8
      Uncle Jei Jei's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 446
      Rep Power : 513
      Likes Received
      70
      Likes Given
      3

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Its true 100%! Wakati nasoma makala hii, nilikuwa na unganisha na matukio yawa-dada ambao nimewahi kuwa nao karibu nikauona ukweli!
      Mtambuzi likes this.

    11. #9
      Eiyer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2011
      Posts : 8,909
      Rep Power : 6888
      Likes Received
      2734
      Likes Given
      34

      Default

      Quote By Mtambuzi
      Kunta Kinte kwa bahati mbaya sana kama unasoma makala zangu juu ya ndoa huwa sizungumzii wanawake wanaowapenda wanaume kwa kuangalia wanachomiliki, hapa nazungumzia wanawake wanaoingia kwenye ndoa bila kuangalia kile mwanaume anachomiliki. Kama ningekuwa nawazungumzia hao wanaosema 'hapendwi mtu, pochi lako tu', basi lugha isingekuwa hii niliyoizungumza hapa.....................
      Ila hawa ni wachache sana,nina miaka 3....Sijakutana na binti wa aina hii!
      Mtambuzi and Kunta Kinte like this.

    12. #10
      BADILI TABIA's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 14,547
      Rep Power : 5611
      Likes Received
      6208
      Likes Given
      2281

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      haya wanaume Mtambuzi keshawapa begipati, kazi kwenu.....

    13. #11
      TaiJike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2011
      Posts : 1,156
      Rep Power : 606
      Likes Received
      387
      Likes Given
      347

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Mtambuzi watu wengi wanahofia kuzungumzia matatizo yaliyopo ktk uhusiano wao. Na wanaona kuzungumzia tatizo kunaweza leta ugomvi, ukweli ni kwamba kuacha tatizo bila ufumbuzi wa njia ya mawasiliano mazuri hutengeneza tatizo.

      Kwa uelewa wangu wanaume wengi ni waoga kufanya makosa na baadaye kulaumiwa na wenzi wao au kuchekwa na hata kudharauliwa, ni vema kwa wanawake kutambua kuwa wanaume wanapenda sana kujilinda na matokeo ambayo yatawaletea aibu. Viumbe ninyi aina ya Adam mnapenda kupongezwa kwa mafanikio yenu, pia mnapenda kujiona kuwa mmefanikiwa kutufurahisha au kutupendezesha (ingawa si wote)
      Binafsi napenda kuonyeshwa kuwa ananijali kwa hali na mali.
      Mtambuzi and mbalu like this.
      * Nitashangaa kama hawa Watanzania watakataa kuasi. Kwanini wasiasi? * - Julius Kambarage Nyerere


    14. #12
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Asante Mtambuzi huwa sitoki kapa ninaposoma threads zako kila wakati huwa kuna mapya ya kujifunza. Natumaini wangu atakuwa amekusoma.
      Mtambuzi likes this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    15. #13
      shizukan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2011
      Posts : 1,160
      Rep Power : 842
      Likes Received
      533
      Likes Given
      219

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Mkuu Mtambuzi unakaribia kuharibu ndoa za watu. Hao unaowazungumzia ni wanawake wa kizungu ambao hisia zao zimejengwa kwa namna waliolelewa na sio malezi tunayopata kibongo-bongo.

      Akikwambia mtoto wa dada yake anapata shida kijijini usidhani anataka kuambiwa pole, maana yake anataka asikie ukisema aletwe aje akae na nyinyi. Na ujue hilo lisipofanywa ipo siku utapewa yote ya moyoni na ndio utajua alikuwa anarundika kusubiri wakati muafaka. "Kuna kitu ulishawahi kunisaidia zaidi ya hizo pole zako, ungejua nikitoka kazini napewa pole njia nzima hata usingepanua mdomo wako kuniambia maneno niliyoyazoea"
      Who Cares? likes this.
      "You know you are in Tanzania whenyour president believes traffic jam is anindicator of development!" Dr. Wilbrod Peter Slaa

    16. #14
      Yummy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Posts : 1,751
      Rep Power : 1894
      Likes Received
      1274
      Likes Given
      983

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By Eiyer
      Ila hawa ni wachache sana,nina miaka 3....Sijakutana na binti wa aina hii!
      Inaelekea njia zako si za kawaida aseee.....hebu badilisha muelekeo.
      God can heal a broken heart but you have to give him all the pieces.

    17. #15
      Yummy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Posts : 1,751
      Rep Power : 1894
      Likes Received
      1274
      Likes Given
      983

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By Eiyer
      Najua kuna ukweli hapo tena mkubwa sana.Lakini hapo kwenye kupendwa nina doubt,inawezekana binadamu wote wawili yaani mwanamke na mwanaume hatujijui vyema au tunabadilika kimtazamo na kihisia kulingana na mazingira au kuna tofauti kati ya binadam mmoja mpaka mwingine jambo linalopelekea hizi tafiti zisiwe za jumla au haziaply kwa kila mtu.Nimesema hivyo nikiwa ninamaana kuwa siku hizi sidhani kama ukimwonesha mwanamke UPENDO anakuelewa,nazungumza hayo kutokana na uzoefu.Huenda kila mwanamke ana jambo lake tofauti linalomvutia tofauti na mwanamke mwingine!
      Eiyer hebu jaribu kudumisha upendo kwa mpenzi wako uone kitakachotokea......ukiona ndivyo sivyo basi ujue umelamba galasha simpo!!!
      God can heal a broken heart but you have to give him all the pieces.

    18. #16
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By TaiJike
      Mtambuzi watu wengi wanahofia kuzungumzia matatizo yaliyopo ktk uhusiano wao. Na wanaona kuzungumzia tatizo kunaweza leta ugomvi, ukweli ni kwamba kuacha tatizo bila ufumbuzi wa njia ya mawasiliano mazuri hutengeneza tatizo.

      Kwa uelewa wangu wanaume wengi ni waoga kufanya makosa na baadaye kulaumiwa na wenzi wao au kuchekwa na hata kudharauliwa, ni vema kwa wanawake kutambua kuwa wanaume wanapenda sana kujilinda na matokeo ambayo yatawaletea aibu. Viumbe ninyi aina ya Adam mnapenda kupongezwa kwa mafanikio yenu, pia mnapenda kujiona kuwa mmefanikiwa kutufurahisha au kutupendezesha (ingawa si wote)
      Binafsi napenda kuonyeshwa kuwa ananijali kwa hali na mali.

      TaiJike kitu kimoja mbacho baadhi ya wanaume hawakijui ni kwamba wanawake wengi ni kama wasomi wa Saikolojia kwa sababu wanajua kushauriana na kupeana moyo kuhusu mahusiano yao ambayo yamekwenda kombo...... Kwa mfano unaposoma baadhi ya thread hapa zinazowekwa na wanawake kuelezea madhila yao, utaona, wakati wanaume wengi wataishia kusema tu "Pole dada." Lakini wanawake kwa asilimia kubwa wataonesha kuguswa na mkasa uliompata mwenzao na hata kutolea mfano yale waliyoshuhudia au yaliyowakuta ambayo yanafanana na yaliyomkuta mwenzao..........na mwishoni humfariji.

      Mara nyingi wanapojadili masuala haya huwa hawafichani lolote na hakuna mwenye kuona aibu au hofu kusema yale yanayomghasi. Hii ni kwa sababu wanawake huw akimaumbile wanaamini katika kusaidia na kusaidiwa, huwa hawaoni ubaya wa kuwasaidia wenzao walio katika tafrani ya kimahusiano
      FirstLady1 likes this.

    19. #17
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,089
      Rep Power : 27012
      Likes Received
      8204
      Likes Given
      17307

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By shizukan
      Mkuu Mtambuzi unakaribia kuharibu ndoa za watu. Hao unaowazungumzia ni wanawake wa kizungu ambao hisia zao zimejengwa kwa namna waliolelewa na sio malezi tunayopata kibongo-bongo.

      Akikwambia mtoto wa dada yake anapata shida kijijini usidhani anataka kuambiwa pole, maana yake anataka asikie ukisema aletwe aje akae na nyinyi. Na ujue hilo lisipofanywa ipo siku utapewa yote ya moyoni na ndio utajua alikuwa anarundika kusubiri wakati muafaka. "Kuna kitu ulishawahi kunisaidia zaidi ya hizo pole zako, ungejua nikitoka kazini napewa pole njia nzima hata usingepanua mdomo wako kuniambia maneno niliyoyazoea"
      Mkuu shizukan , hivi katikam mfano wangu kuna mahali nilizungumzia habari ya ugonjwa kweli........ mimi nimezungumzia maswala ya kawaida sana ambayo yanahitaji a little bit comfort ...... sasa mwenzangu unakuja na kesi za ugonjwa tena. Duh! Kwa kesi kama hizo za mambo ya ugonjwa zinakuwa na namna yake ya ku-handle, inahitaji thread maalum juu ya hilo.
      Quote By Mtambuzi
      Kwa mfano:
      Mwanamke anapomwambia mumewe au rafiki yake, “siku hizi naona kazi zimenizidi sana” hategemei kupewa ufumbuzi wa hilo, badala yake anataka kusikia mwanaume aua rafiki yake akichangia katika hisia (Kumbuka mwanamke hujali zaidi hisia). Katika hili kwa bahati mbaya mwanaume atasema, “punguza baadhi ya kazi” au “labda utafute msichana wa kazi” au “na wewe unajiumiza bure, kazi nyingine hazina hata maana…..”

      Kwa kuwa mwanaume ni mtu wa ufumbuzi tu atadhani ndicho mkewe anachohitaji, wakati ukweli ni kwamba, mkewe anahitaji kusikilizwa tu- anahitaji mawasiliano. Mwanamke hapa angefurahi kusikia, “pole sana mke wangu, hebu njoo nikukumbatie kidogo….” Angefurahi kwa sababu anachotaka ni kusikilizwa ambapo kwake ndio thamani yake.

    20. #18
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 14,946
      Rep Power : 3697
      Likes Received
      3572
      Likes Given
      5738

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Asante sana Mtambuzi unajitahidi sana kutupa mafundisho ya mahusiano
      Tushindwe wenyewe
      Mtambuzi likes this.
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..

    21. #19
      mbalu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Location : Ntuzu
      Posts : 214
      Rep Power : 395
      Likes Received
      98
      Likes Given
      68

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Komejaga ngosha naona sasa pumu imepata mpumuaji na kama ni upele tayari una mkunaji, napenda sana darasa lako Mtambuzi obhe'ja nkoi.
      Mtambuzi likes this.
      Ong'wizukuru Shimba nawe Shimba.

    22. #20
      mwaJ's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th September 2007
      Location : Nowhere
      Posts : 3,442
      Rep Power : 14606
      Likes Received
      2277
      Likes Given
      1497

      Default Re: Wanaume: Mnapokosea kudhani mnawaelewa wanawake………!

      Quote By shizukan
      Mkuu Mtambuzi unakaribia kuharibu ndoa za watu. Hao unaowazungumzia ni wanawake wa kizungu ambao hisia zao zimejengwa kwa namna waliolelewa na sio malezi tunayopata kibongo-bongo.

      Akikwambia mtoto wa dada yake anapata shida kijijini usidhani anataka kuambiwa pole, maana yake anataka asikie ukisema aletwe aje akae na nyinyi. Na ujue hilo lisipofanywa ipo siku utapewa yote ya moyoni na ndio utajua alikuwa anarundika kusubiri wakati muafaka. "Kuna kitu ulishawahi kunisaidia zaidi ya hizo pole zako, ungejua nikitoka kazini napewa pole njia nzima hata usingepanua mdomo wako kuniambia maneno niliyoyazoea"
      Mkuu sikubaliani nawe hata kidogo! Yaan kwa jinsi ulivyoeleza, inaelekea una mke mkorofi sana.
      Mtambuzi likes this.
      “Anyone who has never made a mistake has never tried anything new” -
      Albert Einstein

    23. FemaTV & Radio
    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...