Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

    Report Post
    Page 1 of 8 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 154
    1. #1
      Chal's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th October 2010
      Posts : 113
      Rep Power : 460
      Likes Received
      45
      Likes Given
      4

      Default Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      habari!
      Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 34, ni mwanafunzi wa Masters katika chuo kimoja hapa nchini. Nimehitimu chuo kikuu UCLAS (kwa sasa Ardhi University) mwaka 2008.Wakati nipo chuoni mwaka wa kwanza nilitokea kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi mwenzangu,mahusiano ambayo mwanzoni sikuona kama yangefika mbali kwani hata jinsi yalivyoanza ilikuwa katika mazingira ambayo hakuna hata mmoja wetu aliyetarajia.

      Tulihitimu chuo mwaka 2008 bahati nzuri kila mmoja wetu akapata kazi ingawa ni mikoa tofauti. Mara kadhaa nilimwambia umuhimu wa kuachana kwani nilihisi kuwa sitakuwa na furaha katika familia kama tutaoana lakini alipinga na kulia sana akidai kuwa yeye ananipenda sana. Nakumbuka wakati tuko chuoni alitaka hata kuacha chuo kwasababu yangu. Sikuwa tayari kuona hili linatokea hivyo niliendelea na mahusiano naye nikitafuta namna nitakavyoachana naye kwa amani.

      Tuliendelea na mahusiano hayo ingawa sikuwa na furaha nayo na bahati mbaya niseme mwezi februari mwaka huu amenambia ana ujauzito wangu. Sifikirii kabisa suala la yeye kutoa mimba kwani kwa umri wangu nataka kuwa na mtoto. Nakumbuka katika mahusiano yetu sikuwahi kuishi naye kama mke wangu mtarajiwa hivyo mambo ninayopenda mke wangu awe nayo na tabia ninazopenda wala sikumuhimiza ayafanye.

      Naomba ushauri nifanyeje nimechanganyikiwa, sitaki kuwa na watoto wa mama tofauti tofauti na pia nataka sana mtoto wake azaliwe salama?

      Last edited by Chal; 12th June 2012 at 20:28.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Zinduna's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th November 2011
      Location : Mzizima
      Posts : 1,239
      Rep Power : 11041
      Likes Received
      1441
      Likes Given
      2026

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Duh! Mtoto wa nje ya ndoa huyoo yu aja ...........Kama kawaida ya wanaume wa siku hizi

    4. #3
      Gurta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th September 2010
      Location : Mang'ola
      Posts : 1,944
      Rep Power : 907
      Likes Received
      374
      Likes Given
      483

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Toka 2008 na kapata ujauzito mwaka huu, hiyo ni good 5 years. Gaademu...
      FirstLady1, FP, Maty and 1 others like this.

    5. #4
      andishile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 610
      Rep Power : 482
      Likes Received
      151
      Likes Given
      311

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      mungu wa siku hizi ni vodafasta,wewe mtelekeze huyo dada uone malipo yako chapchap!
      Sal, LD, Maty and 2 others like this.

    6. #5
      Osaka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Location : Morogoro
      Posts : 1,099
      Rep Power : 620
      Likes Received
      269
      Likes Given
      162

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Pole! Ulipokuwa unaingia ktk soft center pekupeku ulitarajia nini mkuu? after all, una uhakika gani kuwa hiyo mimba ni yako?


    7. #6
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,175
      Rep Power : 21618
      Likes Received
      13496
      Likes Given
      17794

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      haukuwahi kusikia matangazo ya kutumia kifudusi(condoms)??????????
      Sal, daughter, FirstLady1 and 9 others like this.
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    8. #7
      andishile's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 610
      Rep Power : 482
      Likes Received
      151
      Likes Given
      311

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      muoe huyo dada,kwanza yaonyesha anakupenda sana,ina maana ukimuoa hawezi kuwa na macho ya nje,mtadumu ktk penzi,na mtalea mwanenu pamoja!

    9. #8
      Chal's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th October 2010
      Posts : 113
      Rep Power : 460
      Likes Received
      45
      Likes Given
      4

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Quote By andishile
      mungu wa siku hizi ni vodafasta,wewe mtelekeze huyo dada uone malipo yako chapchap!
      sifikirii kumtelekeza mtoto lakini pia sifikirii kumuoa mama yake mbaya zaidi sihitaji kuwa na watoto wa mama tofauti.

    10. #9
      Yummy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Posts : 1,751
      Rep Power : 1895
      Likes Received
      1274
      Likes Given
      983

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Hii kali,yani ww huna mapenzi na huyo binti lakini uliweza kupiga kavu???!! Sasa unataka msaada wa nn?!
      LD and Ipycalypse like this.

    11. #10
      Preta's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 28th November 2009
      Location : yaeda chini
      Posts : 14,783
      Rep Power : 15113
      Likes Received
      7241
      Likes Given
      6930

      Default

      Quote By andishile
      muoe huyo dada,kwanza yaonyesha anakupenda sana,ina maana ukimuoa hawezi kuwa na macho ya nje,mtadumu ktk penzi,na mtalea mwanenu pamoja!
      lakini jamaa hampendi....raha ya ndoa kupendana.....mapenzi ya kuoneana huruma hayafai....
      kaka mwenye thread.....nakushauri fuata moyo wako.....
      big-diamond, kapotolo and YNNAH like this.

    12. #11
      Sokwe Mjanja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th July 2009
      Posts : 473
      Rep Power : 12063
      Likes Received
      205
      Likes Given
      29

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Mbona maelezo yako umeyatoa vizuri tu na umeonesha kabisa unachokitaka, hufikirii kutoa mimba, unataka mtoto azaliwe salama, hutaki kuwa na watoto wa mama tofauti( hufikirii kuja kuzaa na mwingine) sasa unaomba ushauri upi kiongozi?
      Kajitambulishe kwa binti haraka iwezekanavyo. Huyo ndio kashakuwa mkeo tena, kama uliweza kuwa nae kwa miaka 5 tena mko mikoa tofauti nini shida sasa rafiki?
      Peleka posa, toa mahari kuwa na binti hasa kipindi hiki yu-mimbani, anahitaji sana ukaribu wako aisee, hata kama harusi itasubiri kidogo ila usithubutu kutoa hiyo mimba wala kumtelekeza huyo mama. Amekusaidia kukupunguzia mahamu yako wakati wa chuo umjali sasa na yeye please. Tena una bahati unasema anakupenda sana, huoni fahari kuwa na mke anaekupenda sana? Angalia usije kupata gume gume likaja kukusumbua katika ndoa
      Sal, Maty, Kaunga and 2 others like this.

    13. #12
      Chal's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th October 2010
      Posts : 113
      Rep Power : 460
      Likes Received
      45
      Likes Given
      4

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Quote By Osaka
      Pole! Ulipokuwa unaingia ktk soft center pekupeku ulitarajia nini mkuu? after all, una uhakika gani kuwa hiyo mimba ni yako?
      Inawezekena uko sahihi kabisa osaka, lakini kwasasa hilo halina mjadala kwani imeshatokea.

    14. #13
      Elizabeth Dominic's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 7th December 2007
      Posts : 2,741
      Rep Power : 5465
      Likes Received
      1963
      Likes Given
      2652

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Jaribu kumpenda kama akupendavyo, kumpata mwenye mapenzi ya kweli siku hizi si rahisi.........maana umesema una miaka 34, ujue wakati haukusubiri wewe na maji yakishamwagika hayazoleki.......just be a man about it
      BE RESPECTED............DEMAND RESPECT

    15. #14
      Chal's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th October 2010
      Posts : 113
      Rep Power : 460
      Likes Received
      45
      Likes Given
      4

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Quote By Zinduna
      Duh! Mtoto wa nje ya ndoa huyoo yu aja ...........Kama kawaida ya wanaume wa siku hizi
      Nachelea kusema ni mtoto wa nje ya ndoa kwani bado sijaoa.
      Nawaza kutooa kabisa ili nisiwe na mke niseyekuwa na furaha naye na pia nisiwe na watoto wenye mama tofauti tofauti

    16. #15
      MwalimuZawadi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2007
      Posts : 623
      Rep Power : 724
      Likes Received
      50
      Likes Given
      3

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Maswali mengine bana? Unamajibu mkuu, chagua majibu 3 kati ya haya yatakupa mwelekeo
      a. Hutaki mtoto wa mama tofauti
      b. Humpendi mwanamke
      c. Unataka mtoto azaliwe salama
      d. Hutaki kutoa mimba
      e. Unataka mtoto
      Sal, MadameX, Tasia I and 5 others like this.
      Sent from my Nokia rinGo using JamiiForums

    17. BAK
      #16
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,666
      Rep Power : 44978
      Likes Received
      8395
      Likes Given
      8376

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Priority yako kwa sasa ni kuhakikisha ujauzito wake uko salama mpaka hapo atakapojifungua kisha kutoa pesa za matunzo ya mtoto bila kukosa na kuvunja kabisa mahusiano ya kimapenzi na huyo mdada kabla hajapata mimba nyingine...Labda mtoto akizaliwa unaweza kubadili mawazo na kuamua kuishi naye kama mke.
      Maty, Kongosho and Ipycalypse like this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    18. #17
      Doreen22's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd June 2012
      Posts : 478
      Rep Power : 605
      Likes Received
      69
      Likes Given
      7

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Wewe ***** kweli, yaani kukutishia kuwa ataacha Chuo, ndio kisa cha kuendelea kuwa naye!, kwanini na wewe hukumtishia kama ataendelea kukung'ang'ania utahama Chuo mbali ya Tz, eti aache Chuo, thubutu, alikuja Chuo kusoma au kukufuata wewe!, angejuana na maisha yake na familia yake, alikosa kabisa wengine hapo Chuoni, yaani unalo, huruma yako, itakukomesha, na kisa mpaka cha kumvulia nguo or hasa kuendelea kumvulia nguo, hukujua hilo lingeweza kutokea, tena kwa yeye kujitegesha kabisa, ilitakiwa usido naye kabisa, toka ulipoanza kumweleza ukweli kuwa hufeel kuwa naye, ungeacha kudo naye na utafute Girlfriend mwingine, amuone kabisa akija kwako kukupikia na kukusafishia nyumba, unafikiri angekuganda tena, na huyo GF wako ungemweleza ukweli, ili asibabaishwe na maneno ya wachonganishi na wambeya, but nakushauri usimwoe, kama vipi, mtoto akae na wazazi wenu or wako, oa unayemtaka, usijikoseshe raha katika ndoa my Bro.
      Ipycalypse and Jestina like this.

    19. #18
      mashambaJr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th May 2012
      Location : Loading....
      Posts : 368
      Rep Power : 426
      Likes Received
      58
      Likes Given
      27

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Inaelekea binti huyo anakupenda kwa dhati.pili binti anaujauzito wako hivi Mungu unataka akuoneshe nini ili ujue huyo ndio chaguo lako.
      Pole kwa mawazo yako finyu ambayo hayana uwezo wa kupambanua mambo kwani we ulivyo ingia kwenye uhusiano ulikuwa unamaana gani licha ya hivyo mlipo kuwa faragha ulisahau kutumia dawa ya penzi.
      Sina mengi ya kuandika maana Ndoa umeitaka mwenyewe.

    20. #19
      Chal's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th October 2010
      Posts : 113
      Rep Power : 460
      Likes Received
      45
      Likes Given
      4

      Default Re: Nimempa ujauzito binti nisiyempenda....nifanye nini?

      Quote By Zinduna
      Duh! Mtoto wa nje ya ndoa huyoo yu aja ...........Kama kawaida ya wanaume wa siku hizi
      Nachelea kusema ni mtoto wa nje ya ndoa kwani bado sijaoa.
      Nawaza kutooa kabisa ili nisiwe na mke niseyekuwa na furaha naye na pia nisiwe na watoto wenye mama tofauti tofauti

    21. #20
      Osaka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Location : Morogoro
      Posts : 1,099
      Rep Power : 620
      Likes Received
      269
      Likes Given
      162

      Default

      Quote By Chal
      Inawezekena uko sahihi kabisa osaka, lakini kwasasa hilo halina mjadala kwani imeshatokea.
      Ok! Huyo mdada yaelekea anakupenda sana, na alikuwa tayari kuacha chuo kwa ajili yako; Tatizo ni nini hasa?

    Page 1 of 8 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...